ASKOFU DKT.SHOO AKEMEA UPOTOSHAJI MCHANGO WA RAIS SAMIA KWA TAASISI ZA DINI

July 04, 2025 Add Comment

Mwenyekiti wa CCT, Askofu Dkt. Fredrick Shoo amesema kuwa baadhi ya watu kwa sababu zao binafsi wamekuwa wakidai kuwa msaada wa Rais, Dkt. Samia ni sehemu ya hongo, madai ambayo yamekuwa yakimuumiza sana kama kiongozi wa dini. Niendelee kumsihi Rais Samia asirudishwe nyuma na watu hao bali aendelee kuwa na hofu ya Mungu katika kusaidia huduma za kiroho nchini. 

Askofu Mkuu Shoo amebainisha hayo Julai 03, 2025 Jijini Dodoma wakati wa Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Kikristo nchini Tanzania - CCT ambapo Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko alimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano huo.

BENKI YA CRDB YASHINDA TUZO YA DHAHABU YA KIMATAIFA YA UWEKEZAJI KATIKA JAMII KUPITIA CRDB MARATHON

July 04, 2025 Add Comment

 

Benki ya CRDB imeshinda tuzo ya dhahabu ya Kimataifa ya Uwekezaji katika Jamii (International CSR Awards 2025) kupitia mbio zake za kimataifa ya CRDB BANK International Marathon.

Tuzo hii ya hadhi ya juu imetolewa na CSR Society, shirika huru la kimataifa linalotambua na kuenzi mashirika yenye juhudi za uwajibikaji wa kijamii duniani kote lenye makao makuu yake nchini Uingereza.
Mwaka huu, Benki ya CRDB ilikuwa miongoni mwa washiriki 300 walioshindana kutoka nchi mbalimbali duniani na kushinda tuzo hiyo kwa kuonyesha ubunifu mkubwa katika uwezeshaji wa kijamii katika nyanja tofauti.

Akiiwakilisha Benki ya CRDB na kupokea tuzo na cheti cha ushindi, Afisa Uwekezaji wa Jamii, Natalia Tuwano amesema tuzo hii inaipa Benki ya CRDB heshima na hadhi ya juu katika kuiwezesha jamii na makala yake kuhusu jambo hilo kubwa yatachapishwa na Jarida la Viongozi wa Uwezeshaji Jamii Duniani – rejeleo la kimataifa la mazoea bora ya uwajibikaji wa kijamii. Hii pia inaruhusu benki kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Green World Awards mwakani ujao.
“CRDB Bank International Marathon ni mfano wa jinsi juhudi za kijamii zinavyoweza kuleta mabadiliko chanya na kuimarisha jamii zetu,” amesema Natalia. “Tunawashukuru CSR Society kwa kutambua jitihada zetu na tunaahidi kuendelea kutekeleza mipango inayolenga maendeleo endelevu ya kijamii.”

Benki ya CRDB imekuwa mstari wa mbele katika kukuza afya, elimu, uendelevu wa mazingira, na mshikamano wa kijamii kupitia kampeni hii ambayo imevutia maelfu ya watu kutoka makundi mbalimbali.

UDOM Yaja na Mashine ya Kuuza Vinywaji Inayojiendesha

July 03, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kupitia Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu, kimebuni mashine ya kisasa ya kuuza vinywaji baridi inayojiendesha yenyewe bila kuhitaji uwepo wa mtu kwa ajili ya kutoa huduma kwa mteja.

NEEC WAJA NA FURSA ZA KIUCHUMI KATIKA MAONEHO YA 49 YA KIMATAIFA YA BIASHARA (SABA SABA)

July 03, 2025 Add Comment
Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) linashiriki katika maonesho ya 49 ya kimataifa ya Biashara katika banda la Ofisi ya Waziri Mkuu na watakuwepo hapo kipindi chote cha maonesho ili kuwawezesha Watanzania.

MRADI WA BOMBA LA GESI NTORYA–MADIMBA KUGHARIMU SHILINGI BILIONI 120

July 03, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limesaini mkataba wa makubaliano na kampuni ya China ya CPP na CPTDC kwaajili ya ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka Ntorya hadi Madimba mkoani Mtwara kwa kipindi cha miezi 12.