WAZIRI DKT.NCHEMBA: SH.TRILION 56.49 KUTEKEKEZA BAJETI 2025/2026

June 12, 2025 Add Comment






Na Saidina Msangi, WF, Dodoma



Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), anamewasilisha Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali, ambapo ameliomba Bunge ridhaa ya kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 56.49 kwa Mwaka wa Fedha 2025/26.



Dkt. Nchemba ameomba ridhaa hiyo bungeni jijini Dodoma, wakati akiwasilisha mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2025/26, ambapo bajeti hiyo inatarajiwa kugharamiwa na mapato ya ndani ya shilingi trilioni 40.47, misaada shilingi trilioni 1.07 na mikopo ya shilingi trilioni 14.95.



‘‘Kati ya mapato ya ndani yanayotarajiwa, mapato ya kodi ni shilingi trilioni 32.31, mapato yasiyo ya kodi shilingi trilioni 6.48, na mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 1.68. Aidha, mikopo inajumuisha shilingi trilioni 6.27 kutoka vyanzo vya ndani na shilingi trilioni 8.68 kutoka vyanzo vya nje’’, alifafanua Mhe. Nchemba.



Alieleza kuwa makadirio ya matumizi ya Serikali ya shilingi trilioni 56.49 kwa mwaka 2025/26 yanajumuisha Stahiki za watumishi na michango ya pensheni (Serikali Kuu) shilingi trilioni 9.17 pamoja na ununuzi wa bidhaa na huduma shilingi trilioni 5.58









Aliongeza kuwa matumizi mengine ni malipo ya riba za mikopo shilingi trilioni 6.49; na ruzuku kwa taasisi za Serikali, mashirika ya umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 22.17 na shilingi trilioni 7.72 kugharamia malipo ya mtaji kwa deni la ndani na nje.



‘‘Katika Mwaka wa Fedha 2025/26 Serikali inatarajia kuongeza kasi ya ukuaji wa Pato Halisi la Taifa kufikia asilimia 6.0 mwaka 2025 kutoka ukuaji wa asilimia 5.5 mwaka 2024, kuendelea kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei na kuhakikisha kuwa unabaki kwenye wigo wa tarakimu moja ya wastani wa asilimia kati ya 3.0 - 5.0 katika muda wa kati’’, alifafanua Mhe. Nchemba.



Aidha, Dkt. Nchemba alisema Serikali inatarajia kuongeza Mapato ya ndani kufikia asilimia 16.7 ya Pato la Taifa mwaka 2025/26 ikilinganishwa na asilimia 15.8 mwaka 2024/25 na mapato ya kodi kufikia asilimia 13.3 ya Pato la Taifa mwaka 2025/26 kutoka asilimia 12.8 mwaka 2024/25.



Dkt. Nchemba alisema vipaumbele vya bajeti ya mwaka 2025/26 ni pamoja na kuendelea kutekeleza na kukamilisha miradi ya kielelezo na ile ya kimkakati, kuimarisha sekta za uzalishaji zenye matokeo chanya katika kukuza uchumi, kuimarisha rasilimali watu hususan katika sekta za huduma za jamii na kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji nchini ili kuvutia ushiriki wa sekta binafsi katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.



‘‘Maeneo mengine mahsusi ya vipaumbele ni pamoja na ugharamiaji wa Deni la Serikali; mishahara na stahiki za watumishi wa umma, pamoja na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya michezo kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya AFCON 2027. Aidha, nipende kuwafahamisha Watanzania kuwa Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 tutaugharamia kwa fedha zetu za ndani’’, alisema Mhe. Nchemba.



Aidha, Dkt. Nchemba alisema katika mwaka 2025/26, Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ukusanyaji wa mapato ikiwemo kuendelea kuhamasisha umma kuhusu kutoa na kudai risiti za malipo za kielektroniki za EFD na kuboresha utaratibu wa ukusanyaji wa mapato kutoka vyanzo vinavyosimamiwa na mamlaka za udhibiti.



‘‘Serikali itaendelea kuboresha Mfumo wa TAUSI ili kuhakikisha vyanzo vyote vya mapato vya Mamlaka za Serikali za Mitaa vinajumuishwa katika mfumo huo, kuongeza ufanisi wa mifumo ya ukusanyaji wa mapato ya mashirika, taasisi za umma na wakala za Serikali ili kuhakikisha gawio na michango stahiki inawasilishwa kwa wakati na kuendelea kutekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (MKUMBI)’’, alifafanua Mhe. Nchemba.



MABORESHO YA MIFUMO YA KODI



Dkt. Nchemba alisema Serikali inalenga kufanya maboresho ya mfumo wa kodi, ikiwemo baadhi ya viwango vya kodi, tozo na ada zinazotozwa chini ya sheria mbalimbali pamoja na kuboresha taratibu za ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya Serikali ili kuwa na mfumo wa kodi ambao ni tulivu na wa kutabirika unaolenga kuchochea shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ndani ya nchi.



Mapendekezo ya kurekebisha mfumo wa kodi kwa mwaka 2025/26 yanatarajiwa kuiongezea Serikali jumla ya shilingi milioni 4,260,023.77 ambapo baadhi ya mapendekezo hayo ni kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye viuatilifu vinavyotambulika kwa HS Codes 3808.61.00, 3808.62.00 na 3808.69.00, ili kuwapa unafuu wakulima ya kupata dawa za kuua wadudu mashambani na hivyo kuongeza uzalishaji wa mazao nchini.



Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye miamala ya ununuzi wa bima mtawanyo inayofanywa baina ya kampuni za bima na zile za bima mtawanyo ili kuongeza ushindani wa kampuni za ndani, kukuza Sekta ya Bima na kuhamasisha matumizi ya bima katika kukabiliana na majanga nchini.



Kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha asilimia 0 kwenye bidhaa za nguo zinazotengenezwa kwa kutumia pamba inayolimwa nchini kwa kipindi cha mwaka mmoja ili kuleta unafuu kwa wakulima wa pamba na viwanda vinavyotengeneza nguo nchini.



Kutoza kodi ya ongezeko la thamani kwa kiwango cha asilimia 0 kwenye mbolea inayozalishwa ndani ya nchi kwa kipindi cha miaka mitatu ili kuleta unafuu kwa wakulima na walaji hasa katika kipindi hiki ambacho dunia imetoka kwenye mdororo wa kiuchumi duniani.



Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye mafuta ya kula yanayozalishwa ndani ya nchi kwa kutumia mbegu zinazozalishwa nchini kwa muda wa mwaka mmoja ili kuendelea kuleta unafuu wa bei ya mafuta ya kula nchini.



Kufuta Msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani unaotolewa kwenye ununuaji na uingizaji wa gaming supply. Hatua hii inalenga kuleta usawa katika utozaji wa kodi kwa kuwa michezo mingine kama vile mpira wa miguu ipo katika wigo wa utozaji wa kodi ya ongezeko la thamani. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 322,022.5.



Kuweka sharti la msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye matairi ya trekta yanayotumika kwenye shughuli za kilimo yanayotambulika kwa HS Code 4011.70.00; dam liners zinazotambulika kwa Heading 39.20; forks (HS Code 8201.90.00); reki (HS Code 8201.30.00); na shoka (HS Code 8201.40.00) kutolewa baada ya kupata ridhaa ya Waziri mwenye dhamana ya masuala ya kilimo.



Kufuta msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani kwenye lami zinazotambulika kwa HS Code 2713.20.00 na 2715.00.00 ili kuendana na azma ya Serikali ya kupunguza misamaha isiyo na tija ili kulinda mapato ya Serikali na kupunguza matumizi yanayohusiana na utoaji wa misamaha ya kodi. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 85,606.2.



Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye magazeti yanayozalishwa nchini pekee ili kupunguza gharama za magazeti hayo na hivyo kuwezesha upatikanaji wa taarifa muhimu. Hatua hii inatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 1,274.4.



Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye gesi asilia inayouzwa kwenda kwenye vituo vya kushindilia gesi kwa ajili ya matumizi ya magari ili kuweka unafuu kwa wawekezaji, kuvutia uwekezaji wa vituo vya kusambazia gesi asilia iliyosindikwa kwenye magari na kupunguza utegemezi wa mafuta na uzalishaji wa hewa ya ukaa.



Kusamehe kodi ya ongezeko la thamani kwenye matanki na mitungi ya gesi ya kupikia zinazotambulika kwa HS Code 7311.00.10 pamoja na mitambo ya kuondoa hewa ukaa yenye HS Code 8417.80.00 inayotumika katika uzalishaji wa mikaa mbadala. Hatua hii inalenga kupunguza gharama za upatikanaji wa bidhaa hizi ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.



Kujumuisha masoko mtandao na huduma za masoko za kimtandao kwenye wigo wa tafsiri ya neno wakala wa huduma za kimtandao ili kutanua wigo wa kodi kwa kuweka ufafanuzi utakaopelekea kutatua changamoto zilizopo katika utozaji na usimamizi wa kodi ambapo tafsiri iliyopo sasa haijumuishi huduma hizo katika utozaji kodi. Hatua hii inatarajia kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi milioni 116,073.4.



Kuweka unafuu wa kutoza kodi ya mapato kwa kundi la pikipiki ya miguu miwili, pikipiki ya miguu mitatu (Bajaji) na magari ya kubeba mizigo yenye uzito usiozidi Kilogramu 500 ikiwemo Guta kwa kuweka utaratibu mpya wa kukadiria kodi ya mapato kwenye vyombo hivyo. Maboresho ya viwango vya kodi elekezi yanalenga kuweka unafuu wa kodi kwa kundi husika na hivyo kurahisisha utekelezaji wa sheria.



Kupunguza tozo ya ushuru wa huduma kutoka utaratibu wa sasa wa kutoza kiwango kisichozidi asilimia 0.3 ya pato ghafi kwenda kiwango mfuto cha asilimia 0.25 ya pato ghafi. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini pamoja na kuendana na masharti ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (MKUMBI).



Kupunguza kiwango cha ada ya ushuru wa hoteli (hotel levy) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 2. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini.



Kufuta ada za upakiaji (loading) na upakuaji (offloading) zinazotozwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa zinazohusiana na usafirishaji wa mizigo. Lengo la hatua hii ni kupunguza gharama za ufanyaji biashara na uwekezaji nchini ili kuendana na masharti ya Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara nchini (MKUMBI).



Kupunguza ada ya usajili wa pikipiki za biashara kutoka shilingi 340,000 hadi shilingi 170,000 kwa miaka mitatu ambapo ada husika italipwa wakati wa usajili wa awali pekee. Kupunguza ada ya leseni ya uendeshaji wa pikipiki, bajaji na guta kutoka shilingi 70,000 hadi shilingi 30,000.



KUGHARAMIA BIMA YA AFYA



Serikali inapendekeza kuanzisha vyanzo mbadala vya mapato ili kupunguza nakisi ya kibajeti kwa kufanya marekebisho katika sheria mbalimbali. Aidha inapendekezwa asilimia 70 ya mapato yatakayoongezeka ipelekwe kwenye Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI (ATF) na asilimia 30 ipelekwe kwenye Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa Wote. Marekebisho hayo ni kama ifuatavyo:



Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147 ili kuongeza ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vya kilevi vinavyozalishwa na vinavyoingizwa kutoka nje ya nchi kama ifuatavyo: shilingi 20 kwa bia zinazotambulika kwa Heading 22.03; shilingi 30 kwa mvinyo unaotambulika kwa Heading 22.04, 22.05, na 22.06; shilingi 50 kwa spirits na vinywaji vingine vinavyotambulika kwa Heading 22.08.



Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, SURA 147 ili kuongeza kiwango cha ushuru wa bidhaa kwenye huduma za mawasiliano ya kielektroniki kutoka asilimia 17 hadi asilimia 17.5.



Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Barabara na Mafuta, SURA 220 ili kutoza kiasi cha shilingi 10 kwa kila lita ya mafuta ya Petroli, Dizeli na Mafuta ya Taa pamoja na kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Madini, SURA 123 ili kutoza kiwango cha asilimia 0.1 kwenye thamani ya soko ya madini.



Kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Michezo ya Kubahatisha, SURA 41 ili kuongeza kiwango cha kodi kwenye zawadi ya ushindi (Winning tax) kwenye michezo ya kubashiri matokeo (sports betting) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 15; na kwenye michezo ya kasino ya ardhini (land based casino) kutoka asilimia 12 hadi asilimia 15.



Kutoza magari na mashine (heavy machines) zinazoingizwa kutoka nje ya nchi kama ifuatavyo: Shilingi 50,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kati ya 0 -1000; Shilingi 100,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 1001-1500; Shilingi 150,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 1501-2500; Shilingi 200,000 kwa magari yenye ukubwa wa injini (CC) kuanzia 2501 na zaidi; Shilingi 250,000 kwa mashine (Excavators, Bulldozers, Fork Lifts) zenye Heading 84.29 na 84.27.



Kutoza shilingi 500 kwa kila tiketi inayotolewa na mtoa huduma za usafirishaji kwa njia ya treni na kutoza shilingi 1000 kwa kila tiketi inayotolewa na mtoa huduma za usafirishaji kwa njia ya anga. Hatua hizi kwa pamoja zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa shilingi milioni 586,404.9.



KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA



Ili kuiwezesha nchi kuwa na sera bora za biashara na kuweka mazingira mazuri ya ufanyaji biashara baina ya wazawa na wageni, Serikali inatarajia kufanya marekebisho kwenye Sheria ya Utoaji wa Leseni za Biashara ikiwemo:



Kufuta kifungu cha 3(4) kinachozipa nguvu mamlaka za utoaji wa leseni za biashara kufunga biashara pale ambapo wafanyabiashara wamekiuka masharti ya Sheria husika. Lengo la hatua hii ni kuwaondolea kero wafanyabiashara na pia kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kutofunga biashara.



Kuongeza kifungu cha 8(7) ambacho kinampa mamlaka Waziri mwenye dhamana na masuala ya biashara kuainisha shughuli za kibiashara ambazo hazipaswi kufanywa na wageni. Utaratibu wa utekelezaji wa kifungu hiki utafanywa kupitia Amri (Order) itakayotolewa na Waziri ambayo itakua na orodha ya shughuli za kibiashara ambazo hazipaswi kufanywa na wageni.



Dkt. Nchemba alisema bajeti hii inaendeleza na kukamilisha utekelezaji wa miradi, Kuchochea uchumi shindani na shirikishi, kuimarisha uzalishaji wa bidhaa viwandani na utoaji huduma, kukuza uwekezaji na biashara, kuchochea maendeleo ya watu na kuendeleza rasilimali watu ili kuhakikisha ufikiwaji wa malengo ya Dira 2025.

SERIKALI KUNUNUA TANI LAKI 2 ZA MBOLEA VIWANDA VYA NDANI.

June 12, 2025 Add Comment


 -Dodoma

Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe amesema katika kuhakikisha wanalinda viwanda vya ndani Serikali imejipanga kununua mbolea tani laki 2 katika viwanda vya ndani na tani elfu 50 za chokaa kwaajili ya kuboresha shughuli za kilimo.

Waziri Bashe ameyasema hayo Jijini Dodoma Juni wakati akitoa taarifa juu ya Uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha Mbolea cha Itracom Fertilisers Limited utakaofanyika Juni 28,2025 ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi.

Ambapo amesema ununuzi huo wa Mbolea hautalenga kuathiri mfumo wa ruzuku unaoendelea kwani wao watapeleka zaidi maeneo yale ambayo mbolea hazitumiki kwa wingi ili Watanzania wahamasike kuzitumia na kuona matokeo.

"Ili kulinda viwanda vyetu vya ndani Serikali mwaka huu imeamua itanunua mbolea kutoka viwanda vya ndani tani laki 2 na tani elfu 50 zitanunuliwa nu za chokaa kwaajili ya shughuli za kilimo".

"Na pia Serikali itanunua hizi mbolea bila kuathiri mfumo wa ruzuku unaoendelea, ila zitakaponunuliwa tutazipeleka kwenye maeneo ambayo mbolea hazitumiki sana ili Watanzania waanze kutumia za viwanda vya ndani na kuona matoke yake".

Aidha amesema Nchi imekuwa ikiagiza karibu tani milioni 1.2 za mbolea kutoka nje lakini kwasasa kutokana na uwepo wa kiwanda hiki na uwekezaji wake mahitaji ya mbolea yatapatikana kutoka viwanda vya ndani.

Naye Mkurugenzi wa Kiwanda cha Itracom Fertilisers Limited Bwana Nduwimana Nazaire amesema kuwa wao kwa kushirikiana na Taasisi za Serikali kama vile TARI na TFRA mpaka sasa tayari kuna aina 14 ambazo kiwanda kinazalisha ambapo pia kiwanda kina uwezo wa kutengeneza mbolea kulingana na eneo,kulingana na zao na pia kulingana na hitaji la mkulima.

Na kuongeza kuwa kiwanda hicho kinazalisha mbolea mchanganyiko wa chumvi chumvi na malighafi za asili kama vile samadi na zinginezo.

Uzinduzi huu ni miaka mitatu na nusu toka uwekezaji huu kuanza kufanyika hapa Jijini Dodoma.


WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ZANZIBAR AZINDUA MAONYESHO YA MADINI LINDI

June 12, 2025 Add Comment

 

Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.

Na Fredy Mgunda, Ruangwa, Lindi.


Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Kaduara alisema thamani ya dhahabu imeendelea kupanda katika soko la dunia kutokana na athari za vita kati ya Urusi na Ukraine, ambako dhahabu inayozalishwa na Urusi imewekewa vikwazo kuingia katika masoko ya kimataifa.


"Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya 1996, pamoja na Sera ya Maendeleo ya Viwanda ya 1996–2020 na ile ya Viwanda Vidogo ya mwaka 2003, zipo kwenye mchakato wa kupitia upya kwa lengo la kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo ya kimkakati," alisema Kaduara.


Waziri huyo alibainisha kuwa miradi ya madini ni miongoni mwa miradi ya kimkakati nchini, ambayo inaendelea kufanyiwa tathmini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sera mpya itakayowezesha Watanzania kunufaika zaidi na sekta hiyo.


Lindi Yajitokeza Kama Kitovu cha Madini Nchini

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Zainab Telack, alisema mkoa huo umebarikiwa kuwa na rasilimali kubwa za madini ambazo tayari zimeanza kuwanufaisha wananchi moja kwa moja.


“Maonyesho haya yanafungua milango kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Yanachochea uchumi wa eneo hili na kuongeza thamani ya madini tunayochimba,” alisema RC Telack.


Aliongeza kuwa maonyesho ya awamu ya kwanza mwaka 2023 yalivutia wageni kutoka mataifa 14 na zaidi ya watu 6,000 walihudhuria, jambo lililoongeza hadhi ya Lindi kama eneo la kimkakati kwa shughuli za madini nchini.


“Kwa sasa tunaona ongezeko la wawekezaji, uboreshaji wa miundombinu na fursa za ajira, hali inayodhihirisha kuwa Lindi ni sehemu muhimu katika ajenda ya maendeleo ya taifa,” aliongeza.


Ongezeko la Wachimbaji na Teknolojia ya Uchimbaji

Kwa mujibu wa Mratibu wa Maonyesho hayo, Bw. Mwinjuma Mkungu, ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi mkoani Lindi, idadi ya wachimbaji imeongezeka kutoka 2,265 hadi 2,948 baada ya maonyesho ya kwanza, huku mitambo ya kisasa ya uchimbaji ikiongezeka pia.


“Tumeona ongezeko kubwa la wawekezaji na mapato ya serikali yameongezeka kwa asilimia 10.1 baada ya maonyesho ya awali. Hii inaonyesha mchango wa moja kwa moja wa maonyesho haya kwa uchumi wa taifa,” alisema Mkungu.


Alfred Chilumba, mchimbaji mdogo, alishuhudia mabadiliko makubwa baada ya kupata elimu kupitia maonyesho ya awali.


“Tulikuwa hatujui kama tunaweza kutumia mitambo ya kisasa. Maonyesho haya yametufungua macho,” alisema.


Anna Milanzi, mama lishe anayehudumu kwenye maonyesho hayo, alisema ametumia fursa ya ongezeko la wageni kuongeza kipato chake.


“Kwa siku za kawaida napika kilo 5 za unga, lakini leo nimepika kilo 15. Biashara imenoga,” alisema kwa furaha.


Maonyesho Yadumu kwa Siku Kadhaa

Maonyesho hayo ya siku kadhaa yanahusisha maonesho ya bidhaa za madini, teknolojia mpya za uchimbaji, warsha za kitaalamu, na majadiliano baina ya serikali, wawekezaji na wachimbaji wadogo.


Yamebeba kauli mbiu: “Madini na Uwekezaji wa Fursa za Kiuchumi Lindi – Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025”, yakisisitiza uhusiano kati ya maendeleo ya sekta ya madini na ushiriki wa wananchi katika mustakabali wa taifa.

KIKAO KAZI CHA KUPITIA NA KUTHIBITISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA TAIFA WA KUZUIA KUZAMA MAJI CHAFANYIKA DODOMA

June 12, 2025 Add Comment

 

 



Na Mwandishi wetu Dodoma.

Kikao kazi cha kupitia na kuthibitisha Rasimu ya Mpango Mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji chafanyika tarehe 11 Juni, 2025 katika ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na uokoa Jijini Dodoma.

Kikao hicho kimewashirikisha Wawakilishi kutoka Wizara, Taasisi na Idara za Serikali, Mashirika ya Kimataifa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mikoa mbalimbali ikiwemo Mwanza na Mara.

Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Kanali Selestine Masalamado amesema Nchi yetu imeendelea kukumbwa na matukio mbalimbali ya majanga ya asili na yanayosababishwa na shughuli za kibinadamu, ambayo yamekuwa na madhara makubwa kwa maisha ya wananchi hasa waishio pembezoni mwa fukwe wakiwemo Wazee, Vijana na Watoto, hivyo kuathiri maendeleo ya kijamii na kiuchumi.


Hata hivyo Kanali Masalamado amesema, Kutokana na majanga hayo, Serikali ilianza Mchakato wa kuandaa mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji mwaka 2024, kwa lengo la kuanzisha mfumo madhubuti na jumuishi wa kupunguza matukio ya vifo vinavyotokana na kuzama maji.










Ameongeza kwa kusema, Mkakati huu umeandaliwa kwa njia shirikishi, ukihusisha wadau kutoka sekta mbalimbali, ili kuhakikisha hatua zinazopendekezwa zinajengwa juu ya ushahidi wa kisayansi, uzoefu wa jamii, na muktadha halisi wa Tanzania.


Ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa washiriki wote kuchangia mawazo yao kwa weledi na uzalendo katika kupitia na kuboresha Rasimu ya Mkakati, ili ifikie viwango vinavyostahili kabla ya kuidhinishwa rasmi na kuanza kutekelezwa.

Mwisho

WAZAZI WAASWA KUTOCHANGIA MMOMONYOKO WA MAADILI KWA WATOTO

June 12, 2025 Add Comment


Serengeti-Mara.


Polisi Kata wa Kata ya Ikoma Wilaya ya Serengeti mkoani Mara Sajenti Emmanuel, ametoa wito kwa wazazi kutokuwa chanzo cha mmomonyoko wa maadili kwa watoto wao. 


Ametoa kauli hiyo wakati akitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wananchi wa kitongoji cha Momorogoro kijiji cha Robanda, kata ya Ikoma, katika mwendelezo wa kampeni ya Elimu ya Nyumba kwa Nyumba.


Katika maelezo yake, Sajenti Emmanuel amewakumbusha wazazi kuwa wanalo jukumu kubwa la kuiandaa vyema kesho ya watoto wao kwa kuwapatia malezi bora, ambayo yatawasaidia kuwa watu wenye tija na mafanikio katika nyanja za elimu, afya, na uchumi.

Aidha, aliwasisitiza wazazi kuwafundisha watoto wao kuvaa mavazi ya heshima yanayomstiri mtu, kudumisha usafi wa mwili, mavazi, na mazingira yanayowazunguka, kama njia ya kulinda maadili yao.


Aliwakumbusha wazazi kuwa urithi wa kudumu ambao wanaweza kuwaachia watoto wao ni elimu, alisema itawapatia maarifa muhimu katika kipindi chote cha ukuaji wao na kuwasaidia kuwa watu wanaofaa na kuheshimika katika jamii.