-Dodoma
Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe amesema katika kuhakikisha wanalinda viwanda vya ndani Serikali imejipanga kununua mbolea tani laki 2 katika viwanda vya ndani na tani elfu 50 za chokaa kwaajili ya kuboresha shughuli za kilimo.
Waziri Bashe ameyasema hayo Jijini Dodoma Juni wakati akitoa taarifa juu ya Uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha Mbolea cha Itracom Fertilisers Limited utakaofanyika Juni 28,2025 ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi.
Ambapo amesema ununuzi huo wa Mbolea hautalenga kuathiri mfumo wa ruzuku unaoendelea kwani wao watapeleka zaidi maeneo yale ambayo mbolea hazitumiki kwa wingi ili Watanzania wahamasike kuzitumia na kuona matokeo.
"Ili kulinda viwanda vyetu vya ndani Serikali mwaka huu imeamua itanunua mbolea kutoka viwanda vya ndani tani laki 2 na tani elfu 50 zitanunuliwa nu za chokaa kwaajili ya shughuli za kilimo".
"Na pia Serikali itanunua hizi mbolea bila kuathiri mfumo wa ruzuku unaoendelea, ila zitakaponunuliwa tutazipeleka kwenye maeneo ambayo mbolea hazitumiki sana ili Watanzania waanze kutumia za viwanda vya ndani na kuona matoke yake".
Aidha amesema Nchi imekuwa ikiagiza karibu tani milioni 1.2 za mbolea kutoka nje lakini kwasasa kutokana na uwepo wa kiwanda hiki na uwekezaji wake mahitaji ya mbolea yatapatikana kutoka viwanda vya ndani.
Naye Mkurugenzi wa Kiwanda cha Itracom Fertilisers Limited Bwana Nduwimana Nazaire amesema kuwa wao kwa kushirikiana na Taasisi za Serikali kama vile TARI na TFRA mpaka sasa tayari kuna aina 14 ambazo kiwanda kinazalisha ambapo pia kiwanda kina uwezo wa kutengeneza mbolea kulingana na eneo,kulingana na zao na pia kulingana na hitaji la mkulima.
Na kuongeza kuwa kiwanda hicho kinazalisha mbolea mchanganyiko wa chumvi chumvi na malighafi za asili kama vile samadi na zinginezo.
Uzinduzi huu ni miaka mitatu na nusu toka uwekezaji huu kuanza kufanyika hapa Jijini Dodoma.
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ZANZIBAR AZINDUA MAONYESHO YA MADINI LINDI
habari
Na Fredy Mgunda, Ruangwa, Lindi.
Waziri wa Nishati na Madini wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mheshimiwa Shaibu Hassan Kaduara, amezindua rasmi awamu ya pili ya Maonyesho ya Madini (Lindi Mining Expo) mkoani Lindi, yakilenga kuvutia wawekezaji na kutangaza fursa mbalimbali za rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Kaduara alisema thamani ya dhahabu imeendelea kupanda katika soko la dunia kutokana na athari za vita kati ya Urusi na Ukraine, ambako dhahabu inayozalishwa na Urusi imewekewa vikwazo kuingia katika masoko ya kimataifa.
"Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya 1996, pamoja na Sera ya Maendeleo ya Viwanda ya 1996–2020 na ile ya Viwanda Vidogo ya mwaka 2003, zipo kwenye mchakato wa kupitia upya kwa lengo la kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo ya kimkakati," alisema Kaduara.
Waziri huyo alibainisha kuwa miradi ya madini ni miongoni mwa miradi ya kimkakati nchini, ambayo inaendelea kufanyiwa tathmini kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sera mpya itakayowezesha Watanzania kunufaika zaidi na sekta hiyo.
Lindi Yajitokeza Kama Kitovu cha Madini Nchini
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Zainab Telack, alisema mkoa huo umebarikiwa kuwa na rasilimali kubwa za madini ambazo tayari zimeanza kuwanufaisha wananchi moja kwa moja.
“Maonyesho haya yanafungua milango kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Yanachochea uchumi wa eneo hili na kuongeza thamani ya madini tunayochimba,” alisema RC Telack.
Aliongeza kuwa maonyesho ya awamu ya kwanza mwaka 2023 yalivutia wageni kutoka mataifa 14 na zaidi ya watu 6,000 walihudhuria, jambo lililoongeza hadhi ya Lindi kama eneo la kimkakati kwa shughuli za madini nchini.
“Kwa sasa tunaona ongezeko la wawekezaji, uboreshaji wa miundombinu na fursa za ajira, hali inayodhihirisha kuwa Lindi ni sehemu muhimu katika ajenda ya maendeleo ya taifa,” aliongeza.
Ongezeko la Wachimbaji na Teknolojia ya Uchimbaji
Kwa mujibu wa Mratibu wa Maonyesho hayo, Bw. Mwinjuma Mkungu, ambaye ni Katibu Tawala Msaidizi Uchumi mkoani Lindi, idadi ya wachimbaji imeongezeka kutoka 2,265 hadi 2,948 baada ya maonyesho ya kwanza, huku mitambo ya kisasa ya uchimbaji ikiongezeka pia.
“Tumeona ongezeko kubwa la wawekezaji na mapato ya serikali yameongezeka kwa asilimia 10.1 baada ya maonyesho ya awali. Hii inaonyesha mchango wa moja kwa moja wa maonyesho haya kwa uchumi wa taifa,” alisema Mkungu.
Alfred Chilumba, mchimbaji mdogo, alishuhudia mabadiliko makubwa baada ya kupata elimu kupitia maonyesho ya awali.
“Tulikuwa hatujui kama tunaweza kutumia mitambo ya kisasa. Maonyesho haya yametufungua macho,” alisema.
Anna Milanzi, mama lishe anayehudumu kwenye maonyesho hayo, alisema ametumia fursa ya ongezeko la wageni kuongeza kipato chake.
“Kwa siku za kawaida napika kilo 5 za unga, lakini leo nimepika kilo 15. Biashara imenoga,” alisema kwa furaha.
Maonyesho Yadumu kwa Siku Kadhaa
Maonyesho hayo ya siku kadhaa yanahusisha maonesho ya bidhaa za madini, teknolojia mpya za uchimbaji, warsha za kitaalamu, na majadiliano baina ya serikali, wawekezaji na wachimbaji wadogo.
Yamebeba kauli mbiu: “Madini na Uwekezaji wa Fursa za Kiuchumi Lindi – Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025”, yakisisitiza uhusiano kati ya maendeleo ya sekta ya madini na ushiriki wa wananchi katika mustakabali wa taifa.
KIKAO KAZI CHA KUPITIA NA KUTHIBITISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA TAIFA WA KUZUIA KUZAMA MAJI CHAFANYIKA DODOMA
habari
Na Mwandishi wetu Dodoma.
Kikao kazi cha kupitia na kuthibitisha Rasimu ya Mpango Mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji chafanyika tarehe 11 Juni, 2025 katika ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na uokoa Jijini Dodoma.
Kikao hicho kimewashirikisha Wawakilishi kutoka Wizara, Taasisi na Idara za Serikali, Mashirika ya Kimataifa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mikoa mbalimbali ikiwemo Mwanza na Mara.
Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Kanali Selestine Masalamado amesema Nchi yetu imeendelea kukumbwa na matukio mbalimbali ya majanga ya asili na yanayosababishwa na shughuli za kibinadamu, ambayo yamekuwa na madhara makubwa kwa maisha ya wananchi hasa waishio pembezoni mwa fukwe wakiwemo Wazee, Vijana na Watoto, hivyo kuathiri maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Hata hivyo Kanali Masalamado amesema, Kutokana na majanga hayo, Serikali ilianza Mchakato wa kuandaa mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji mwaka 2024, kwa lengo la kuanzisha mfumo madhubuti na jumuishi wa kupunguza matukio ya vifo vinavyotokana na kuzama maji.



Ameongeza kwa kusema, Mkakati huu umeandaliwa kwa njia shirikishi, ukihusisha wadau kutoka sekta mbalimbali, ili kuhakikisha hatua zinazopendekezwa zinajengwa juu ya ushahidi wa kisayansi, uzoefu wa jamii, na muktadha halisi wa Tanzania.

Ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa washiriki wote kuchangia mawazo yao kwa weledi na uzalendo katika kupitia na kuboresha Rasimu ya Mkakati, ili ifikie viwango vinavyostahili kabla ya kuidhinishwa rasmi na kuanza kutekelezwa.
Mwisho


WAZAZI WAASWA KUTOCHANGIA MMOMONYOKO WA MAADILI KWA WATOTO
Serengeti-Mara.
Polisi Kata wa Kata ya Ikoma Wilaya ya Serengeti mkoani Mara Sajenti Emmanuel, ametoa wito kwa wazazi kutokuwa chanzo cha mmomonyoko wa maadili kwa watoto wao.
Ametoa kauli hiyo wakati akitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wananchi wa kitongoji cha Momorogoro kijiji cha Robanda, kata ya Ikoma, katika mwendelezo wa kampeni ya Elimu ya Nyumba kwa Nyumba.
Katika maelezo yake, Sajenti Emmanuel amewakumbusha wazazi kuwa wanalo jukumu kubwa la kuiandaa vyema kesho ya watoto wao kwa kuwapatia malezi bora, ambayo yatawasaidia kuwa watu wenye tija na mafanikio katika nyanja za elimu, afya, na uchumi.
Aidha, aliwasisitiza wazazi kuwafundisha watoto wao kuvaa mavazi ya heshima yanayomstiri mtu, kudumisha usafi wa mwili, mavazi, na mazingira yanayowazunguka, kama njia ya kulinda maadili yao.
Aliwakumbusha wazazi kuwa urithi wa kudumu ambao wanaweza kuwaachia watoto wao ni elimu, alisema itawapatia maarifa muhimu katika kipindi chote cha ukuaji wao na kuwasaidia kuwa watu wanaofaa na kuheshimika katika jamii.
MWENGE WA UHURU KUZINDUA MIRADI YA 7 YA THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 WILAYA YA MUHEZA
habari
Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa wilaya ya Muheza Zainabu Abdallah wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema wataupokea mwenge huo ukitokea wilaya Korogwe na ukiwa kweye wilaya hiyo utaweka mawe ya msingi miradi miwili,miradi minne itazinduliwa na mmoja utakaguliwa
Akizungumza maandalizi ya ujio huo wa mwenge mwaka huu alisema kwamba mwaka jana walikuwa namba moja kimkoa wilaya ambapo alisem wamejipanga katika maeneo ya miradi kuhakikisha inakuwa bora na viwango lakini kuhakikisha hamasa ya kutosha inakuwepo eneo la mpokezi,kwenye miradi na mkesha.
Aidha alisema katika mkesha wa mwenge huo wa uhuru watakuwepo wasanii mbalimbali ili kuweza kutoa burudani mbalimbali kwa wakazi wa mji huo na wageni ambao watashiriki huku akitoa wito wajitokeze kwa wingi kwa maana utakuwa wa aina yake kutokana na namna walivyojipanga.
Hata hivyo alisema pia watakuwa na kongamano maalumu la vijana na Mgeni rasmi atakuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchjini (TIC) Gilead Teri sambamba na watoa mada mashuhuri na wabobezi .
Mwishi