KIKAO KAZI CHA KUPITIA NA KUTHIBITISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA TAIFA WA KUZUIA KUZAMA MAJI CHAFANYIKA DODOMA

June 12, 2025 Add Comment

 

 



Na Mwandishi wetu Dodoma.

Kikao kazi cha kupitia na kuthibitisha Rasimu ya Mpango Mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji chafanyika tarehe 11 Juni, 2025 katika ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na uokoa Jijini Dodoma.

Kikao hicho kimewashirikisha Wawakilishi kutoka Wizara, Taasisi na Idara za Serikali, Mashirika ya Kimataifa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mikoa mbalimbali ikiwemo Mwanza na Mara.

Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Kanali Selestine Masalamado amesema Nchi yetu imeendelea kukumbwa na matukio mbalimbali ya majanga ya asili na yanayosababishwa na shughuli za kibinadamu, ambayo yamekuwa na madhara makubwa kwa maisha ya wananchi hasa waishio pembezoni mwa fukwe wakiwemo Wazee, Vijana na Watoto, hivyo kuathiri maendeleo ya kijamii na kiuchumi.


Hata hivyo Kanali Masalamado amesema, Kutokana na majanga hayo, Serikali ilianza Mchakato wa kuandaa mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji mwaka 2024, kwa lengo la kuanzisha mfumo madhubuti na jumuishi wa kupunguza matukio ya vifo vinavyotokana na kuzama maji.










Ameongeza kwa kusema, Mkakati huu umeandaliwa kwa njia shirikishi, ukihusisha wadau kutoka sekta mbalimbali, ili kuhakikisha hatua zinazopendekezwa zinajengwa juu ya ushahidi wa kisayansi, uzoefu wa jamii, na muktadha halisi wa Tanzania.


Ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa washiriki wote kuchangia mawazo yao kwa weledi na uzalendo katika kupitia na kuboresha Rasimu ya Mkakati, ili ifikie viwango vinavyostahili kabla ya kuidhinishwa rasmi na kuanza kutekelezwa.

Mwisho

WAZAZI WAASWA KUTOCHANGIA MMOMONYOKO WA MAADILI KWA WATOTO

June 12, 2025 Add Comment


Serengeti-Mara.


Polisi Kata wa Kata ya Ikoma Wilaya ya Serengeti mkoani Mara Sajenti Emmanuel, ametoa wito kwa wazazi kutokuwa chanzo cha mmomonyoko wa maadili kwa watoto wao. 


Ametoa kauli hiyo wakati akitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wananchi wa kitongoji cha Momorogoro kijiji cha Robanda, kata ya Ikoma, katika mwendelezo wa kampeni ya Elimu ya Nyumba kwa Nyumba.


Katika maelezo yake, Sajenti Emmanuel amewakumbusha wazazi kuwa wanalo jukumu kubwa la kuiandaa vyema kesho ya watoto wao kwa kuwapatia malezi bora, ambayo yatawasaidia kuwa watu wenye tija na mafanikio katika nyanja za elimu, afya, na uchumi.

Aidha, aliwasisitiza wazazi kuwafundisha watoto wao kuvaa mavazi ya heshima yanayomstiri mtu, kudumisha usafi wa mwili, mavazi, na mazingira yanayowazunguka, kama njia ya kulinda maadili yao.


Aliwakumbusha wazazi kuwa urithi wa kudumu ambao wanaweza kuwaachia watoto wao ni elimu, alisema itawapatia maarifa muhimu katika kipindi chote cha ukuaji wao na kuwasaidia kuwa watu wanaofaa na kuheshimika katika jamii.

MWENGE WA UHURU KUZINDUA MIRADI YA 7 YA THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 WILAYA YA MUHEZA

June 11, 2025 Add Comment

 


Na Siwema Afisa Habari MUHEZA

MWENGE wa Uhuru unatarajiwa kuwasili katika wilaya ya Muheza Ijumaa June 13 ukitokea wilaya Korogwe ambapo utazindua miradi 7 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Biloni 1.6 na utakimbizwa kwa umbali wa kilomita 90.4.


Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa wilaya ya Muheza Zainabu Abdallah wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema wataupokea mwenge huo ukitokea wilaya Korogwe na ukiwa kweye wilaya hiyo utaweka mawe ya msingi miradi miwili,miradi minne itazinduliwa na mmoja utakaguliwa

Akizungumza maandalizi ya ujio huo wa mwenge mwaka huu alisema kwamba mwaka jana walikuwa namba moja kimkoa wilaya ambapo alisem wamejipanga katika maeneo ya miradi kuhakikisha inakuwa bora na viwango lakini kuhakikisha hamasa ya kutosha inakuwepo eneo la mpokezi,kwenye miradi na mkesha.

Aidha alisema katika mkesha wa mwenge huo wa uhuru watakuwepo wasanii mbalimbali ili kuweza kutoa burudani mbalimbali kwa wakazi wa mji huo na wageni ambao watashiriki huku akitoa wito wajitokeze kwa wingi kwa maana utakuwa wa aina yake kutokana na namna walivyojipanga.

Hata hivyo alisema pia watakuwa na kongamano maalumu la vijana na Mgeni rasmi atakuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchjini (TIC) Gilead Teri sambamba na watoa mada mashuhuri na wabobezi .

Mwishi

MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 18 KUKAGULIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI LUSHOTO

June 11, 2025 Add Comment

 



Na Ashrack Miraji, 

Mwenge wa Uhuru umeingia rasmi katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto leo, baada ya kukabidhiwa kutoka Halmashauri ya Bumbuli, ambapo utakimbizwa umbali wa kilomita 112.8 kupitia tarafa mbili, kata nne na vijiji 23. Katika mbio hizo, Mwenge utakagua na kuzindua miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.8.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Zephania Sumaye, alisema kuwa kaulimbiu ya Mwenge wa mwaka huu ni: “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu,” ambayo inaakisi dhamira ya kitaifa ya kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mchakato wa kidemokrasia kwa njia ya amani na utulivu.

“Tumepokea Mwenge wa Uhuru tukiwa na maandalizi kamili. Kauli mbiu ya mwaka huu ni wito kwa kila Mtanzania kushiriki uchaguzi mkuu ujao kwa njia ya amani, busara na utulivu,” alisema Sumaye.

Aliongeza kuwa Mwenge huo utakagua na kuzindua miradi saba ya maendeleo inayogusa sekta mbalimbali kama elimu, afya, maji na miundombinu, ikiwa ni ishara ya dhamira ya Serikali katika kuwahudumia wananchi, hasa wa maeneo ya vijijini.


“Kwa jumla, miradi tunayokwenda kukagua ina thamani ya shilingi bilioni 1.8. Hii inaonesha jitihada kubwa zinazofanywa kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi wote,” aliongeza Mkuu huyo wa Wilaya.

Sumaye pia alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika mapokezi ya Mwenge huo, sambamba na kudumisha mshikamano na amani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mwenge wa Uhuru ni alama ya mshikamano wa kitaifa na maendeleo, ambao huzunguka nchini kote kila mwaka tangu mwaka 1961 kwa lengo la kuhamasisha maendeleo, uwajibikaji wa kijamii, mshikamano wa kitaifa, na sasa zaidi — ushiriki wa amani katika chaguzi za kidemokrasia.


 

KIKAO KAZI CHA KUPITIA NA KUTHIBITISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA TAIFA WA KUZUIA KUZAMA MAJI CHAFANYIKA DODOMA

June 11, 2025 Add Comment


Na Mwandishi wetu Dodoma.

Kikao kazi cha kupitia na kuthibitisha Rasimu ya Mpango Mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji chafanyika tarehe 11 Juni, 2025 katika ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na uokoa Jijini Dodoma.

Kikao hicho kimewashirikisha Wawakilishi kutoka Wizara, Taasisi na Idara za Serikali, Mashirika ya Kimataifa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mikoa mbalimbali ikiwemo Mwanza na Mara.


Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Kanali Selestine Masalamado amesema Nchi yetu imeendelea kukumbwa na matukio mbalimbali ya majanga ya asili na yanayosababishwa na shughuli za kibinadamu, ambayo yamekuwa na madhara makubwa kwa maisha ya wananchi hasa waishio pembezoni mwa fukwe wakiwemo Wazee, Vijana na Watoto, hivyo kuathiri maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Hata hivyo Kanali Masalamado amesema, Kutokana na majanga hayo, Serikali ilianza Mchakato wa kuandaa mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji mwaka 2024, kwa lengo la kuanzisha mfumo madhubuti na jumuishi wa kupunguza matukio ya vifo vinavyotokana na kuzama maji. 


Ameongeza kwa kusema, Mkakati huu umeandaliwa kwa njia shirikishi, ukihusisha wadau kutoka sekta mbalimbali, ili kuhakikisha hatua zinazopendekezwa zinajengwa juu ya ushahidi wa kisayansi, uzoefu wa jamii, na muktadha halisi wa Tanzania.

Ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa washiriki wote kuchangia mawazo yao kwa weledi na uzalendo katika kupitia na kuboresha Rasimu ya Mkakati, ili ifikie viwango vinavyostahili kabla ya kuidhinishwa rasmi na kuanza kutekelezwa.

Mwisho