MWENGE WA UHURU KUZINDUA MIRADI YA 7 YA THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 WILAYA YA MUHEZA

June 11, 2025 Add Comment

 


Na Siwema Afisa Habari MUHEZA

MWENGE wa Uhuru unatarajiwa kuwasili katika wilaya ya Muheza Ijumaa June 13 ukitokea wilaya Korogwe ambapo utazindua miradi 7 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Biloni 1.6 na utakimbizwa kwa umbali wa kilomita 90.4.


Hayo yalisemwa leo na Mkuu wa wilaya ya Muheza Zainabu Abdallah wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema wataupokea mwenge huo ukitokea wilaya Korogwe na ukiwa kweye wilaya hiyo utaweka mawe ya msingi miradi miwili,miradi minne itazinduliwa na mmoja utakaguliwa

Akizungumza maandalizi ya ujio huo wa mwenge mwaka huu alisema kwamba mwaka jana walikuwa namba moja kimkoa wilaya ambapo alisem wamejipanga katika maeneo ya miradi kuhakikisha inakuwa bora na viwango lakini kuhakikisha hamasa ya kutosha inakuwepo eneo la mpokezi,kwenye miradi na mkesha.

Aidha alisema katika mkesha wa mwenge huo wa uhuru watakuwepo wasanii mbalimbali ili kuweza kutoa burudani mbalimbali kwa wakazi wa mji huo na wageni ambao watashiriki huku akitoa wito wajitokeze kwa wingi kwa maana utakuwa wa aina yake kutokana na namna walivyojipanga.

Hata hivyo alisema pia watakuwa na kongamano maalumu la vijana na Mgeni rasmi atakuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchjini (TIC) Gilead Teri sambamba na watoa mada mashuhuri na wabobezi .

Mwishi

MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 18 KUKAGULIWA NA MWENGE WA UHURU HALMASHAURI LUSHOTO

June 11, 2025 Add Comment

 



Na Ashrack Miraji, 

Mwenge wa Uhuru umeingia rasmi katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto leo, baada ya kukabidhiwa kutoka Halmashauri ya Bumbuli, ambapo utakimbizwa umbali wa kilomita 112.8 kupitia tarafa mbili, kata nne na vijiji 23. Katika mbio hizo, Mwenge utakagua na kuzindua miradi ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.8.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Zephania Sumaye, alisema kuwa kaulimbiu ya Mwenge wa mwaka huu ni: “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa Amani na Utulivu,” ambayo inaakisi dhamira ya kitaifa ya kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mchakato wa kidemokrasia kwa njia ya amani na utulivu.

“Tumepokea Mwenge wa Uhuru tukiwa na maandalizi kamili. Kauli mbiu ya mwaka huu ni wito kwa kila Mtanzania kushiriki uchaguzi mkuu ujao kwa njia ya amani, busara na utulivu,” alisema Sumaye.

Aliongeza kuwa Mwenge huo utakagua na kuzindua miradi saba ya maendeleo inayogusa sekta mbalimbali kama elimu, afya, maji na miundombinu, ikiwa ni ishara ya dhamira ya Serikali katika kuwahudumia wananchi, hasa wa maeneo ya vijijini.


“Kwa jumla, miradi tunayokwenda kukagua ina thamani ya shilingi bilioni 1.8. Hii inaonesha jitihada kubwa zinazofanywa kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi wote,” aliongeza Mkuu huyo wa Wilaya.

Sumaye pia alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika mapokezi ya Mwenge huo, sambamba na kudumisha mshikamano na amani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mwenge wa Uhuru ni alama ya mshikamano wa kitaifa na maendeleo, ambao huzunguka nchini kote kila mwaka tangu mwaka 1961 kwa lengo la kuhamasisha maendeleo, uwajibikaji wa kijamii, mshikamano wa kitaifa, na sasa zaidi — ushiriki wa amani katika chaguzi za kidemokrasia.


 

KIKAO KAZI CHA KUPITIA NA KUTHIBITISHA RASIMU YA MPANGO MKAKATI WA TAIFA WA KUZUIA KUZAMA MAJI CHAFANYIKA DODOMA

June 11, 2025 Add Comment


Na Mwandishi wetu Dodoma.

Kikao kazi cha kupitia na kuthibitisha Rasimu ya Mpango Mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji chafanyika tarehe 11 Juni, 2025 katika ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na uokoa Jijini Dodoma.

Kikao hicho kimewashirikisha Wawakilishi kutoka Wizara, Taasisi na Idara za Serikali, Mashirika ya Kimataifa, Asasi zisizo za Kiserikali, Mikoa mbalimbali ikiwemo Mwanza na Mara.


Akifungua kikao hicho, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Kanali Selestine Masalamado amesema Nchi yetu imeendelea kukumbwa na matukio mbalimbali ya majanga ya asili na yanayosababishwa na shughuli za kibinadamu, ambayo yamekuwa na madhara makubwa kwa maisha ya wananchi hasa waishio pembezoni mwa fukwe wakiwemo Wazee, Vijana na Watoto, hivyo kuathiri maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Hata hivyo Kanali Masalamado amesema, Kutokana na majanga hayo, Serikali ilianza Mchakato wa kuandaa mkakati wa Taifa wa Kuzuia Kuzama Maji mwaka 2024, kwa lengo la kuanzisha mfumo madhubuti na jumuishi wa kupunguza matukio ya vifo vinavyotokana na kuzama maji. 


Ameongeza kwa kusema, Mkakati huu umeandaliwa kwa njia shirikishi, ukihusisha wadau kutoka sekta mbalimbali, ili kuhakikisha hatua zinazopendekezwa zinajengwa juu ya ushahidi wa kisayansi, uzoefu wa jamii, na muktadha halisi wa Tanzania.

Ametumia nafasi hiyo kutoa wito kwa washiriki wote kuchangia mawazo yao kwa weledi na uzalendo katika kupitia na kuboresha Rasimu ya Mkakati, ili ifikie viwango vinavyostahili kabla ya kuidhinishwa rasmi na kuanza kutekelezwa.

Mwisho 


WAONGOZA WATALII WATOA KONGOLE KWA NCAA MABORESHO YA BARABARA KUTEKEKEA MSIMU WA UTALII

June 11, 2025 Add Comment



Na Mwandishi wa NCAA, Ngorongoro


Waongoza utalii kutoka kampuni mbalimbali zinazojihusisha na shughuli za utalii nchini wameipongeza uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kwa juhudi wanazofanya  kuboresha miundombinu ya barabara katika Eneo la  Hifadhi ya Ngorongoro. 


Wadau hao wameelezeq hatua hiyo kuwa ni suluhisho la muda mrefu kwa changamoto zilizokuwa zikiwakabili, hasa wakati wa msimu wa kilele cha utalii (high season)


Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika geti la kuingia hifadhi ya Ngorongoro Juni 11, 2025, baadhi waongoza utalii hao wameeleza kuwa maboresho hayo yameleta mabadiliko makubwa katika usafiri, kupunguza muda wa safari, kuongeza usalama wa wageni, na kuboresha hali ya utalii katika hifadhi hiyo maarufu duniani.

“Tunatoa pongezi kwa NCAA kwa kazi kubwa waliyoifanya kuboresha barabara,  kwa sasa imekuwa rahisi zaidi kuwafikisha wageni kwa haraka na salama kwenye maeneo ya vivutio vya utalii vilivyopo Ngorongoro 

” alisema Mohammed Tenga kutoka kumpuni ya Zara Tours. 

Kwa upande wake Walter Temba kutoka 

kampuni ya utalii ya Serengeti Smiles alieleza kuwa maboresho ya miundombinu ya barabara yanayoendelea yamekuja kwa wakati muafaka, ikizingatiwa kuwa sekta ya utalii nchini inaendelea kukua kwa kasi huku idadi ya wageni kutoka ndani na nje ya nchi ikiendelea kuongezeka kila mwaka.

“Kwa muda mrefu tumekuwa tukikumbana na changamoto kubwa hasa wakati wa mvua magari yanakwama na wageni kuharibika hata kabla ya kufika kwenye vivutio. Lakini sasa hali ni tofauti kabisa, barabara zimekarabatiwa kwa kiwango kizuri na zinaweza kupitika hata kipindi cha mvua ombi letu ni kuwa jitihada hizi ziwe endelevu,” alisema Temba.


Kwa Mujibu wa NCAA, maboresho ya barabara ni sehemu ya maandalizi ya taasisi hiyo kukabiliana na ongezeko kubwa la watalii ambalo limeanza mwezi juni ambalo linatarajiwa kuongezeka   hadi mwezi Oktoba kila mwaka.

 Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro hupokea maelfu ya wageni kutoka mataifa mbalimbali duniani wanaokuja kutembelea vivutio vya utalii ambapo takwimu zinaonesha kuwa kati ya Mwezi Julai 2024 hadi Mei, 2025 jumla ya watalii 972,896 wametembelea hifadhi kwa shughuli za utalii.

WAKUU WA VITENGO REA,TARURA,RUWASA WAKUTANA KUJENGEANA UWEZO

June 11, 2025 Add Comment

 Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Bi. Martha Chassama amekutana na kuzungumza na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasilino wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Bi. Catherine Sungura na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Masoko wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Bw. Athumani Shariff katika kikao kifupi kilichofanyika jijini Dodoma.   Kikao hicho kifupi kililenga kujengeana uwezo wa taasisi hizo hususan katika maeneo ya vijijini ili kuongeza chachu katika maeneo hayo.