DKT.BITEKO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KITUO KIKUBWA CHA GESI AFRIKA MASHARIKI

June 05, 2025 Add Comment


📌 *Tanga kuwa Kitovu cha Nishati nchini*


📌 *Dkt. Biteko Asisitiza Ajira Kwa Wazawa*


📌*Kampeni ya Rais Samia ya Nishati Safi ya Kupikia  Yavutia Wawekezaji*


📌*Matumizi ya Gesi ya Kupikia Yaongezeka Kila Mwaka*


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa wawekezaji nchini kutoa kipaumbele cha ajira kwa Watanzania ili kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na uchumi wa Taifa kwa ujumla.


Amewaomba wawekezaji wa mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy licha ya kuwa zitazalishwa ajira zaidi ya 300 na baadae zaidi ya 2,000, waangalie utaratibu katika ujenzi wa mradi huo ambao utawezesha wazawa kupata kazi na hakuna sababu ya kutafuta watu kutoka mbali.


Dkt. Biteko ametoa wito huo leo Juni 5, 2025 jijini Tanga wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ujenzi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy mkoani humo.


“ Mradi huu uwe mfano wa kielelezo kila kazi anayoweza kufanya Mtanzania apewe, ili asilimia 40 ya fedha za ujenzi wa mradi zizunguke nchini. Nitasikitika nikiona kila aina ya kazi analetwa mtu kutoka nje kuja kufanya,” amesema Dkt. Biteko.

Ameendelea kutoa wito kwa wawekezaji kufikiria namna ya kupeleka huduma ya ujazaji mitungi ya gesi katika maeneo ya vijijini ikiwa ni pamoja na kuanzisha teknolojia ya kusaidia mtu aweze kulipia gesi kulingana na mahitaji yake badala ya kujaza mtungi mzima.


Dkt. Biteko amesema kwa mujibu wa taarifa ya utendaji sekta ndogo ya mafuta ya EWURA ya mwaka 2024, matumizi ya gesi ya kupikia yaani (LPG) huongezeka kwa kasi kila mwaka. Ambapo kwa mwaka 2023/24 matumizi yalifikia zaidi ya tani 403,000 ikilinganishwa na tani 293,000 mwaka wa fedha 2022/23 sawa na ongezeko la asilimia 38.


Amewahakikishia Kampuni ya Tanga Energy International Ltd kuwa mradi wao utakuwa na uhakika wa soko ndani na nje ya nchi na kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao  ili kufikia malengo yao ya kuleta huduma bora na nafuu kwa Watanzania.

Katika kuthibitisha hilo, Dkt. Biteko amesema kupitia Wakala wa Nishati Vijijini, Serikali inaendelea na programu ya kutoa ruzuku ili wananchi wapate mitungi ya gesi ya kupikia kwa punguzo la bei hadi kufikia asilimia 50 na kusambaza mitungi 452,445 ambapo hadi kufikia Aprili, 2025 jumla ya mitungi 154,225 imeshasambazwa.


“ Tarehe 2 Juni, 2025 pale jijini Dodoma tumezindua Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia. Hivyo, kupitia Mkakati huu, Serikali itaendelea kutoa elimu nchi nzima na hivyo kuinua uelewa wa wananchi na hatimaye kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo LPG ni chanzo kikuu,” amesisitiza Dkt. Biteko.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema Rais Samia anataka Mkoa wa Tanga uwe kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, na hivyo ameendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kutimiza lengo hilo ikiwemo kupanua mfumo wa kusafirisha umeme kutoka Majani mapana hadi Pemba kutoka kilovoti 33 hadi 132.


Pamoja na hayo ametoa wito kwa Watanzania kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa kuchagua viongozi wanaofaa “ Tumuunge mkono Rais Samia kwa kuwa kinara wa Kampeni ya Nishati Safi kimataifa ili Watanzania wengi watumie nishati safi ya kupikia,” amemaliza Dkt. Biteko.


Naye, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Suleiman Jafo amesema kuwa utendaji kazi wa Dkt. Biteko umesaidia kuimarika kwa sekta ya nishati huku akisisitiza kuwa kukamilika kwa mradi huo mkubwa wa Kituo cha Gesi kutaifanya Tanzania kuwa msafirishaji mkubwa wa gesi  na kuchochea ukuaji wa viwanda nchini.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Burian amesema mradi huo utasaidia kuitangaza Tanga kimataifa, kuongeza ajira na pato la mkoa na Taifa kwa ujumla.

Akitoa salamu za Chama cha Gesi na Mafuta, Mkurugenzi Mtendaji wa TOAG, Abdulsamad Abdulrahim amesema mradi huo utaisaidia Tanzania kuleta mapinduzi ya nishati katika ukanda wa Afrika Mashariki, kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo safi.


Bw. Abdulrahim amebainisha kuwa Watanzania wako tayari na hiyo ni fursa kwa wawekezaji wazawa kuonesha uwezo wao na wako tayari kufanya kazi.


“Tunaishukuru Serikali kwa kuweka mazingira wezeshi ya kusaidia utekelezaji wa miradi kama hii ambayo ni zao la ushirikiano wa wageni na wazawa wenye kufanya mawazo kuwa uhalisia,” amesema Abdulrahim.


Awali akitoa maelezo ya mradi, Michael Dimond amesema LPG ni suluhu ya nishati safi ya kupikia na kuwa Kampuni ya Pretedec imefurahishwa jitihada za Rais Samia katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na lengo la Serikali la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.


“Leo tunajivunia kuwekwa kwa jiwe la msingi katika mradi huu wa kipekee Tanzania ambao umezingatia usalama wa usambazaji wa LPG katika ukanda wa Afrika Mashariki,” amesema Dimond.


Mwakilishi wa Kampuni ya Asas, Bw. Ahmed Asas amesema mbali na manufaa ya kiafya na mazingira mradi huo utachochea uchumi jumuishi na kuchangia katika ukuaji wa viwanda vya ndani.


Mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy unatekelezwa kwa ushirikiano wa Kampuni ya Pretedec na Asas ambao unatagharimu dola za marekani milioni 100 utakuwa mradi mkubwa wa LPG nchini. Aidha, kupitia mradi huo unaotarajiwa kukamilika 2027 utanufaisha pia nchi za Burundi, Kenya, Uganda, Burundi na Zambia kwa kuagiza gesi kutoka nchini Tanzania.


Mwisho

DKT.BITEKO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA KITUO CHA GESI AFRIKA MASHARIKI

June 05, 2025 Add Comment


📌 *Tanga kuwa Kitovu cha Nishati nchini*


📌 *Dkt. Biteko Asisitiza Ajira Kwa Wazawa*


📌*Kampeni ya Rais Samia ya Nishati Safi ya Kupikia  Yavutia Wawekezaji*


📌*Matumizi ya Gesi ya Kupikia Yaongezeka Kila Mwaka*


*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa wawekezaji nchini kutoa kipaumbele cha ajira kwa Watanzania ili kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na uchumi wa Taifa kwa ujumla.



Amewaomba wawekezaji wa mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy licha ya kuwa zitazalishwa ajira zaidi ya 300 na baadae zaidi ya 2,000, waangalie utaratibu katika ujenzi wa mradi huo ambao utawezesha wazawa kupata kazi na hakuna sababu ya kutafuta watu kutoka mbali.


Dkt. Biteko ametoa wito huo leo Juni 5, 2025 jijini Tanga wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ujenzi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy mkoani humo.

“ Mradi huu uwe mfano wa kielelezo kila kazi anayoweza kufanya Mtanzania apewe, ili asilimia 40 ya fedha za ujenzi wa mradi zizunguke nchini. Nitasikitika nikiona kila aina ya kazi analetwa mtu kutoka nje kuja kufanya,” amesema Dkt. Biteko.


Ameendelea kutoa wito kwa wawekezaji kufikiria namna ya kupeleka huduma ya ujazaji mitungi ya gesi katika maeneo ya vijijini ikiwa ni pamoja na kuanzisha teknolojia ya kusaidia mtu aweze kulipia gesi kulingana na mahitaji yake badala ya kujaza mtungi mzima.


Dkt. Biteko amesema kwa mujibu wa taarifa ya utendaji sekta ndogo ya mafuta ya EWURA ya mwaka 2024, matumizi ya gesi ya kupikia yaani (LPG) huongezeka kwa kasi kila mwaka. Ambapo kwa mwaka 2023/24 matumizi yalifikia zaidi ya tani 403,000 ikilinganishwa na tani 293,000 mwaka wa fedha 2022/23 sawa na ongezeko la asilimia 38.

Amewahakikishia Kampuni ya Tanga Energy International Ltd kuwa mradi wao utakuwa na uhakika wa soko ndani na nje ya nchi na kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao  ili kufikia malengo yao ya kuleta huduma bora na nafuu kwa Watanzania.


Katika kuthibitisha hilo, Dkt. Biteko amesema kupitia Wakala wa Nishati Vijijini, Serikali inaendelea na programu ya kutoa ruzuku ili wananchi wapate mitungi ya gesi ya kupikia kwa punguzo la bei hadi kufikia asilimia 50 na kusambaza mitungi 452,445 ambapo hadi kufikia Aprili, 2025 jumla ya mitungi 154,225 imeshasambazwa.

“ Tarehe 2 Juni, 2025 pale jijini Dodoma tumezindua Mkakati wa Taifa wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia. Hivyo, kupitia Mkakati huu, Serikali itaendelea kutoa elimu nchi nzima na hivyo kuinua uelewa wa wananchi na hatimaye kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo LPG ni chanzo kikuu,” amesisitiza Dkt. Biteko.


Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema Rais Samia anataka Mkoa wa Tanga uwe kitovu cha biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki, na hivyo ameendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kutimiza lengo hilo ikiwemo kupanua mfumo wa kusafirisha umeme kutoka Majani mapana hadi Pemba kutoka kilovoti 33 hadi 132.


Pamoja na hayo ametoa wito kwa Watanzania kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa kuchagua viongozi wanaofaa “ Tumuunge mkono Rais Samia kwa kuwa kinara wa Kampeni ya Nishati Safi kimataifa ili Watanzania wengi watumie nishati safi ya kupikia,” amemaliza Dkt. Biteko.


Naye, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Suleiman Jafo amesema kuwa utendaji kazi wa Dkt. Biteko umesaidia kuimarika kwa sekta ya nishati huku akisisitiza kuwa kukamilika kwa mradi huo mkubwa wa Kituo cha Gesi kutaifanya Tanzania kuwa msafirishaji mkubwa wa gesi  na kuchochea ukuaji wa viwanda nchini.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Burian amesema mradi huo utasaidia kuitangaza Tanga kimataifa, kuongeza ajira na pato la mkoa na Taifa kwa ujumla.


Akitoa salamu za Chama cha Gesi na Mafuta, Mkurugenzi Mtendaji wa TOAG, Abdulsamad Abdulrahim amesema mradi huo utaisaidia Tanzania kuleta mapinduzi ya nishati katika ukanda wa Afrika Mashariki, kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya nishati isiyo safi.


Bw. Abdulrahim amebainisha kuwa Watanzania wako tayari na hiyo ni fursa kwa wawekezaji wazawa kuonesha uwezo wao na wako tayari kufanya kazi.


“Tunaishukuru Serikali kwa kuweka mazingira wezeshi ya kusaidia utekelezaji wa miradi kama hii ambayo ni zao la ushirikiano wa wageni na wazawa wenye kufanya mawazo kuwa uhalisia,” amesema Abdulrahim.


Awali akitoa maelezo ya mradi, Michael Dimond amesema LPG ni suluhu ya nishati safi ya kupikia na kuwa Kampuni ya Pretedec imefurahishwa jitihada za Rais Samia katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na lengo la Serikali la kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034.


“Leo tunajivunia kuwekwa kwa jiwe la msingi katika mradi huu wa kipekee Tanzania ambao umezingatia usalama wa usambazaji wa LPG katika ukanda wa Afrika Mashariki,” amesema Dimond.


Mwakilishi wa Kampuni ya Asas, Bw. Ahmed Asas amesema mbali na manufaa ya kiafya na mazingira mradi huo utachochea uchumi jumuishi na kuchangia katika ukuaji wa viwanda vya ndani.


Mradi wa Kituo cha Gesi cha Tanga International Energy unatekelezwa kwa ushirikiano wa Kampuni ya Pretedec na Asas ambao unatagharimu dola za marekani milioni 100 utakuwa mradi mkubwa wa LPG nchini. Aidha, kupitia mradi huo unaotarajiwa kukamilika 2027 utanufaisha pia nchi za Burundi, Kenya, Uganda, Burundi na Zambia kwa kuagiza gesi kutoka nchini Tanzania.


Mwisho

JAB YAANZA KUGAWA PRESS CARD KWA WAANDISHI WA HABARI

June 05, 2025 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Zikiwa zimesalia siku 17 kwa Waandishi wa Habari Kujisajili katika Mfumo wa TAI-HABARI ili kuomba Ithibati na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card), tayari waliokidhi vigenzo vilivyoanishwa Kisheria wameanza kupewa Vitambulisho hivyo.

Waandishi wa Habari wa kwanza kufika Ofisi za Bodi zilizopo Mtaa wa Jamhuri Jijini Dar es Salaam kuchukua vitambulisho vyao ni David Mayunga, Erasto Vedasto na Fredrick Mwantandi wote kutoka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Wengine waliokabidhiwa vitambulisho vyao ni Mhariri wa gazeti la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar- Zanzibaleo Mwanajuma Hassan na Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Taasisi ya Goshen Tanzania-goshenonlinetv Isaya Momba.
Mfumo huo uliofunguliwa rasmi Mei 19 mwaka huu, unatoa fursa kwa Wahariri, Waandishi wa Habari, Wapiga Picha, Watangazaji wa Radio na Televisheni, Waandishi wa Kujitegemea na Waandaaji wa Vipindi, waliokidhi vigezo vya Kitaaluma kujisali na kujaza taarifa zao kupitia kiunganishi cha https://taihabari.jab.go.tz ili kuomba Ithibati na Kitambulisho ambapo mwisho wa kujisajili ni Juni 21 mwaka huu.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo Wakili Patrick Kipangula amewapongeza waandishi hao na kutoa wito kwa waandishi wengine kuutumia vema muda uliotolewa.

BENKI YA CRDB YANG'ARA KATIKA TUZO ZA AFRICAN BANKER 2025,YATWAA TUZO YA BENKI BORA KWA WAJASIRIAMALI

June 05, 2025 Add Comment

 


Dar es Salaam, 05 Juni 2025 – Benki ya CRDB imeandika ukurasa mpya wa mafanikio baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya Benki Bora kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (SME) katika hafla ya tuzo za sekta ya benki barani Afrika ‘African Banker Awards 2025,’ iliyofanyika sambamba na Mkutano Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) jijini Abidjan, Côte d’Ivoire.

Kaulimbiu ya mwaka huu wa tuzo hizo ilikuwa “Mabadiliko ya Tabianchi na Maendeleo Endelevu,” ikiakisi umuhimu wa sekta ya fedha katika kuchochea ukuaji wa kijani, ujumuishi wa kijinsia na uhimilivu wa kiuchumi barani Afrika.

Katika mwaka huu ambapo Benki ya CRDB inaadhimisha miaka 30 ya huduma ubunifu, ilipata heshima ya kutajwa katika vipengele vinne vikuu, vikiwemo: Benki Bora kwa Wajasiriamali (Mshindi), Banker of the Year – kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki, Abdulmajid Mussa Nsekela, Benki Bora kwa maendeleo endelevu, Benki Bora ya mwaka (AFAWA).

Tuzo hiyo ya Benki Bora kwa Wajasiriamali ilipokelewa na Afisa Mkuu wa Biashara, Boma Raballa, ambaye alieleza kuwa ushindi huo ni kielelezo cha dhamira ya Benki hiyo ya kuwapatia wateja na watanzania kwa ujumla wake huduma bunifu za fedha. Katika miaka 30 tokea kuanzishwa kwake, benki hiyo imeendelea kuwa nguzo ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wajasiriamali, hususan vijana na wanawake. “Ushindi huu si wetu pekee, bali ni wa jamii nzima tunayoihudumia,” ameeleza Raballa.

Benki ya CRDB imejidhihirisha kuwa mshirika mkubwa wa wajasiriamali nchini ikitoa uwezeshaji wa hadi shilingi bilioni 5. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2024 mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 1.2 imetolewa kwa zaidi ya wajasiriamali 230,000 kutoka sekta mbalimbali.

Benki ya CRDB imekuwa kinara katika huduma bunifu kwa wajasiriamali nchini, ikiwa Benki ya kwanza kuanzisha kitengo maalum kwa ajili ya kuhudumia kundi hili la wateja mwaka 2000.

Mwaka 2024, Benki ya CRDB ilifanya maboresho makubwa ya akaunti ya wajasiriamali ‘Biashara Akaunti’, ikiboresha pia fursa za uwezeshaji kupitia mikopo, pamoja na kutoa suluhisho za kidijitali kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa upokeaji malipo kwa wateja kupitia huduma za ‘LIPA HAPA’ na mashine za manunuzi (PoS).

Aidha, Benki hiyo pia inazo bidhaa mahususi kwa ajili ya kusaidia wafanyabiashra wanaogaiza bidhaa nje ya nchi kama ‘Mkopo wa Komboa,’ ukisaidia wateja kutoa mizigo yao bandarini kwa wakati. Hatua ambayo imeondoa ucheleweshaji katika uzalishaji na usambazaji wa bidhaa sokoni.

Sambamba na huduma, Benki pia inatoa huduma za ufadhili wa biashara (trade finance) na ufadhili wa rasilimali (asset financing), ambazo zimekuwa msaada mkubwa kwa wateja katika kukuza na kuimarisha biashara zao.

Benki ya CRDB pia imekuwa ikiwapatia wajasiriamali uzoefu wa biashara kimataifa kwa kuwapeleka nchi mbalimbali duniani ili kuwapa fursa za kujifunza na kuongeza thamani kwenye biashara wanazozifanya, huku ikiwajengea uwezo wa kushindana katika masoko ya kimataifa. Hii ni hatua muhimu katika kukuza ushindani wa bidhaa na huduma za Kitanzania.

Aidha Benki ya CRDB imekuwa ikishirikiana kimakakati na tasisi za kimataifa zinazolenga kuwasaidia wajasiriamali kama vile AGF, PROPARCO, DFC, GuarantCo na GCF pamoja na taasisi za hapa nchini kama vile PASS na TADB. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Benki hiyo imeweza kukusanya zaidi ya Dola za Marekani Milioni 700, ikionyesha imani ya washirika wa kimataifa katika uwezo na utayari wa benki katika kuwawezesha wajasiriamali nchini.

“Katika miaka 30 ya uwepo wetu, tumejifunza kuwa hakuna maendeleo ya kweli bila kuwainua wajasiriamali. Tunaendelea kujipanga kufikia wengi zaidi kupitia mikakati madhubuti ya ujumuishi, hasa kwa wanawake na vijana, kama sehemu ya kusaidia ajenda ya serikali ya maendeleo jumuishi,” aliongeza Raballa.
Tuzo hii ni ushahidi mwingine wa jinsi Benki ya CRDB imejikita kwa dhati katika kuwa daraja la mafanikio kwa maelfu ya wajasiriamali nchini. Kuelekea mbele, Benki hiyo imeendelea kuonyesha utayari wake katika kuwahudumia wajasiriamali kwa kutoa kipaumbele kikubwa kwa kundi hilo la wateja katika Mkakati wake wa Muda wa Kati wa Biashara wa 2023 – 2027.

UDSM yawaita Wadau wa Elimu kushiriki maadhimisho Wiki ya Utafiti na Ubunifu

June 05, 2025 Add Comment

 

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

CHUO  Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimeutaarifu umma wa Watanzania na kuwaalika wadau wa elimu na maendeleo, kwa ujumla kushiriki katika Maadhimisho ya kumi ya Wiki ya Utafiti na Ubunifu ya UDSM yatakayofanyika kuanzia Juni 9- 11, 2025 katika Viwanja ya Maktaba ya Chuo.

Akizungumza na Waandishi  wa Habari Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo-Utafiti, Prof. Nelson Boniface (Pichani) amesema kuwa Maonesho hayo yanatarajiwa kuhitimishwa Juni 11, 2025 na mazungumzo ya mashirikiano ya kimkakati, kongamano, maonesho na mawasilisho ya watafiti na wabunifu likiwa ni jukwaa la washiriki kupata fursa ya kubadilishana maarifa na ushirikiano.

Aidha, Prof.  Boniface amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni: "Kutumia teknolojia ya Dijitali ili kukuza utafiti, ubunifu na ubiasharishaji,".

Ameongeza kuwa miradi mingi itakayooneshwa ni ile ya wanafunzi na Wanataaluma huku akitanabaisha kuwa mtoa Mada Mkuu ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mhandisi Peter Ulanga na Profesa Lilian Kaale Mkurugenzi katika masuala ya Ubunifu UDSM.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinatumia fursa hiyo kujipambanua kwa jamii kwa kuonesha shughuli zake za utafiti, ubunifu, huduma kwa umma na ubadilishanaji maarifa kwa kuunga mkono Dira ya  Taifa ya  Maendeleo 2050.