DKT.BITEKO AWATAKA WAZAZI KUVUMILIANA KUTUNZA FAMILIA ZAO

May 24, 2025 Add Comment

📌 Asisitiza wazazi kutenga muda wa kuwa na watoto wao


📌 Asema familia imara ni msingi wa dunia imara


📌 Mashirika, Wadau wa Maendeleo waipongeza Serikali kuimarisha malezi ya watoto


📌 Zaidi ya kaya 15,000 zapata elimu ya malezi jumuishi na huduma za afya ngazi ya jamii


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa rai kwa wazazi nchini kuvumiliana na kushirikiana katika malezi ya watoto wao ambao ndio msingi wa familia yeyote na Taifa kwa ujumla. 

Dkt. Biteko ametoa rai hiyo Mei 24, 2025 jijini Mwanza wakati akimwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdory Mpango katika Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia yenye Kaulimbiu inayosema “ Mtoto ni Malezi: Msingi wa Familia Bora kwa Taifa Imara”

“ Mtoto ni zao la matokeo ya wazazi wawili, Naomba wazazi tuthamini kuwa mtoto ni mtu muhimu na anahitaji  kulelewa, jambo hili la kutolea watoto likiendelea tutakuwa na jamii isiyo na msingi imara wa familia,” amesema Dkt. Biteko.

Ameendelea kusema “ Na sisi tukumbuke kuwa tumefika hapa kwa kuwa wako wazazi walivumiliana na wakatulea katika familia, sisi tusiwe watu wa kutelekeza familia zetu, ni wajibu wa kila mmoja kujua kuwa familia ni msingi, tukijua kuwa kila mtu ana mapungufu hivyo tuvumiliane tulee familia zetu, ”

Dkt. Biteko amebainisha kuwa familia ikiimarika na dunia itaimarika hivyo wazazi watenge muda wa kuwa na familia zao ili kuwarithisha mila na tamaduni zao. Aidha, matokeo ya wazazi kushtakiana kwa watoto yanajenga chuki miongoni mwa watoto hata katika maisha yao ya baadaye.


Pia, ametoa rai kwa watoto kuwa watiifu kwa wazazi na walimu wao sambamba na kujifunza kwa bidii na kuishi kwa kufuata miongozo ya dini.

Katika kuadhimisha siku hiyo ya familia, Dkt. Biteko ametaja baadhi ya majukumu ya familia kuwa ni kutoa huduma ili kukidhi mahitaji ya watoto na familia, kusimamia malezi na makuzi mema ya watoto na kurithisha mila na tamaduni nzuri kwa watoto na familia kwa ujumla kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine.

Fauka ya hayo, amesema katika kuimarisha malezi bora kwa watoto chini ya miaka 8, Serikali kwa kushirikiana na Wadau imeandaa na inatekeleza Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kwa kipindi cha mwaka 2021/22 – 2025/26.


Programu ambayo inahakikisha kuwa watoto wanapata huduma stahiki na jumuishi za malezi kwa uwiano ulio sawa kuanzia mtoto anapokuwa tumboni mwa mama yake hadi anapofikisha umri wa miaka 8.  

Ametaja mafanikio ya programu hiyo kuwa ni kuwajengea uwezo walimu wa awali 12,000 kutoka Halmashauri 184 kwa kutoa elimu ya malezi chanya ya watoto, wakihudumia zaidi ya watoto 360,000, kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo mchana 4,178, kutoa huduma za malezi na elimu ya awali kwa zaidi ya watoto 400,000. Aidha, vituo vya kijamii 206 vinavyomilikiwa na jamii yenyewe vimeanzishwa vikitoa huduma kwa watoto 11,675.


“ Katika kuimarisha huduma za kundi la watoto wa miaka 5 hadi 8, Serikali imejenga madarasa mapya ya awali 1,316 na kupatiwa vifaa vya kujifunzia. Pia, zaidi ya kaya 15,000 zimefikiwa na elimu ya malezi jumuishi na huduma za afya ngazi ya jamii wakipata huduma muhimu za afya, lishe, malezi yenye kuitikia hisia za mtoto, elimu ya awali na uchangamshi wa mtoto na ulinzi na usalama na mtoto,  amesititiza Dkt. Biteko


Aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau wengine imetoa mafunzo kwa wataalamu zaidi ya 15,000 wakiwemo Walezi wa Vituo vya Kulelea Watoto Wadogo mchana, Wahudumu wa Afya, Waandishi wa Habari, na Maafisa wa Ustawi na Maendeleo ya Jamii katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.


Naye, Naibu Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mwanaidi Ali Khamis amesema kuwa Maadhimisho hayo yanalenga  kutathmini nafasi ya familia katika malezi ya watoto ambao ndio msingi wa familia yeyote na Taifa kwa ujumla. Vilevile, malezi ya mtoto yanaanza mara tu mtoto anapozaliwa na Serikali inasisitiza baba na mama kuwa karibu na mtoto wakati huo.


“ Akina mama na akina baba washirikiane  kwa pamoja kulea watoto ili wawe na  malezi bora, wapate elimu na huduma zingine muhimu kwao,” amesema Mhe. Mwanaidi.


Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. John Jingu amesema kupitia maadhimisho hayo wameandaa maazimio matano yanaloyenga kukuza malezi na makuzi ya mtoto ili kuimarisha familia.


Ametaja maazimio hayo kuwa ni kueneza vituo vya malezi na makuzi ya mtoto nchi nzima ili kila mtoto apate huduma jumuishi, lishe na kuwa na usalama wao pamoja na kufanya kazi kwa kushirikiana na sekta binafsi.


Ameendelea kusema maazio hayo ni pamoja na kuimarisha huduma za  utambuzi ili watoto wapate huduma mapema na kukuza eneo la smart malezi kwa kuimarisha matumizi ya TEHAMA ili wazazi waweze kubadilishana  mawazo kwa kutumia TEHAMA na watoto kupata nafasi ya kukua vizuri.


“ Kukuza na kuimarisha ushirikiano na taasisi za dini na mila ili kuimarisha masuala ya malezi, makuzi na taasisi  ya familia na kuongeza idadi ya watoa huduma wenye uwezo ili waweze kuenea  nchi nzima,” amemalizia Dkt. Jingu.


Akitoa salamu za Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Elizabeth Maganga amesema kuwa Mashirika hayo yameendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika malezi na makuzi ya mtoto nchini.


Amesema umri wa kisayansi wa kumlea mtoto ni mwaka 0 hadi 8 na kuwa ni kipindi kizuri cha kumsaidia mtoto kukua vizuri hivyo ni fursa kwa Taifa kuwekeza katika malezi ya mtoto.


Akitoa salamu za Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Laximi Bhawan amesema kuwa Shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali katika kuweka mikakati ya kusaidia malezi ya watoto.


Aidha, pamoja na Maadhimisho hayo, Dkt. Biteko amezindua Miongozo ya Afua za Utekelezaji wa Malezi na Matunzo ya Watoto na Familia, Kutambua Mchango wa Wadau kwenye Malezi na Ustawi wa Familia na Kuzindua Kampeni ya Malezi kwa Mtoto.


Mwisho

MBEKI AWAASA VIONGOZI WA AFRIKA KUWA WAZALENDO KATIKA KULINDA MASLAHI YA BARA LAO

May 24, 2025 Add Comment

 Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Mheshimiwa Thabo Mbeki, amewahimiza viongozi wa Bara la Afrika kuwa wakweli na waaminifu katika kulinda maslahi ya bara lao, ili kufanikisha malengo ya kukuza uchumi na kuboresha maisha ya Waafrika.


Mheshimiwa Mbeki ameyasema hayo katika hafla ya chakula cha jioni iliyofanyika tarehe 23 Mei, 2025 jijini Dar es Salaam .

Mheshimiwa Mbeki amesisitiza kuwa maendeleo ya Bara la Afrika yatapatikana endapo viongozi wataweka mbele maslahi ya nchi zao na kuongoza kwa uadilifu, uwazi, na dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko chanya kwa Waafrika wote.

“Tunapoadhimisha Siku ya Afrika mwaka huu kwa kaulimbiu ‘Haki kwa Waafrika na Watu wa Asili ya Kiafrika Kupitia Fidia: Kuangazia Historia Yetu, na Kuunda Mustakabali Wetu,’ tunakumbushwa kuwa haki siyo mwisho, bali ni dai endelevu la ukweli, heshima, na uongozi unaoakisi hali halisi za watu wetu. Tuwekeze katika elimu, ubunifu, ushirikishaji wa vijana katika maamuzi, na kupambana na ufisadi unaoharibu maendeleo,” alifafanua Mheshimiwa Mbeki.

Ameongeza kuwa Bara la Afrika lina utajiri na uwezo mkubwa ambao unahitaji Viongozi wanaowaza zaidi ya uchaguzi, wasioogopa uwajibikaji, wenye maono, na wanaotanguliza maslahi ya wananchi wao na Taifa, kuliko matakwa yao binafsi.

Awali Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo alisema kila mwafrika lazima atakafari mafanikio, changamoto na matarajio ya kuinua maendeleo ya Afrika kwa amani ya utulivu.

Amesisitiza umuhimu wa kuwaenzi viongozi walioendeleza fikra za Uafrika na wanaoendelea kupigania ukombozi wa kiuchumi na mshikamano wa Bara la Afrika kwani wameacha urithi mkubwa kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho.

“Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Tanzania, nichukue nafasi hii kusema kuwa tunawakumbuka na kuwapongeza waanzilishi wa Umoja wa Afrika (OAU) — ambao ndoto yao ya kuunganisha na kushirikisha zaidi mataifa ya Afrika imeendelea kuishi hadi leo. Tunawakumbuka pia kwa heshima kubwa viongozi waliowafuata, ambao waliendeleza dhima ya Uafrika (Pan-Africanism) na wanaoendelea kupigania ukombozi wa kiuchumi na mshikamano wa bara letu tukufu,” alisema Mhe. Kombo

Hafla hiyo iliwakutanisha pamoja mabalozi , viongozi wa Serikali, Mabalozi wastaafu, viongozi wa serikali, wanadiplomasia, wasomi, pamoja na wawakilishi wa asasi za kiraia na kijamii kwa ajili ya kusherehekea mshikamano, utofauti na maendeleo ya Afrika.

Usiku huo ulipambwa na burudani mbalimbali za kitamaduni, vyakula kutoka nchi za Afrika, pamoja na tafakuri juu ya mchango wa mataifa ya Afrika katika historia na maendeleo ya sasa kuelekea amani na kujitegemea.

Hafla hiyo ilifanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 62 ya Umoja wa Afrika, ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za kuelekea maadhimisho ya Siku ya Afrika ambayo huadhimishwa tarehe 25 Mei ya kila mwaka.
.







RAIS DKT. SAMIA ATOA BILIONI 42.34 KULIPA FIDIA KWA WANANCHI WA MKOA WA ARUSHA

RAIS DKT. SAMIA ATOA BILIONI 42.34 KULIPA FIDIA KWA WANANCHI WA MKOA WA ARUSHA

May 24, 2025 Add Comment








Na Prisca Libaga RAS Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa kiasi cha shilingi bilioni 42.34 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha ili kumaliza migogoro ya ardhi na uendelezaji wa maeneo mbalimbali katika mkoa huo.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Moshono, Jijini Arusha, Mhe. Makonda amesema fidia hiyo imetolewa kwa maeneo kadhaa yaliyoguswa na miradi ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa barabara, uwanja wa ndege, maeneo ya jeshi, na uchimbaji wa madini.

Katika Jiji la Arusha, eneo la Losirwa lililokuwa chini ya matumizi ya Jeshi limepewa fidia ya shilingi Bilioni 2.27, ambapo fidia hiyo imekwishalipwa, eneo la Oloresho kwaajili ya maandalizi ya mashindano ya AFCON, limetengewa fidia ya shilingi bilioni 7.27, barabara ya Mianzini – Ngaramtoni nayo imelipwa fidia ya shilingi bilioni 3.49 ambapo fedha hizo zimelipwa tayari pamoja na eneo la barabara ya Mirongoine – Olmot limepokea fidia ya shilingi milioni 591.64 ambayo nayo imelipwa.

Aidha, Wilaya ya Arumeru, fidia kwa eneo la Jeshi lililopo Duluti imetolewa kwa kiasi cha shilingi bilioni 7.9 na tayari imelipwa yote kwa walengwa.

Wilaya ya Karatu imepata fidia ya shilingi bilioni 5.9 kwa ajili ya uwanja wa ndege wa Manyara uliopo katika eneo hilo, hatua inayolenga kufanikisha uboreshaji wa miundombinu ya usafiri wa anga.

Kwa upande wa Wilaya ya Monduli, eneo la Engaruka, ambalo linahusishwa na shughuli za uchimbaji wa madini ya magadi soda, limetengewa fidia ya shilingi bilioni 14.9, ikiwa ni sehemu ya uwekezaji wa kimkakati katika sekta ya madini.

Katika hatua nyingine, Mhe. Makonda amewataka viongozi wote wa Mkoa huo kuacha mara moja tabia ya kuwaondoa wananchi kwenye maeneo yao bila kuwapa fidia stahiki, akisisitiza kuwa serikali ya awamu ya sita inalenga haki, usawa na maendeleo ya watu na ndiyo dhamira ya Rais Dkt. Samia katika kulinda haki za wananchi na kusukuma mbele ajenda ya maendeleo ya Taifa.

RAIS DKT.SAMIA AWAAPISHA VIONGOZI ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI IKULU JIJINI DAR LEO

May 24, 2025 Add Comment

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Prof. Tumaini Joseph Nagu kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia masuala ya Afya kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Dkt. Blandina Bugazi Kilama kuwa Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango anayeshughulikia biashara na ubunifu kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.


Viongozi wateule wakiapa Kiapo cha Maadili kwenye hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Jaji Mstaafu John Samweli Mgetta kuwa Mjumbe wa Baraza la Maadili kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Mei, 2025.

RC BALOZI BATILDA :TAKWIMU NI NGUZO MUHIMU KATIKA MAENDELEO YA NCHI

May 24, 2025 Add Comment

 



Na Oscar Assenga,TANGA

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amesema kwamba takwimu ni nguzo na nyenzo muhimu katika kupanda utekelezaji wa mipango mbalimbali maendeleo duniani.

Dkt Batilda aliyasema hayo leo Jijini Tanga wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Baraza la Saba la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini (NBS) ambapo alisema kwamba mabazara hayo yana maada mkubwa kwa wafanyakazi.

Ambapo alisema kwamba Serikali inatambua jukumu hilo kubwa la (NBS) kuzalisha na kusambaza pamoja na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa takwimu rasmi kwa ajili ya kupanda utekelezaji wa mipango mbalimbali ya maendeleo katika nchi.

Alisema kutokana na hilo wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa utashi wake mkubwa wa kisiasa alionao katika kuendeleza Tasnia ya Takwimu nchini na wote wameona mafanikio yake .

“Wote tunaona kwa namna ya kipekee  Serikali ya awamu ya sita  imekuwa mstari wa mbele kuwezesha uzalishaji wa takwimu rasmi pamoja na matumizi ya takwimu katika mipango mbalimbali ya maendeleo na Dira bila takwimu hakuna kinachoendelea”Alisema

Hata hivyo aliipongeza timu ya  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa  umoja na mshikamano kutokana na takwimu huanzia katika uzalishaji,uchakataji wake,uhakiki wake mpaka usambazaji wake kutokana na kwamba  mtu moja hawezi kufanya pekee yake hivyo lazima wafanye kazi kwa ushirikiano.

Alisema kwamba wanaendelea kuhamasisha wenzao wajiunge kwebye vyama vya wafan yakazi hasa tughe ili waweze na kauli kubwa ambavyo itakuwa na maslahi mapana kwa nchi na sisi wenyewe.

Aidha aliwataka kuhakikisha wanafanya kazi kwa tija na uzalendo na kuongea nao waelewe dira na dhima ya taasisi zao na mambo ambayo hawataji kuyaona kwenye taasisi zao ikiwemo uvujaji wa siri.

“Katika mambo ambayo tunawapongeza sana NBS ni usiri mkubwa mlionao kwa kweli mnafanya kazi kubwa na sasa wanakwenda kwenye teknolojia ya habari tunaweza kuwa na usiri lakini mkaingiliwa kuna viti ya kimtandao inabidi tuendelee kujiimarisha sana kwa maana nyie ndio wamebeba roho ya nchi”Alisema

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kwa sababu taarifa zote zipo kwao kwa hiyo wajipange na moja ya maeneo ambayo watapaleka watu wengi kusoma ni masuala ya ulinzi wa kimtandao ili kuungana na kikosi kazi cha Serikali  ili kuhakikisha kwamba taarifa zinakuwa salama na hakuna jambo ambalo litaingizwa.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi (NBS) na Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt Amina Msengwa alimshukru Rais Dkt Samia Suluhu kwa kumteua kuwa Mtakwimu Mkuu wa Serikali anatambua heshima kubwa aliyopewa na kuhaidi kuendelea kusimamia ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa maelekezo na waledi mkubwa ili kuhakikisha majukumu ya NBS yanakwenda sambamba na kasi ya maendeleo ya Rais.

“Nimshukuru Kamisaa Anna Makinda kwa kuendelea kutusaidia katika ushauri lakini kusimamia mkakati wetu wa usambazaji wa matokeo ya Sensa na tunaendelea kujivunia kutoka kwake”Alisema

Aidha alisema kwamba kupitia ofisi ya Taifa ya Takwimu wanataka kuijenga Tanzania yenye maendeleo ya juu kabisa huku akieleza kwamba wamekuwa wakitekeleza sheria na kanuni za zinazoongoza uundaaji na uendeshaji  na u vikao vya mabaraza la wafanyakazi .

Naye kwa upande wake Kamisa wa Sensa na Spika wa Bunge Mstaafu Anna Makinda alisema  baraza la wafanyakazi ndio roho muhimu ambayo inaunganisha wafanyakazi na menejimenti ambapo alitumia wasaa huo kuwataka watumishi kujiunga kwenye mabaraza hayo kutokana na uwepo wa manufaa mbalimbali.

Mwisho