RAIS SAMIA APELEKA NEEMA TANGA
*📌Bilioni 20 kusambaza umeme katika vitongoji 180*
*📌Zaidi ya Kaya 5,940 kufikiwa*
*📌RC Tanga amshukuru Rais Samia, awasisitiza wananchi kuchangamkia fursa*
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 20 wa kusambaza umeme katika vitongoji 180 utakaonufaisha zaidi ya Kaya 5,940 Mkoani Tanga.
Hayo yameelezwa na Meneja Usimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy Mei 22, 2025 wakati wa kumtambulisha Mkandarasi aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi, Kampuni ya Transpower Limited na International Contractor Limited Jv kwa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian.
“Leo hii tupo hapa Mkoani Tanga kwa ajili ya kumtambulisha mkandarasi ambaye atatekeleza mradi huu wenye thamani ya shilingi 20,581,548,011.20,” alibainisha Mha. Lwena.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian alimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea mradi huo ambao alisema unakwenda kuongeza kasi ya maendeleo kwa wananchi wake na alimsisitiza mkandarasi kuhakikisha anatoa ajira kwa wananchi wa maeneo ya mradi.
“Wananchi wa Tanga tujitokeze kwa wingi kuchangamkia fursa, mradi unaotekelezwa ni mkubwa hivyo mbali na manufaa tutakayopata baada ya kukamilika kwa mradi lakini pia kuna fursa nyingi wakati wote wa hatua zote za utekelezaji wake ikiwemo ajira na biashara mbalimbali,” alisisitiza Mhe Dkt. Burian.
Akizungumzia utekelezaji wa mradi, Mhandisi Lwena alisema mradi unatekelezwa katika majimbo 12 ya uchaguzi na kwamba kwa kila jimbo vitongoji 15 vitafikiwa na mradi.
Alitaja majimbo ambayo ni Jimbo la Tanga, Pangani, Mkinga, Muheza, Korogwe Mjini, Korogwe Vijijini, Lushoto, Bumbuli, Mlalo, Handeni Mjini, Handeni Vijijini na Kilindi.
Alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa ya kuunganishiwa umeme ambapo alibainisha kuwa gharama ya kuunganisha umeme kupitia mradi huo ni shilingi 27,000 pekee.
“Katika mradi huu, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa ruzuku ili kila mwananchi aweze kuunganisha umeme kwa gharama ya shilingi 27,000, tumuunge mkono kwa kuchangamkia fursa hii,” alisisitiza Mha. Lwena.
Kwa upande wake mwakilishi wa Mkandarasi kutoka Kampuni ya Transpower Ltd, Mha. Cuthbert Shirima alisema kampuni hiyo inao uzoefu wa muda mrefu na aliahidi kufanya kazi kwa weledi na kukamilisha mradi huo kwa kipindi cha miezi 18 badala ya 24 iliyoainishwa katika mkataba.
TANESCO MUHEZA: KATIKATIKA YA UMEME ILITOKANA NA WIZI WA NYAYA ZA KOPA KWENYE TRANSFOMA
habariNa Paskal Mbunga, MUHEZA.
SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) katika wilaya ya Muheza Mkoani Tanga limetolea ufafanuzi katikakatika ya Umeme katika wiki mbili zilizopita ilitokana na kuibiwaa kwa wizi wa nyaya za kopa kwenye Transfoma 18 katika maeneo tofauti tofauti wilayani humo na hivyo kupelekea kuungua na kusababisha umeme kuzima.
Hayo yalisemwa na Meneja wa TANESCO wilaya ya Muheza African Chuwa wakati akizungumza na waandishi wa habari kutolea ufafanuzi suala hilo lililosababisha baadhi ya wananchi kulalamika, ambapo alisema jitahada zilifanywa ili kuurejesha umeme kwa haraka.
Alisema wakati wa zoezi la kurejesha umeme, walilazimika kufanya majaribio ili kutambua eneo lenye matatizo kwani wilaya hiyo pia inapeleka huduma ya umeme kwenye wilaya za Mkinga na Pangani.
Alibainisha kwamba kwa vile baadhi ya maeneo yanachukua umeme kutoka Muheza, na kwamba ili kubaini tatizo lipo upande upi, ilikuwa lazima kwanza kuurejesha umeme ili endapo itazima, watabaini changamoto ipo wapi. Alieleza kwamba wanaendelea kufuatilia vitendo vya wizi wa waya unaofanywa na baadhi ya watu uliosababisha b umeme kukatika mara kwa mara.
“Lakini niwaambie kwamba tatizo jingine linalosababisha umeme kukatikakatika ni matengenezo makubwa yanayofanyika pale kituo cha kuzalisha umeme Hale yanayopelekea kuzimwa kwa line inayokwenda Muheza na kusisitiza kwamba wanalazimika kuzima umeme wakati wa matengenezo wa line inayotoka Hale kwenda Songa na kwenda Muheza na line inayotoka Kituo cha Hale Songa kwenda Korogwe.
Hata hivyo alibainisha kwamba Ofisi ya TANESCO wilayani Muheza inatoa taarifa kwa wananchi ya uwepo wa matengenezo na kwamba wakati wa matengenezo hayo, umeme huzimwa. Meneja huyo wa TANESCO wilayani hapa alifahamisha kwamba kutakuwa na katikakatika kwa umeme wakati wa matengenezo yanayoendelea kwa kipindi cha miezi minne hadi mwezi Agosti, 2025 ambapo yatakuwa yamekamilika.
(Mwisho)
Tanzania na Umoja wa Ulaya kuendeleza Ushirikiano wa Kimkakati
habariNCAA YASHIRIKIANA NA JAMII INAYOZUNGUKA HIFADHI KUKABILIANA NA GUGU KAROTI
Na Mustapha Seifdine, Karatu.
Katika kuhakikisha mazingira ya hifadhi na shoroba za Wanyamapori yanabaki salama kwa uhifadhi endelevu, Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) imeendelea kushirikiana kwa karibu na wananchi wa vijiji vinavyopakakana na hifadhi ya Ngorongoro kupambana na mmea vamizi hatari uitwao Gugu Karoti (Parthenium hysterophorus) ambao umeota baadhi ya maeneo.
Hatua ya ushirikishaji wa jamii ni sehemu ya mpango wa kitaifa wa kudhibiti mimea vamizi nchini, hususan katika maeneo ya yaliyohifadhiwa na kuzilinda shoroba muhimu zinazounganisha mifumo ya ikolojia kama vile shoroba ya Upper Kitete inayounganisha hifadhi za Ngorongoro, ziwa Manyara na Tarangire.
![]() |
Afisa Uhifadhi darala la Kwanza Gregory Mtega kutoka NCAA akiongoza wananchi wa Kijiji cha Upper Kitete na baadhi ya wataalam ameeleza kuwa operesheni ya kung’o gugu karoti imefanyika kwa mafanikio makubwa kupitia ushirikiano kati ya NCAA, Halmashauri ya Wilaya ya Karatu na shirika la PAMS na kuongeza kuwa juhudi hizo zinaendelea katika vijiji vingine vinavyopakana na hifadhi kwa ajili ya kuhifadhi uoto wa asili, malisho ya mifugo, na maisha ya wanyamapori.
“Tumekuwa na utaratibu wa kutoa elimu ya uhifadhi shirikishi kwa wananchi wa vijiji vinavyozunguka hifadhi, NCAA kila mwaka tunatoa miche ya miti bure wananchi wapande kwenye maeneo yao, tunagawa mizinga ya Nyuki kuwainua kiuchumi na kupambana na Wanyama wanaoingia kwenye maeneo hayo, pamoja na programu hizo tumeamua pia kuwahusisha kwenye kung’oa mimea vamizi ili kulinda mfumo wa ikolojia kuwa imaraa, kuimarisha nyanda za malisho na kuwa na uhifadhi endelevu”
Mtega ameongeza kuwa Gugu Karoti ni mmea unaosababisha uharibifu mkubwa wa mazingira kwa kuwa unazaliana kwa kasi (mbegu zaidi ya 40,000 kutoka mmea mmoja!), na ni tishio kwa wanyamapori, mifugo, na hata kilimo cha wananchi hivyo mamlaka imewekeza juhudi za kutosha kukabiliana nalo kw akutumia njia mbalimbali.
Afisa Wanyamapori wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Kornelio Lengai, amepongeza ushirikiano wa NCAA na kueleza kuwa mmea huo umekuwa kikwazo kwa uzalishaji wa chakula na maisha ya wakazi wa vijiji vinavyozunguka hifadhi hivyo Jitihada za NCAA kushirikiana na wadau mbalimbali ni ishara nzuri katika uhifadhi endelevu kwa vizazi vijavyo.
Kwa upande wake, Emanuel Siriri, mkazi wa kijiji cha Upper Kitete, ameishukuru NCAA kwa kuendelea kutoa elimu na kuwashirikisha wananchi wa kijiji hicho ambapo jitihada hizo si tu zinaleta matumaini bali zimefungua fursa za kiuchumi kwa vijana kupitia kazi za udhibiti wa mmea huo ambao unapodhibitiwa unaboresha shughuli za kilimo na kupata mazao ya kutosha.