DKT .TULIA ATANGAZA KUGOMBEA JIMBO LA UYOLE

May 23, 2025 Add Comment


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ametangaza nia ya kugombea Ubunge katika jimbo jipya la Uyole mkoani Mbeya katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.


Dkt. Tulia ametoa tamko hilo leo tarehe 23 Mei, 2025 alipokuwa akihutubia Mkutano Mkuu Maalum wa Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo amesema kuwa ameamua kufanya uamuzi huo ili kuwahudumia wananchi wa Uyole kutokana na kasi ndogo ya maendeleo iliyopo katika eneo hilo.


“Maendeleo ya Uyole yanasonga kwa taratibu sana, nimeona ni vyema nijitoe kwa moyo wote kuhakikisha wananchi wa Uyole wanapata huduma stahiki na maendeleo ya haraka. Nitoe wito kwenu, watu wengi watakuja kwenu, chagueni kiongozi, chagueni mtumishi, itasaidia sana kuendelea kuyakimbiza maendeleo ya jamii," amesema Dkt. Tulia.

TBS YAWAKUMBUSHA WANANCHI UMUHIMU WA KUJIRIDHISHA NA TAARIFA ZA BIDHAA

May 22, 2025 Add Comment
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea kutoa msisitizo kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiridhisha na taarifa zilizo kwenye vifungashio vya bidhaa kabla ya kununua, likisema taarifa hizo ni sehemu muhimu ya uthibitisho wa ubora na usalama wa bidhaa husika.

RAIS SAMIA APELEKA NEEMA TANGA

May 22, 2025 Add Comment


*📌Bilioni 20 kusambaza umeme katika vitongoji 180*


*📌Zaidi ya Kaya 5,940 kufikiwa*


*📌RC Tanga amshukuru Rais Samia, awasisitiza wananchi kuchangamkia fursa*


Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 20 wa kusambaza umeme katika vitongoji 180 utakaonufaisha zaidi ya Kaya 5,940 Mkoani Tanga.


Hayo yameelezwa na Meneja Usimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy Mei 22, 2025  wakati wa kumtambulisha Mkandarasi aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi, Kampuni ya Transpower Limited na International Contractor Limited Jv kwa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian.



“Leo hii tupo hapa Mkoani Tanga kwa ajili ya kumtambulisha mkandarasi ambaye atatekeleza mradi huu wenye thamani ya shilingi 20,581,548,011.20,” alibainisha Mha. Lwena.


Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian alimshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea mradi huo ambao alisema unakwenda kuongeza kasi ya maendeleo kwa wananchi wake na alimsisitiza mkandarasi kuhakikisha anatoa ajira kwa wananchi wa maeneo ya mradi.

“Wananchi wa Tanga tujitokeze kwa wingi kuchangamkia fursa, mradi unaotekelezwa ni mkubwa hivyo mbali na manufaa tutakayopata baada ya kukamilika kwa mradi lakini pia kuna fursa nyingi wakati wote wa hatua zote za utekelezaji wake ikiwemo ajira na biashara mbalimbali,” alisisitiza Mhe Dkt. Burian.


Akizungumzia utekelezaji wa mradi, Mhandisi Lwena alisema mradi unatekelezwa katika majimbo 12 ya uchaguzi na kwamba kwa kila jimbo vitongoji 15 vitafikiwa na mradi.


Alitaja majimbo ambayo ni Jimbo la Tanga, Pangani, Mkinga, Muheza, Korogwe Mjini, Korogwe Vijijini, Lushoto, Bumbuli, Mlalo, Handeni Mjini, Handeni Vijijini na Kilindi.

Alitoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa ya kuunganishiwa umeme ambapo alibainisha kuwa gharama ya kuunganisha umeme kupitia mradi huo ni shilingi 27,000 pekee.


“Katika mradi huu, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa ruzuku ili kila mwananchi aweze kuunganisha umeme kwa gharama ya shilingi 27,000, tumuunge mkono kwa kuchangamkia fursa hii,” alisisitiza Mha. Lwena.


Kwa upande wake mwakilishi wa Mkandarasi kutoka Kampuni ya Transpower Ltd, Mha. Cuthbert Shirima alisema kampuni hiyo inao uzoefu wa muda mrefu na aliahidi kufanya kazi kwa weledi na kukamilisha mradi huo kwa kipindi cha miezi 18 badala ya 24 iliyoainishwa katika mkataba.

TANESCO MUHEZA: KATIKATIKA YA UMEME ILITOKANA NA WIZI WA NYAYA ZA KOPA KWENYE TRANSFOMA

May 22, 2025 Add Comment


Na Paskal Mbunga, MUHEZA.

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) katika wilaya ya Muheza Mkoani Tanga limetolea ufafanuzi katikakatika ya Umeme katika wiki mbili zilizopita ilitokana na kuibiwaa kwa wizi wa nyaya za kopa kwenye Transfoma 18 katika maeneo tofauti tofauti wilayani humo na hivyo kupelekea kuungua na kusababisha umeme kuzima.

Hayo yalisemwa na Meneja wa TANESCO wilaya ya Muheza African Chuwa wakati akizungumza na waandishi wa habari kutolea ufafanuzi suala hilo lililosababisha baadhi ya wananchi kulalamika, ambapo alisema jitahada zilifanywa ili kuurejesha umeme kwa haraka.

Alisema wakati wa zoezi la kurejesha umeme, walilazimika kufanya majaribio ili kutambua eneo lenye matatizo kwani wilaya hiyo pia inapeleka huduma ya umeme kwenye wilaya za Mkinga na Pangani.

Alibainisha kwamba kwa vile baadhi ya maeneo yanachukua umeme kutoka Muheza, na kwamba ili kubaini tatizo lipo upande upi, ilikuwa lazima kwanza kuurejesha umeme ili endapo itazima, watabaini changamoto ipo wapi. Alieleza kwamba wanaendelea kufuatilia vitendo vya wizi wa waya unaofanywa na baadhi ya watu uliosababisha b umeme kukatika mara kwa mara.

“Lakini niwaambie kwamba tatizo jingine linalosababisha umeme kukatikakatika ni matengenezo makubwa yanayofanyika pale kituo cha kuzalisha umeme Hale yanayopelekea kuzimwa kwa line inayokwenda Muheza na kusisitiza kwamba wanalazimika kuzima umeme wakati wa matengenezo wa line inayotoka Hale kwenda Songa na kwenda Muheza na line inayotoka Kituo cha Hale Songa kwenda Korogwe.

Hata hivyo alibainisha kwamba Ofisi ya TANESCO wilayani Muheza inatoa taarifa kwa wananchi ya uwepo wa matengenezo na kwamba wakati wa matengenezo hayo, umeme huzimwa. Meneja huyo wa TANESCO wilayani hapa alifahamisha kwamba kutakuwa na katikakatika kwa umeme wakati wa matengenezo yanayoendelea kwa kipindi cha miezi minne hadi mwezi Agosti, 2025 ambapo yatakuwa yamekamilika.



(Mwisho)

Tanzania na Umoja wa Ulaya kuendeleza Ushirikiano wa Kimkakati

May 22, 2025 Add Comment
Brussels, 21 Mei,2025

Tanzania na Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuendeleza ushirikiano wa kimkakati baina yao.