MADAKTARI WANAWAKE WA KIISLAM TANZANIA WAZINDUA MFUKO WA KUSAIDIA HUDUMA ZA AFYA KWA WATOTO WENYE UHITAJI

May 19, 2025 Add Comment

 

Katika kuunga mkono falsafa ya UTU NA MAENDELEO inayoasisiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Madaktari Wanawake wa Kiislam nchini wamezindua rasmi Mfuko wa Kusaidia Huduma za Afya kwa Watoto Wenye Uhitaji, unaojulikana kama Muslimah Medical Support Fund (MMSF).

Mfuko huu ni mwendelezo wa juhudi za kujitolea ambazo madaktari hao wamekuwa wakizifanya kwa muda katika utaratibu usio rasmi, ambapo wamekuwa wakisaidia watoto kutoka familia zisizo na uwezo kupata matibabu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mwenyekiti wa MMSF Dkt. Asha Omari Mahita alisema kuwa wazo hilo lilianza kupitia mawasiliano ya kawaida katika kundi la WhatsApp, baada ya madaktari kuguswa na mateso ya watoto wanaokosa huduma muhimu za afya kutokana na ukosefu wa rasilimali.

“Kwa mujibu wa maadili ya Uislamu, huduma ya afya ni haki ya msingi kwa kila binadamu. Tumeona ni wajibu wetu kusaidia kundi hili linaloathirika zaidi, kwa kuanzia na watoto, mpaka Sasa tumekwisha wakatia bima za Afya watoto 500 na malipo ya moja kwa moja hospitalini bila kujali ni dini gani” alisisitiza Dkt. Mahita.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mstaafu, Prof. Mussa J. Assad, aliwapongeza Madaktari hawa Wanawake kwa moyo wao wa kujitolea na kuonyesha mfano bora wa uwajibikaji wa kijamii. Alisisitiza umuhimu wa kutumia uzoefu wa madaktari waliostaafu ili kupanua huduma kwa walengwa zaidi.

“Mfuko huu unaonyesha dira sahihi ya mshikamano wa kitaifa na matendo yenye kugusa maisha ya wengi. Ninafurahishwa na muundo wa MMSF ambao ni himilivu na unaolenga kupanua wigo wa huduma kwa kushirikiana na wadau mbalimbali,” alisema Prof. Assad.

Waanzilishi wa MMSF wamesema wanatarajia kushirikiana na hospitali, taasisi, watubinafsi na wahisani mbalimbali ili kuhakikisha kuwa watoto kutoka familia zisizo na uwezo wanapata huduma za kitabibu zenye ubora bila vikwazo vya kifedha.

Katika malengo mengine Karibu wa MMSF Dr Khadija Ibrahim alisema malengo ya mbeleni ni pamoja na kusaidia ada kwa waschana waliokwana wanotaka kuwa madaktari na pia kuweka Kambi za kitabibu (Medical camp) vijijini.












WAOMBAJI MIKOPO YA ELIMU,TAFUTENI NAMBA ZA NIDA MAPEMA

May 18, 2025 Add Comment


Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga


Ni takwa la kisheria kwa waombaji wa mikopo ya elimu kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuwa na namba ya utambulisho (National Identification Number-NIN) au kitambulisho cha uraia kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili kuweza kuomba mikopo ya elimu.


Pamoja na kwamba takwa hilo la kisheria kwa miaka ya nyuma kwa mwombaji ambaye hakuwa na namba ya utambulisho au kitambulisho cha uraia aliweza kuomba na kupata mkopo, lakini kwa mwaka huu wa masomo wa 2025/2026, bila namba ya utambulisho au kitambulisho cha uraia, mwombaji atashindwa kuomba mkopo na hivyo kukosa mkopo.


Bodi ya Mikopo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa walifanya mkutano Mei 16, 2025 ambapo mkazo juu ya kila mwombaji  wa mkopo wa elimu kuhakikisha ana namba ya utambulisho au kitambulisho cha uraia uliwekwa bayana mbele ya vyombo vya habari na Watanzania kwa ujumla.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Dk. Bill Kiwia alisisitiza juu ya umuhimu wa waombaji kuwa na namba ya NIN. "NIN itaiwezesha HESLB kuwa na taarifa sahihi na za kipekee za kila mwanafunzi. Kwa kutumia NIN kutatuwezesha kuboresha uwezo wetu wa kufuatilia wanufaika waliokopeshwa baada ya kuhitimu. Tumeunganisha mifumo yetu ili kuwezesha kuhakiki taarifa za waombaji mikopo kupitia NIN. Tayari wataalamu wa Tehama kutoka pande zote mbili (HESLB na NIDA) wanashirikiana kuhakikisha mifumo yetu iliyounganishwa inafanya kazi kwa ufanisi," amesema Dk. Kiwia.


Kimsingi, serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Dk. Samia Suluhu Hassan, imekuwa ikisisitiza mifumo ya serikali kusomana ili kurahisisha utendajikazi na ufuatiliaji kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama). Kabla ya maboresho makubwa yaliyofanywa na HESLB kuhusiana na mifumo ya kidigitali, kulikuwa na changamoto ya kupata taarifa za wanufaika wahitimu ambao hawajarejesha mikopo ambayo ni fedha zilizotumika kuwasomesha elimu ya juu katika taasisi mbalimbali za elimu.


Kwahiyo, maboresho makubwa yamefanyika kwa HESLB kuungana na taasisi nyingine mbalimbali ili kuwa na mfumo wa pamoja ambao utarahisisha utendajikazi na ufuatiliaji. Sambamba na hilo, kwa kuzingatia gharama zilizopo katika elimu ya kati na ya juu yaani ada, chakula, malazi, vitabu, kudurufu matini (kutoa photocopy), mafunzo kwa vitendo; Watanzania wengi wanahitaji kuwezeshwa kifedha kupitia mikopo inayoratibiwa na HESLB.


Hivyo, niwashauri waombaji wa mikopo ambao hadi sasa hawana namba ya NIN kuomba namba hizo kupitia tovuti ya NIDA au kwenda kwenye ofisi za NIDA zilizopo katika Halmashauri na wilaya zao ili kupata namba ili kuweza kuomba mikopo pindi dirisha la maombi ya mikopo litakapofunguliwa rasmi na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kupata mikopo. 


Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, James Kaji, amesema NIDA wapo tayari kuwahudumia waombaji wa mikopo. "Tunafurahia wenzetu wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu wameona na kutambua jitihada zetu, pamoja na mambo mengine watatuunga mkono katika kutoa hamasa hii kwa vijana. Namba ya utambulisho wa Taifa (NIN) inapatikana ndani ya siku 5 baada ya kujisajili, na kadi ya NIDA inapatikana ndani ya siku 21 baada ya uthibitisho wa taarifa za mwombaji, hakikisha unapojisajili unapata kadi," amesema.


Dirisha la maombi ya mikopo linatarajiwa kufunguliwa mwezi Juni, 2025, ni vyema waombaji watarajiwa wasiokuwa na namba ya utambulisho au kitambulisho cha uraia wakaanza kufuatilia mapema badala ya kusubiri hadi muda wa kuomba mkopo ufike ndipo waanze kuhangaika kufuatilia. Ikumbukwe kuwa bila namba ya utambulisho, maombi ya mikopo hayataweza kukamilika. 


"Tunatarajia kufungua dirisha la maombi ya mikopo mwezi Juni, 2025, kwa mwaka wa masomo wa 2025/2026, namba ya utambulisho wa Taifa itakuwa hitaji la lazima katika kujaza fomu za maombi ya mikopo, hivyo waombaji wote wanapaswa kuwa na namba hii wakati wa kujaza maombi yao ya mkopo," alisisitiza Dk. Kiwia.


Dk. Reubeni Lumbagala ni Mwalimu wa Shule ya Sekondari Funguni ya wilayani Pangani mkoani Tanga.


Maoni: 0620 800 462.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA NI KIPAUMBELE CHA SERIKALI -MHANDISI MRAMBA

May 17, 2025 Add Comment


📌 *Ashiriki Marathon ya Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia*


📌 *Asema Nishati Safi ya Kupikia itapunguza uharibifu wa mazingira na kulinda afya*


Katibu Mkuu wa Wizara Ya Nishati Mha. Felchesmi Mramba amesema kuwa, suala la upatikanaji wa nishati safi ya kupikia ni moja ya vipaumbele vya nchi na kwamba Serikali inahakikisha kuwa Mpango Mkakati wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia unatekelezwa kwa kasi na kwa umakini ili kutimiza azma ya nchi kuhama kutoka matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia kwenda kwenye nishati safi.

Amesema hayo tarehe 17 Mei, 2025 jijini Dar es Salam wakati akishiriki Marathon ya Nishati Safi ya Kupikia oiyofanyika katika viwanja wa Oysterbay..


“Serikali imeamua kwenda nalo kasi suala hili la nishati safi ya kupikia ili kuepusha uharibifu wa mazingira kwani nishati ambayo si salama kama kuni na mkaa inatumika kwa kiasi kikubwa kwa kupikia hivyo tukitekeleza Dira hii, kwa kiasi kikubwa tutapunguza uharibifu wa mazingira pamoja na kulinda afya za wananchi.” Amesema Mramba

Mha. Mramba, amewapongeza waandaaji wa Marathon hiyo Shirika la Wafanyabishara Wanawake (TABWA) ambayo imelenga kuhamasisha Nishati Safi ya Kupikia  kwa Wananchi.

Aidha, amewaasa  Wadau mbalimbali kuzidi kujitokeza ila kuzidi kuendeleza mikakati ya kusambaza elimu ya Nishati Safi ya Kupikia kwa Watanzania wengi zaidi.












MATHIAS CANAL ACHANGIA VIFAA VYA MICHEZO SHULE MBILI ZA MSINGI IRAMBA//AMPA HEKO DKT MWIGULU NCHEMBA

May 17, 2025 Add Comment
Mshindi wa Tuzo za SAMIA KALAMU AWARDS na Afisa Mtendaji Mkuu wa WAZOHURU MEDIA Ndg Mathias Canal amechangia vifaa vya michezo katika shule mbili za Msingi ambazo ni Kiomboi Bomani na Kiomboi Hospitali.

TPDC Yadhamini na Kushiriki Mbio za Marathoni kwa Lengo la Kuelimisha Umma Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

May 17, 2025 Add Comment
 Baadhi ya wanachama wa TPDC Runners Club wakiwa katika picha ya pamoja