Benki ya CRDB yawakaribisha Wanahisa kwenye Mkutano Mkuu wa 30

May 14, 2025 Add Comment

 

Arusha 14 Mei 2025 - Benki ya CRDB imewataka wanahisa wake kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa, unaotarajiwa kufanyika Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya mafanikio tangu kuanzishwa kwa benki hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye hoteli ya Gran Meliá, jijini Arusha, ambapo Benki ya CRDB pia ilizindua Ripoti yake ya Mwaka 2024, inayoonyesha maendeleo makubwa ya kifedha, kiutendaji na kijamii yaliyopatikana katika kipindi hicho.
Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, amesema kuwa Mkutano Mkuu wa mwaka huu utakuwa wa kipekee kwani utatanguliwa na semina maalum kwa wanahisa na umma, itakayofanyika Ijumaa, tarehe 16 Mei 2025, katika ukumbi wa Simba, AICC. “Semina hii ya kihistoria itakuwa chini ya kaulimbiu yetu ya mwaka huu: ‘Miaka 30 ya Ukuaji wa Pamoja,’ na itafunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango. Ni fursa muhimu ya kutafakari mafanikio yetu ya pamoja, changamoto tulizozishinda, na mwelekeo wetu wa miaka ijayo,” amesema Dkt. Laay.

Ajenda mbalimbali zitajadiliwa katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB ni pamoja na uchaguzi wa wajumbe wa bodi, kuteua wakaguzi wa hesabu, kujadili mapendekezo ya maboresho ya Katiba ya Benki, kujadili na kupokea Taarifa ya Bodi ya Wakurugenzi, na Taarifa ya Hesabu zilizokaguliwa, pamoja na gawio kwa mwaka 2024 ambapo pendekezo la gawio la Sh 65 kwa hisa litawasilishwa sawa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa yamekamilika kwa asilimia 100. Nsekela amesema mkutano huo utafanyika kwa njia mseto “Hybrid Meeting” ili kutoa fursa kwa wanahisa wengi zaidi kushiriki moja kwa moja na kwa njia ya kidijitali. “Tumeweka muongozo wa jinsi ya kushiriki mkutano mkuu kwa njia ya mtandao kupitia tovuti yetu ya www.crdbbank.co.tz, mitandao yetu ya kijamii, lakini pia maelekezo yametumwa kwa ujumbe mfupi kwa Wanahisa,” amesema Nsekela huku akiwahakikishia kuwa Benki hiyo vizuri katika kuhakikisha wanashiriki bila chanagamoto yoyote.
Nsekela amewahamasisha wanahisa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu huo wa kihistoria, akisisitiza kuwa uwepo wao ni muhimu kwa ajili ya kushuhudia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika miaka 30. “Tumejenga taasisi imara inayotoa huduma bora, tumeongeza thamani kwa wanahisa, na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa letu. Hii ni fursa adhimu kwa kila mwanahisa kujivunia sehemu yake katika mafanikio haya na kushiriki kuamua mustakabali wa benki yetu katika miaka ijayo,” amesisistiza.

WMA YAHAKIKI VIPIMO ASILIMIA 99 YA LENGO

May 14, 2025 Add Comment
Veronica Simba - WMA

Serikali kupitia Wakala wa Vipimo (WMA) nchini imekagua na kuhakiki vipimo 1,013,859 ambavyo ni sawa na asilimia 99.2 ya lengo la kukagua vipimo 1,022,342 katika mwaka wa fedha 2024/2025.

TANZANIA,MOROCCO KUCHOCHEA USHIRIKIANO SEKTA YA NISHATI

May 14, 2025 Add Comment

 Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini Morroco

Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini
Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini


Sehemu ya wajumbe mbalimbali alioambatana nao Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko wakati wa mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Morocco, Mei 14, 2025.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali mara baada ya mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco.

katika mazungumzo hayo, Dkt. Biteko aliongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dennis Londo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na mwakilishi katika eneo la Morocco, Mhe. Ali Jabir Mwadini pamoja na Wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa  nishati vijijini (REA), Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC), Mei 14, 2025.


Naibu Waziri Mkuu na Waziri  wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akizungumza na Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu, Mhe. Leila Benali kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco, Mazungumzo hayo yamefanyika leo Mei 14, 2025 katika ofisi za Wizara ya Nishati nchini Morocco.



📌 Matumizi ya teknolojia kupewa kipaumbele Sekta ya Nishati


📌 Morocco wampongeza Rais Samia kwa usimamizi bora Sekta ya Nishati


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Tanzania na Ufalme wa Morocco zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa matumizi ya teknolojia katika Sekta ya Nishati ili kuiwezesha sekta hiyo kuwa na mchango endelevu nchini.


Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa  Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko alipokutana na Mwenyeji wake Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu wa Ufalme wa Morocco, Mhe. Leila Benali kuzungumza kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya nishati ili kuimarisha ushirikiano na nchi ya Morocco.


"Mwaka 2016 Tanzania na Morocco zilisaini hati ya makubaliano (MoU) ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya umeme, mafuta na matumizi ya nishati mbadala ili yapewe kipaumbele katika nchi hizo, ". Amesema Dkt. Biteko


Mhe. Dkt. Biteko amesema pamoja na maendeleo ya nishati yaliyofikiwa, bado nchi inahitaji uwekezaji zaidi katika sekta ya nishati mbadala ikiwa na matarajio ya kukuza shughuli za kiuchumi hususan katika sekta za viwanda na madini jambo ambalo linahitaji uwekezaji wa kimkakati zaidi katika sekta ya nishati.


Ametaja mambo mengine ni pamoja na kubadilishana uzoefu miongoni mwa wataalam katika sekta ya nishati ikilenga kuifanya kuwa na tija kwa taifa na uchumi kwa ujumla.


Kwa upande wake, Waziri wa Mageuzi ya Nishati na Maendeleo Endelevu wa Ufalme wa Morocco, Mhe. Leila Benali amesema kuwa Tanzania inaweza kubadilisha sura yake kwa kuwa na juhudi za pamoja za kuunganisha rasilimali zilizopo kuhakikisha nishati ya umeme inawafikia wananchi wengi zaidi. 


Amesema hakuna maendeleo yanayoweza kupatikana gizani hivyo, njia ya kuleta maendeleo na ustawi wa watu ni kuwaangaza maisha yao kwa kupitia sekta ya Nishati.


Aidha, Mhe. Benali amepongeza kwa dhati juhudi za Rais Samia kuwa kinara wa maendeleo ya nishati safi ya kupikia, Tanzania na Afrika kwa ujumla. 


Katika ziara hiyo, Dkt. Biteko ameongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dennis Londo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi katika eneno la Morocco, Mhe. Ally Mwadini, Wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa  Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC).


Mwisho.

SERIKALI INAENDELEA KUTEKEKEZA MIRADI YA UMEME KWENYE MAENEO YA KIMKAKATI-KAPINGA

May 14, 2025 Add Comment


*📌 Maeneo 300 tayari yamefikkwa*


*📌 Asisitiza gharama ya kuunganisha umeme Vijijini ni shilingi 27,000/-*


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye  maeneo ya kimkakati nchini ikiwemo maeneo ya migodi midogo,  maeneo ya uvuvi, Viwanda na  yanayochagiza shughuli za kiuchumi.


Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 14, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Mwibara, Mhe. Charles Kaijage aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali kuyapelekea umeme maeneo ya uvuvi ili kukuza uchumi wa wananchi wa maeneo hayo.

 

"Mheshimiwa Naibu Spika Mradi huu wa kupeleka umeme maeneo ya kimkakati umefikia zaidi ya maeneo 300 ikiwemo vituo vya afya na visima vya maji kwa maeneo ambayo yanatoa huduma za kijamii."  Amesema  Kapinga

Akijibu swali la Mbunge wa Igunga, Mhe. Nicholas Ngassa aliyeuliza lini Serikali itaanza usambazaji umeme kwenye Vitongoji vya Jimbo la Igunga. Mhe. Kapinga amesema  Jimbo la Igunga lina jumla ya Vitongoji 337 ambapo kati ya hivyo, Vitongoji 95 vimepatiwa umeme.


Ameongeza kuwa, katika Vitongoji 15 Wakandarasi wanaendelea na utekelezaji wa miradi kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili A (HEP IIA) na Vitongoji 69 zabuni imetangazwa kupitia Mradi wa Kupeleka Umeme Vitongojini Awamu ya Pili B (HEP IIB).


Amesema kuwa, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itaendelea kutenga fedha za kuvipelekea umeme vitongoji 158 vilivyosalia.


Amesisitiza kuwa, gharama ya kuunganisha umeme kwa maeneo ya Vijijini ni shilingi 27,000/- na kuongeza kuwa, kuna mradi utakaoanza hivi karibuni unaohusisha Vitongoji ambavyo havina laini kubwa ya umeme na vilivyo na kwenye laini kubwa ya umeme.

INEC YAHIMIZA WANANCHI MIKOA 16 KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI AWAMU YA PILI

May 14, 2025 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza na Watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ambayo yanahusisha waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki kutoka Kata zote za Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani. Zoezi la uboreshaji awamu ya pili linataraji kuanza Mei 16 hadi 22, 2025 sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la Wapiga Kura na vituo vitafunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 12:00 jioni. 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza na Watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ambayo yanahusisha waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki kutoka Kata zote za Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani. Zoezi la uboreshaji awamu ya pili linataraji kuanza Mei 16 hadi 22, 2025 sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la Wapiga Kura na vituo vitafunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 12:00 jioni. 
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Hidaya Gwandu akizungumza 
Mapema kabla ya kuanza kikao hicho Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Mei 14, 2025 amemtembelea na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge ofisini kwake. Mwenyekiti wa Tume na ujumbe wake wapo mkoa wa Pwani kwaajili ya zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambalo linaingia awamu ya pili katika mikoa 16 ya Tanzania Bara na Zanzibar ukiwepo mkoa wa Pwani pamoja na uwekaji wazi wa Daftari la awali la wapiga kura.
 ************************
Na Mwandishi wetu, Pwani
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka wananchi kutoka mikoa 16 ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar wanaokwenda kuanza Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu yapili kujitokeza kuboresha taarifa zao pamoja na kutazama daftari la awali la Wapiga Kura lililobandikwa katika vituo walivyotumia kujiandikisha au kuboresha taarifa zao hap[o awali.
 
Hayo yamesemwa leo Mei 14, 2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele wakati akizungumza na washiriki wa mafunzo ya siku moja ya watendaji wa Uboreshaji kutroka Halmashauri ya Mji wa Kibaha Mkoani Pwani.
 
“Niwasisitize watanzania wote katika mikoa hii 16, wajitokeze kuja kuboresha taarifa zao au kuja kujiandikisha kwasababu baada ya hapa Tume haita boresha tena Daftari…litaboreshwa kuanzia tarehe 16 hadi 22 Mei kwa muda wa siku saba,”alisema Jaji Mwambegele.
 
Aidha, mzunguko wa pili utahusisha mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16 hadi 22, 2025.
 
Katika hatua nyingine Jaji Mwambegele amewakumbusha watendaji hao wa uboreshaji ambao ni Waandikishaji Wasaidizi na waendesha vifaa vya Biometriki kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za Uchaguzi wakati wa utekelezaji wa awamu ya pili ya zoezi hilo litakalofanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura.
 
“Nawakumbusha tena kama nilivyowakumbusha katika zoezi lililopita, kwamba katika utekelezaji wa zoezi hili mzingatie sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi, muwe wanyenyekevu kwa wateja mtakao kuwa mnawahudumia,”alisema Jaji Mwambegele.
 
“Zoezi hilo linafanyika kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 16(5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya mwaka 2024 kinachoipa Tume jukumu la kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara mbili mara baada ya uchaguzi mkuu na kabla ya uteuzi wa wagombea kwa uchaguzi mkuu unaofuata.
 
Nae Afisa Mwandikishaji wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa amewataka wananchi wa Kibaha na viunga vyake kujitokeza kutazama daftari la awali lililowekwa wazi na kama kuna changamoto waweze kuziboresha wakati huu.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili ulianza kufanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 na kukamilika tarehe 04 Julai, 2025.
 
Uboreshaji wa Daftari unafanyika kwa mizunguko mitatu ambapo mzunguko wa kwanza ulihusisha mikoa 15, mzunguko wa pili mikoa 16 na mzunguko wa tatu utajumuisha vituo vya magereza na vyuo vya mafunzo.
 
Mikoa iliyohusika kwenye mzunguko wa kwanza wa uboreshaji ni pamoja na Iringa, Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 1 hadi 7 mwaka huu.
 
Mzunguko wa tatu wa zoezi la uboreshaji wa Daftari utahusisha vituo 130 vilivyopo kwenye magereza ya Tanzania Bara na vituo 10 vilivyopo katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar kwa wakati mmoja na utafanyika kwa muda wa siku saba kuanzia Juni 28 hadi Julai 04, 2025.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa awamu ya pili, utafanyika ngazi ya kata kwa Tanzania Bara na ngazi ya jimbo kwa Tanzania Zanzibar, ambapo jumla ya vituo 7,869 vitahusika, vituo 7,659 vipo Tanzania Bara na vituo 210 vipo Tanzania Zanzibar.
 
Katika awamu ya pili ya uboreshaji, wapiga kura wapya 1,396,609 wataandikishwa, wapiga kura 1,092,383 wataboresha taarifa zao na wapiga kura 148,624 watafutwa kwenye Daftari kwa kukosa sifa za kuendelea kuwepo kwenye Daftari,” amesema Jaji Mwambegele.
 
Mambo mengine ni kuhamisha taarifa za wapiga kura waliohama kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa  taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.
 
Aidha, kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 11(1) na (2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume pia ina jukumu la kuandaa Daftari la Awali la Wapiga Kura na kuliweka wazi kwa umma.
 
Lengo la uwekaji wazi wa Daftari hilo ni kutoa fursa kwa wananchi kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.
 
Tume iliboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 na kukamilisha tarehe 25 Machi, 2025.
Baadhi ya viongozi wa Halmashauri wanaoshughulika na Uboreshaji huo wakiwa katika mafunzo. 
Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza.


Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza.

Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza. 

Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia nasaha za Mwenyekiti wa Tume wakati akizungumza.