📌Rais Samia apewa kongole uhamasishaji nishati safi
📌REA, STAMICO kushirikiana uzalishaji wa Rafiki briquettes
📌Kiwanda cha Rafiki briquettes mbioni kujengwa Geita
📍Geita
Wakala wa Nishati Vijijini (REA), umepongezwa na Jeshi la Magereza kwa kuhamasisha, kuwezesha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 hapa nchini.
Hayo yemebainishwa na Mkuu wa Jeshi la Magereza mkoa wa Geita, ACP Jonam Mwakasagule wakati akizungumza na Bodi ya Nishati Vijijini (REB) mkoani Geita.
'Sisi kama Jeshi la Magereza tulikuwa tunapata shida sana hasa wakati tunatumia kuni kupika na kutupotezea muda mwingi porini na kuepuka hatari za kupoteza maisha," Amesema ACP Mwakasagule.
ACP Mwakasagule ameongeza kuwa, matumiz ya nishati safi katika jeshi hilo sasa yamepewa kipaumbe ili kujenga afya bora kwa kupunguza magonjwa ya macho na kifua yanayotokana na matumizi ya kuni wakati wa kupika chakula.
"Mhe. Rais amesema taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100 ziachane na matumizi ya kuni na mkaa na kuanza kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo gesi asilia, umeme, bayogesi na makaa ya mawe yaliyoboreshwa, ". Amesema Mha. Chinemba
Mwisho.