Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts
CHATANDA AZINDUA MSAADA WA KISHERIA INAYORATIBIWA NA KAMATI YA HAKI NA SHERIA YA UWT

CHATANDA AZINDUA MSAADA WA KISHERIA INAYORATIBIWA NA KAMATI YA HAKI NA SHERIA YA UWT

September 08, 2024 Add Comment





MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda, akizindua kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna_DODOMA


MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda ,amezindua kampeni ya msaada wa Kisheria inayoratibiwa na Kamati ya Haki na Sheria ya UWT yenye lengo la kuwasaidia wanawake na makundi maalum kupata haki ya msaada wa Kisheria nchini.

Bi.Chatanda akizungumza mara baada ya kuzindua kamati hiyo iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.

Amesema kuwa lengo la kampeni hiyo ni kuunga mkono jitihada za awamu ya sita chini ya uongozi wa Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kupitia kampeni ya Mama Samia Legal Aid Chini ya Wizara ya Katiba na Sheria inayofanya vizuri kwa sasa.

“Kampeni hii ya utoaji wa msaada wa kisheria itakuwa inafanya kazi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi yenye lengo la kutoa huduma za msaada wa kisheria na kuhakikisha upatikanaji wa haki sawa kwa wote kwa kuzingatia zaidi wanawake ,wasichana,watu wanaoishi na ulemavu na makundi mengine hatarishi,”amesema Bi.Chatanda

Amesema kuwa UWT pamoja na wadau wengine wanalenga kuhakikisha kwamba elimu ya kisheria na msaada wa kisheria inafika kwa watu wote hasa wanawake na makundi maalum.

“UWT inalenga kuchangia jitihada za kuhakikisha upatikanaji wa haki kwa wote kuhusiana na matatizo ya ardhi,matukio ya ukatili wa kijinsia kwa watoto na wanawake urithi,Ndoa,kesi za madai na jinai.”amesema

Aidha ametoa maagizo kwa makatibu wa mikoa na wilaya kama watendaji kutoa ushirikiano wa kutosha pindi zoezi hilo la utoaji msaada wa kisheria litakapoaza kila jumamosi ya mwisho wa mwezi na kuhakikisha ripoti ya uendeshaji wa zoezi hilo.

Pia ametoa rai kwa wananchi hasa wanawake nchini kutumia fursa hiyo ya utoaji wa msaada wa kisheria ambayo imekwenda kuanza leo hapa Dodoma na baadae kwenye mikoa yote nchini kwa siku zijazo.ambapo kwenye viwanja vya Chinangali itakwenda kufanyika leo na kesho Septemba 8,2024.


kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo na Naibu Waziri TAMISEMI, Zainab Katimba amesema imeanzishwa kampeni ya msaada wa kisheria itakayoanza kwenye mikoa 10 na kila jumamosi ya mwisho wa mwezi kwenye ofisi za UWT kutakuwa na watoa msaada kisheria.

Mhe.Katimba amesema kuwa Wanawake, watoto na watu wenye mahitaji maalum ndio walengwa kwenye kampeni hiyo na wameandaa program maalum kufikia watoto shuleni ili kupata elimu ya kujilinda na ukatili.


” Tunaandaa kanzi data ya mawakili ambao wako ndani ya UWT Ili kuwa na timu kubwa ya watu watakao toa msaada kisheria kwa wananchi katika Mikoa waliyopo,”amesema Mhe.Katimba


Aidha amefafanua kuwa Rais Dk.Samia aliona wananchi wanahitaji msaada ndio maana alianzisha kampeni ya msaada wa kisheria ya mama Samia ambayo imekuwa na matokeo chanya

Katika hatua nyingine amesema kupitia kampeni hiyo wametengeneza programu ya kuwafikia watoto na kuwajengea uelewa namna ya kuepuka vitendo vya ukatili.

“Kutakuwa na programu maalumu ambayo itaaenda kuwafikia watoto na kutoa uelewa namna wanavyoweza kuepuka na vitendo vya ukatili,”amesema

Naye Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma Pili Mbaga ,amesema kuwa uzinduzi wa Kampeni hiyo imekuja wakati mwafaka kukiwa na matukio mengi yasiyofaa katika jamii.

“Kampeni hii imekuja wakati mwafaka kutokana na mambo ambayo yamekuwa yakijitokeza na tunaamini itakuwa muarobaini wa matukio,”amesem



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda, akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda,akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.





Mwenyekiti wa Kamati ya Haki na Sheria ya UWT, Zainab Katimba ,akielezea malengo ya kampeni hiyo wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



KATIBU wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma Bi.Pili Mbaga,akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septe.ba 7,2024 jijini Dodoma.



MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Mhe.Subira Mgalu,akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septe.ba 7,2024 jijini Dodoma.



SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda (hayupo pichani), wakati wa uzinduzi wa kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda, akizindua kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.



MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Marry Chatanda,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua kamati ya Haki na Sheria ya UWT,iliyoenda sambamba na uzinduzi wa kampeni ya msaada wa kisheria leo Septemba 7,2024 jijini Dodoma.

MONGELLA AKUTANA NA WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM WILAYA YA SHINYANGA MJINI

September 07, 2024 Add Comment


Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Mongella, leo Septemba 6, 2024, amekutana na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Shinyanga mjini, wajumbe wa baraza la jumuiya, na mabalozi katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini.

Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM pamoja na viongozi wa serikali, akiwemo wakuu wa idara wa Manispaa ya Shinyanga.

Mongella ameanza ziara ya siku saba mkoani Shinyanga kwa lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2024 na kuimarisha uhai wa chama. Katika ziara hiyo, atafanya mikutano ya hadhara na ya ndani ili kusikiliza changamoto zinazowakabili wananchi wa mkoa wa Shinyanga.

Ziara hiyo itamfikisha katika maeneo ya Shinyanga Vijijini, Kahama, Msalala, Kishapu, na Ushetu, ambako atakutana na viongozi wa chama na wananchi kujadili namna bora ya kuimarisha utekelezaji wa sera za chama kwa maendeleo ya mkoa.

Pia, ziara hii inalenga kuwahamasisha wanachama wa CCM kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama na kushughulikia kero za wananchi.










CPA MAKALA ATAKA UJENZI JENGO LA GHOROFA SITA HOSPITALI YA MBAGALA KUKAMILIKA KWA WAKATI, AKUMBUSHA MWAKANI WANA JAMBO

August 29, 2024 Add Comment

 Na Mwandishi Wetu


KATIBU wa Itikadi,Uenezi na Mafunzo CPA Amoss Makala ametoa maelekezo kwa mkandarasi anayejenga jengo la ghorofa sita la Hospitali ya Mbagala mkoani Dar es Salaam kuhakikisha ifikapo Juni mwaka 2024 liwe limekamilika na kuanza kutoa huduma.

CPA Makala ametoa maelekezo hayo baada ya kufanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa Hospitali ya Mbagala ikiwa ni sehemu ya ratiba ya kuangalia utekelezaji wa miradi mbalimbali inayoendelea katika Mkoa wa Dar es Salaam.

"Nimeridhishwa na kasi ya ujenzi wa Hospitali ya Mbagala ya Wilaya kwani hatua ambayo imefikia ni nzuri lakini niwakumbushe hakikisheni hadi Juni mwakani hospitali hii iwe imekamilika na ukizingatia mwakani tunajambo letu,hivyo lazima hospitali ikamilike mambo yawe mazuri,"amesema CPA Makala.

Amesema ujenzi wa hospitali hiyo utakapokamilika utagharimu Sh.bilioni na kwamba Chama Cha Mapinduzi kinamshukuru Rais DK.Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Taifa kwa kuridhia na kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Mbagara Rangi Tatu.

"Ujenzi wa hospitali hii wakati unaanza nikiwa Mkuu wa Dar es Salaam nilisimamia mchakato tangu ulipokuwa unaanza mpaka kumpata mkandarasi na sababu ni mahitaji makubwa ya huduma ya afya.Idadi ya watu Mbagala na Temeke ni kubwa."

"Nawapongeza Meya na madiwani kwa kuhakikisha dhamira ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kuleta huduma karibu na wananchi.Mmmeamua kujenga ghorofa na tunafahamu changamoto ya ya maeneo hivyo tuliamua kujenga ghorofa.

"Baada ya kuona kuna changamoto ya elimu katika mkoa wa Dar es Salaam tulipata fedha lakini shida ilikuwa maeneo, hivyo nilitoa maelekezo nikiwa Mkuu wa Mkoa huu tuanze kujengaSekondari za ghorofa na hata katika hospitali hii ujenzi wake ni wa ghorofa.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mbagala Abdallah Chaurembo amesema wanamshuru Raia Dk.Samia Suluhu Hassan kutoa fedha Sh.bilioni mbili kwa ajili ya kuanza ujenzi huku wao pia wakitenga fedha kila mwaka kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu amemshukuru CPA Makala kwa kufanya ziara katika majimbo ya 10 ya Mkoa huo na ziara yake imekuwa na mafanikio makubwa.






CCM TANGA YATAJA VIGEZO VITAKAVYOTUMIKA KUWAPATA WAGOMBEA WA UDIWANI, UBUNGE TANGA 2025

June 17, 2024 Add Comment

 



Na Oscar Assenga, PANGANI

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga kimesema kuwa vigezo ambavyo vitatumika kuwapata wagombea kwenye chaguzi za Serikali za Mitaa mwaka huu na ule Mkuu wa Wabunge na Madiwani wa mwakani 2025 kwamba ni wale ambao wanashiriki kwenye vikao kuanzia ngazi ya mashina.

Vigezo hivyo vilitangazwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman wakati aliposhiriki kwenye mkutano wa Shina namba 5 Mtaa wa Majengo Kata ya Pangani Mashariki ambapo pamoja na mambo mengine alihamasisha wananchi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura wakati utakapofika.

Katika mkutano huo wa Shina namba 5 Mwenyekiti huyo aligawa viti 100 ikiwa ni kuhakikisha wanakuwa na uchumi imara ambao utawawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi katika shina hilo

Alisema kwamba wanahitaji wapate viongozi ngazi ya serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 wa Ubunge na Madiwani ambao wanakiheshimu chama cha Mapinduzi.

Alisema kwamba tafsiri ya kukiheshimu chama hicho ni kuhudhuria mikutano ya mashina yako na waanapokuwa hawaudhurii maanake bado haujaonyesha kukithamini na kukipenda chama cha mapinduzi.

“Niwaambie kwamba sio hiari ni suala la lazima viongozi wa ngazi za mbalimbali wakiwemo Mwenyekiti wa wilaya, Kata na Mitaa na Vitongoji kuhudhuria kwenye mikutano ya mashina na kwa sasa atakayechukua fomu na kujaza na kueleza mikutano ya shina amehudhuria mara tano wakati hajafanya hivyo tutafuatulia maana mikutasari ipo”Alisema

“Sio suala la Hiari ni lazima kuhakikisha viongozi wa ngazi za wilaya wahudhurie mikutano ya shine lake ,Mwenyekiti wa Kata, Mbunge,Diwani hilo ni jambo la msingi linahimizwa kwenye chama chetu lazima wahudhurie kufanya hivyo ndio kukitendea haki chama chetu ujumbe huo ni kwa viongozi wote wa mkoa wa Tanga kwa sababu ndi anadhama nao na wote”Alisema Mwenyekiti huyo.

Aidha alisema kwamba suala la viongozi hao kuhudhuria kwenye mikutano hiyo ya mashina yao sio suala la hiari ni suala la lazima na mtakumbuka wakati najaza fomu kwenye uchaguzi wa chama 2022 ile fomu inavipengelea vingi miongoni mwao ilitaka ueleza vikao ambavyo ulivyoshiriki vya CCM kwa nafasi yako.

“Kwa maana lazima ueleze mikutano ya shina umehudhuria mara ngani kwa maana vikao vya matawi na mikutano mashina umehudhuria mara ngapi hilo ni suala la lazima na mara nyingi tumekuwa tukifanya mazoea kuona jambo la kawaida kawaida”Alisema

“Niwahakikishie uchaguzi unaokuja wa Serikali za Mitaa Vijiji na Vitongoji na Mkuu wa Mwakani 2025 wa uchaguzi wa kumchagua Rais, Ubunge na Madiwani kipaumbele cha kwanza cha watakaopewa kwenye kugombea ni wale wote ambao wanashiriki vikao na mikutano ya matawi na mashina ya CCM”Alisema

Aidha alisema kwamba atakayejaza fomu na kueleza mikutano ya shina amehudhuria mara tano na hajawahi kufanya hivyo watafuatilia maana mikutasari ipo kwa nafasi hiyo nyeti wanayotaka kumpa huyo mtu wanajua lazima akakiheshimu chama hivyo lazima wapate kumbukumbu zake kwa usahihi na kwa uhakika.

“Kwa hivyo wale wote wanaotarajia kugombea nafasi kwenye chama chao kwenye kura za maoni wajue kama kwenye mashina yao hawakuheshimu vikao vya mashina waliviona havina maana yoyote balozi balozi maana balozi kazi tuliomuachia ni kusuluhusha ndoa za watu”Alisema Mwenyekiti.