Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

WAZIRI MCHENGERWA AIPONGEZA TIMU YA WANAWAKE YA KRIKETI KWA KUONGOZA RWANDA

June 15, 2022 Add Comment

 

Na John Mapepele

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa ameipongeza timu ya Tanzania ya  Wanawake ya Kriketi kwa kufanya vizuri na kuongoza kwenye mashindano ya Kwibuka Cup yanayoendelea nchini hivi sasa nchini Rwanda.

Mhe. Mchengerwa ametoa pongezi hizo leo Juni 15, 2022 alipoongea na simu timu hiyo kupitia kwa Nahodha wa timu hiyo .

Amesema anaipongeza timu hiyo  baada ya kuzishinda timu zote walizokutana nazo kwenye mashindano hayo na kuwa kinalani mwa mashindano hayo.

Amezitaja timu hizo kuwa ni Kenya, Uganda, Rwanda, Botswana na  Ujerumani  bado timu ya Nigeria na Brazil ambapo wakishinda mechi mojawapo wanaingia fainali za mashindano hayo.

Aidha, amemshukuru Balozi wa Tanzania nchini Rwanda Mhe.  Meja Jenerali Richard Makanzo  kwa kuwa karibu na timu hiyo katika kipindi chote huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuisaidia timu hiyo ili ifike mbali zaidi.

WAZIRI MCHENGERWA AFANYA MAZUNGUMZO NA NGULI WA FILAMU WA NIGERIA

June 14, 2022 Add Comment

 



Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amekutana na msanii nguli kutoka Nigeria Jim  Iyke na kufanya mazungumzo ya mashirikiano katika kuandaa filamu za kimkakati za pamoja baina ya Tanzania na Nigeria 

Mazungumzo haya yamefanyika leo Juni 14, 2022 jijini Dodoma  ambapo wamekubaliana  kuwa na mashirikiano  kwenye filamu za kimkakati kwa faida za pande zote mbili.

Aidha,  Mhe. Mchengerwa amesema mashirikiano hayo yataifanya Tanzania kunufaika zaidi kwa kufanya kazi na manguli wa filamu wa Nigeria ambao wanawapenzi  wengi duniani.

Waziri Mchengerwa ametumia fursa hiyo kuwakaribisha watu mbalimbali duniani kuja kuwekeza  kwenye sekta ya Sanaa na Michezo.

Ameongeza kuwa kwa sasa  tayari imeshusha kodi ya zuio katika biashara ya filamu kutoka asilimia 15 hadi 10 ili kuyapa unafu

TANZANIA NA MAREKANI ZAJADILI USHIRIKIANO KATIKA MICHEZO NA SANAA

June 08, 2022 Add Comment

 






Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa wakiambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi wamekutana na Balozi wa Marekani hapa nchini leo Juni 8, 2022 wamekutana jijini Dar es salaam na kujadili masuala mbali mbali ya sekta za ikiwa ni pa moja na ujio wa msanii mashuhuri wa uchoraji ,Ashley Collins hapa nchini.


Wakizungumza katika  kikao hicho ambacho Mhe. Balozi  wa Marekani nchini Tanzania Dkt. Donald Wright ameambatana na Afisa Uhusiano wa Ubalozi huo, James Rodriguez wamejadili pia ujio wa Timu ya wachezaji nguli wanawake ya mchezo wa kikapu wa ligi  ya NBA nchini Marekani  hapa nchini ambao watakuja Tanzania kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wachezaji wanawake wa mchezo huo hapa nchini. 


Mhe. Mchengerwa amesema viongozi hao wamekubaliana  kuendeleza  malengo ya Royal Tour kwa kushirikiana zaidi  kwenye kuendeleza sekta  za sanaa na michezo ikiwemo kuendeleza  filamu za hapa nchini za “Swahiliwood” ili ziwe  katika  kiwango cha kimataifa kama zile za nchini Marekani kwa kupata walaam ambao watasaidia katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa miswada (script)


Amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na maeneo ya kipekee ya kuchezea  filamu ambazo zingeweza  kuwa bora na kusisitiza kuwa ni azma ya serikali kujenga mazingira  wezeshi ikiwa ni pamoja na kuangalia kodi mbalimbali ili kuwavutia wageni kuja  kurekodia  hapa nchini.


Aidha amesema eneo jingine ambalo limejadiliwa ni pamoja na kutoa mafunzo maalum katika eneo la haki miliki na hakishiriki kwa kazi mbalimbali za wasanii ikiwa ni pamoja na tuzo za muziki na Kwa upande mwingine amesema wamejadili namna ya kushirikisha wataalam kwenye program maalum ya kuibua vipaji vya wasanii na wanamichezo ya mtaa kwa mtaa.

UONGOZI WA WIZARA WAITAKA TEMBO WARRIORS KUTUMIA MECHI ZA ULAYA KUSHINDA KOMBE LA DUNIA, WAIAGA RASMI LEO

June 08, 2022 Add Comment

 





Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na michezo.Mhe, Mohamed Mchengerwa ameitaka Timu ya soka ya walemavu ya (Tembo Warriors) kutumia mechi za maandalizi na nchi mbalimbali za Ulaya kujinoa ili kushinda kombe  hilo na kulirejesha nchini.


Mhe Mchengerwa ametoa kauli hiyo leo Juni 8, 2022 uwanja wa Benjamini Mkapa wakati akiikabidhi bendera ya Taifa timu hiyo akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi inayokwenda kuanza kucheza mashindano kwenye maandalizi na timu  mbalimbali za Ulaya kwa kuanzia na timu ya Poland ili kuweza kupata uzoefu wa kucheza na nchi za mabara mbalimbali  kabla ya kuanza mashindano haya.


“Tumeamua kama Serikali kuendelea kuhaakikisha kuwa tunazisaidia timu zinazofanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa ili kuwasaidia kukuza ajira na kuwafanya  waajiriwe  kwenye vilabu  vikubwa  duniani” amefafanua Mhe. Mchengerwa 


Amesema watanzania wamechoka kuona kuwa nchi inasuasua kwenye michezo na amesisitiza kuwa  wakati huu watanzania wanataka  kombe  la dunia kuja  Tanzania ambapo amesema  hilo litafanikiwa kwa kuweka mbele utaifa na uzalendo wanapokuwa kwenye mashindano haya.


Ameongeza kuwa jambo kubwa kwa sasa ni kuwa na nidhamu na kuzingatia misingi ambayo wanapewa na  makocha wa timu zao ili waweze  kufika mbali na kuboresha  maisha yao na uchumi wan chi yetu kwa ujumla.


“Naomba kuwaambia mkifanya vizuri katika mashindano  haya ya maandalizi tu nina uhakika  mtanunuliwa na timu kubwa na mtabaki ulaya, mtabadilisha maisha ya familia zenu na watanzania kwa ujumla” ameongeza Mhe. Mchengerwa


Wakizungumza kwa nyakati tofauti  viongozi wa timu hiyo  wamemwahidi Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kuwa wanakwenda  kuanza kutema cheche  katika maandalizi ya timu hizo za awali ili kujihakikishia  kutwa kombe hilo.


Katibu Mkuu. Dkt, Abbasi amesema  Tembo Warriors ndiyo timu ya kwanza nchini kufuzu kuingia kwenye mashindano hayo na kuitaka kuendelea kushikilia heshima  hiyo kwa kuwa timu ya kwanza kurejesha kombe  nyumbani.

TIMU ZA SERENGETI GIRLS NA TEMBO WARRIORS WAPEWA HESHIMA YA MASHUJAA TAIFA NA BUNGE.

June 07, 2022 Add Comment

 



SPIKA wa Bunge Tulia Ackson akizungumza Bungeni wakati wa Timu ya wanawake ya soka chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Girls) ilipowasili bungeni


Na John Mapepele  

Timu ya wanawake ya soka chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Girls) imeweka  historia  ya kuwa  timu ya  kwanza kupewa heshima na Bunge la Jamhuri ya Muungano kuingia  na kukaa kwenye viti vya mawaziri ndani ya bunge  baada ya kufuzu kuingia  mashindano ya dunia ikiwa ni heshima ya mashujaa wa Taifa kwa kazi kubwa iliyoifanya ambapo kesho ni zamu ya Timu ya soka ya Taifa ya Walemavu ya (Tembo Warriors) ambayo pia imefuzu  mashindano ya dunia ya soka kwa walemavu.

Akiongea   mara baada ya kuketi eneo hilo rasmi la mawaziri, Waziri mwenye dhamana ya Michezo nchini. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema ushindi huo unatokana  na jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan za kuiwezesha  timu hiyo katika kipindi chote cha  maandalizi wa  mashindano hayo.

“Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan kwa kutuwezesha, kututia moyo na kutufuatilia kwa karibu sana katika kipindi chote” amefafanua Mhe. Mchengerwa.

Aidha, amesema Serikali itahakikisha inaendelea kuisaidia timu hiyo ili iweze kwenda  na kushinda kwenye mashindano hayo hatimaye kurejesha kombe hilo  la dunia na kuwataka wadau mbalimbali kushirikiana na Serikali katika kuwatia moyo  na kuwasaidia ili washinde.

Akizungumzia jinsi  timu ilivyopambana hadi kufika hapo amesema  kuwa  timu ilianza kuchabanga  Botswana magoli 11-0, ikaitandika  Burundi jumla ya magoli 6-1, na ikamalizia na kuibamiza timu ya Cameroon jumla ya magoli 5-1.

Kwa upande wa Warriors amesema iliishindilia Cameroon mabao 5-0, kabla ya kuikandamiza Senegal goli 1-0 na kuichakaza Morroco magoli 2-0.

Ameongeza kuwa dhamira ya Serikali ni kuendelea kufanya mapinduzi makubwa katika sekta za michezo na Sanaa ili kuipeleka Tanzania kimataifa ambapo amefafanua kuwa kuanzia Februari mwaka huu timu zote za taifa zinazoshiriki kwenya mashindano ya kimataifa  zimewekwa kambini na zinagharimiwa na Serikali.

Kwa upande wake Nahodha wa timu hiyo Noela Luhala alipewa heshima ya kuzungumza mbele ya Bunge tukufu ambapo amesisitiza kuwa kama ilivyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano. Mhe, Mama Samia Suluhu Hassan kuwa mwanamke wa kwanza kuwa Rais nchini ni ndoto za muda mrefu kwa timu hiyo kuwa ya kwanza kuingia mashindano ya Kombe la Dunia na kuwa Timu ya kwanza kulileta kombe hilo nchini.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania. Mhe Tulia Ackson ameipongeza timu hiyo kwa  niaba  ya bunge zima na kuwataka  kurejea na kombe hiyo  kwenye mashindano hayo.