Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

PROF. CAROLYNE NOMBO ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA KAMPASI YA MZUMBE TANGA

July 03, 2025 Add Comment
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo ametembelea eneo la ujenzi wa Kampasi mpya ya Chuo iliyopo Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, mnamo tarehe 2 Julai 2025 na kuridhishwa na kasi ya ujenzi huo. Ziara hiyo imelenga kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kampasi hiyo ikiwa ni ufadhili wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET).

REA YAJA NA MPANGO KABAMBE WA KUWEZESHA UJENZI WA VITUO VYA MAFUTA VIJIJINI

July 03, 2025 Add Comment
-Mkopo wa hadi Shilingi Milioni 133 kwa riba ya 5%-7% kutolewa

EWURA YAENDELEA KUTOA ELIMU KWENYE MAONESHO SABASABA

July 02, 2025 Add Comment
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake na namna ya kushiriki katika ufuatiliaji wa huduma za nishati na maji nchini, kupitia ushiriki wake kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.

WMA Yatoa Onyo Kali kwa Wafanyabiashara Wahujumu Vipimo vya Mafuta

July 02, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MENEJA wa Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) Kitengo cha Bandari, Alfred Shungu amesema kuwa wafanyabiashara wanaobainika kuhujumu vipimo vya mafuta, hasa kwa kutumia vifaa visivyotimiza viwango, watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kifungo au faini isiyozidi Shilingi Milioni 20 kwa kosa la kwanza.

MTENDAJI MKUU ADEM ASISITIZA UMUHIMU WA MAAFISA ELIMU KATA NCHINI KUJENGEWA UWEZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA ELIMU

July 02, 2025 Add Comment
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, ameeleza Maafisa Elimu Kata wanawajibika kusimamia shughuli za elimu kwenye ngazi ya Kata, hivyo ni muhimu Maafisa hao kujengewa uwezo kuhusu usimamizi fanisi wa shughuli za elimu ili kuchagiza maendeleo ya sekta ya elimu katika ngazi ya Kata.