WAZIRI MAVUNDE ATAKA WATANZANIA KUPEWA KIPAUMBELE KUSAMBAZA BIDHAA NA HUDUMA MIGODINI
habari▪️Aelekeza mabadiliko ya Kanuni ili kuruhusu uhaulishwaji teknolojia kwa Kampuni za Kigeni
▪️Ataka Watanzania kuchangamkia Trilioni 5.3 za usambazaji bidhaa na utoaji huduma
▪️Rais Samia apongezwa kwa uongozi wa maono
▪️Watanzania 19,371 wanufaika na ajira rasmi
▪️Kamati ya Bunge yaipongeza Wizara kwa ukuaji wa sekta
MWANZA
Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde ameitaka Tume ya Madini kuwapa kipaumbele watanzania kwenye usambazaji wa huduma na bidhaa kwenye migodi ya madini ili kujipatia kipato, kuongeza mzunguko wa fedha nchini hivyo Sekta ya Madini kuendelea kuwa na mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa.
Mhe. Waziri Mavunde ameyasema hayo mapema leo Juni 17, 2025 jijini Mwanza kwenye ufunguzi wa Jukwaa la Nne la Utekelezaji wa Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini linalokutanisha wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Wizara ya Madini na Taasisi zake, Taasisi za Serikali, Taasisi Binafsi, Taasisi za Fedha, Kampuni za Uchimbaji wa Madini na Watoa Huduma kwenye Migodi ya Madini.
Amesema kuwa katika kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini na kuhakikisha watanzania wananufaika na rasilimali madini, Serikali imeendelea kusimamia ipasavyo Sheria ya Madini, Sura 123 Kifungu Na. 102 na Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania za Mwaka 2018 ili kuweka usimamizi thabiti katika utekelezaji wa masuala ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini nchini.
Amesisitiza kuwa lengo la uwepo wa Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini ni kuhakikisha watanzania wanashiriki ipasavyo kupitia usambazaji wa bidhaa na huduma kwenye migodi ya madini badala ya kampuni kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi.
Aidha Mhe. Mavunde ameitaka Tume ya Madini kufanya mabadiliko ya Kanuni ili kuruhusu uhaulishwaji teknolojia kwa Kampuni za Kigeni ambapo itatoa fursa kwa kampuni za kitanzania kushirikiana na kampuni za kigeni kwenye utoaji wa huduma migodini na kujifunza teknolojia mpya kutoka kampuni za kigeni.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mavunde amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake makubwa ya kuendeleza Sekta ya Madini hali iliyopelekea mabadiliko makubwa ambapo mpaka sasa mafanikio makubwa yamepatikana.
“Mpaka sasa mafanikio makubwa yamepatikana hasa kwa wachimbaji wadogo ambapo wameanza kukopesheka kutoka kwenye Taasisi za Fedha, ushiriki wa watanzania kwenye shughuli za uchimbaji, uchenjuaji, biashara ya madini na utoaji wa bidhaa na huduma kwenye migodi ya madini umeongezeka na mchango wa wachimbaji wadogo kwenye makusanyo ya maduhuli umeendelea kuimarika,” amesisitiza Mhe. Mavunde.
Akielezea mafanikio ya utekelezaji wa kanuni za ushirikishwaji wa watanzania katika Sekta ya Madini, Waziri Mavunde amesema katika kipindi cha mwaka 2023/2024 jumla ya ajira rasmi 19,874 zilizalishwa katika migodi ya madini ambapo ajira 19,371 sawa na asilimia 97 zilitolewa kwa Watanzania na ajira 503 sawa na asilimia 3 zilitolewa kwa wageni.
![]() |
Aidha, amewataka watanzania kuchangamkia fursa za uwekezaji katika Sekta ya Madini hasa kwenye usambazaji wa bidhaa na huduma kwenye migodi ya madini kama vile usambazaji wa vifaa, vyakula na huduma na kuzitaka Taasisi za Kifedha kuendelea kuwakopesha mitaji.
Amesema kuwa kampuni za madini zinatumia kiasi cha shilingi Trilioni 5.3 kila mwaka kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa na huduma zinazotumika migodini na kuwataka watanzania kuchangamkia fursa hizo.
Naye Mkuu wa Wilaya Ilemela, Mhe. Hassan Masala akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda amempongeza Waziri Mavunde kwa usimamizi mzuri wa Sekta ya Madini hali iliyopelekea mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na ongezeko la wawekezaji nchini.
Ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kuwekeza katika mkoa wa Mwanza hasa katika eneo la uchimbaji wa madini na utoaji wa huduma mbalimbali kwenye migodi ya madini.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo amesisitiza kuwa Wizara ya Madini itaendelea kufungamanisha Sekta ya Madini na sekta nyingine muhimu za kiuchumi ili kuongeza ushiriki wa watanzania kwenye shughuli za madini nchini.
Wakati huohuo akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Dkt David Mathayo, Mbunge wa Ilemela, Dkt. Angeline Mabula amepongeza kazi kubwa inayofanywa na Waziri Mavunde hali iliyochangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa.
“Kupitia uongozi wa Mhe. Mavunde tumeshuhudia mapinduzi makubwa kwenye Sekta ya Madini ambapo Tanzania imepiga hatua kubwa ya kihistoria kwa kufikia mchango wa asilimia 10.1 katika Pato la Taifa kwa Mwaka 2024, ikiwa ni Mwaka mmoja (1) kabla ya lengo la asilimia 10 lililowekwa kwenye Sera ya Madini ya Mwaka 2009 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026),” amesisitiza Dkt. Mabula
Naye Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo amesema kuwa Tume imeanza kukusanya takwimu za bidhaa zinazoingizwa nchini ili kushauri Serikali kuhusu uanzishwaji wa viwanda vinavyotoa bidhaa husika na kuongeza mzunguko wa fedha nchini huku wananchi wakijipatia ajira.
Katika hatua nyingine, Kamishna wa Tume ya Madini ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini, Dkt. Theresia Numbi ameeleza mikakati iliyowekwa na Tume ya Madini ya kuongeza ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini kuwa ni pamoja na mikutano, majukwaa na vyombo vya habari.
DKT. YONAZI AMEONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA TAIFA YA USHAURI YA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022
habariKIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU AIPONGEZA TANGA UWASA KWA MATUMIZI YA MITA ZA MALIPO KABLA
habariNa Oscar Assenga,TANGA
MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa)
imepongezwa kwa kiongozi wa mbio wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 Ismail Ali
Ussi kwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Rais Dkt Samia Suluhu la ufungaji wa
mita za maji za malipo kabla kwa wananchi lengo likiwa kuboresha utoaji wa
huduma
Pongezi hizo zimetolewa leo na Kiongozi wa Mbio mara baada ya
kutembelea na kukagua mradi wa Ufungaji wa Dira za Malipo kabla katika eneo la
Mwakidila kata ya Tangasisi Jijini Tanga baada ya kupokea taarifa ya mradi na kujionea hali ya halisi ya utekelezaji wake.
Alisema kwamba amewapongeza kutokana na kwamba mamlaka hiyo kuwa
wasikivu na kutekeleza agizo la MRais kwa
mradi huo wa kimkakati unaoenda kuondosha changamoto ya muda mrefu
ambayo walikuwa wakiipata wananchi ya malalamiko ya bili za maji.
Alisema kwamba mfumo huo sasa unaenda kuondosha lawama kwa
viongozi kwani wananchi wanaenda kupata maji kulingana na uwezo wao hivyo
kutokana na hilo wamehaidi kwenda kuwa mabalozi waziri kwa kuwasemea juu ya
usimamizi wao mzuri wa mfumo huo kwa sababu unaenda kuwasaidia wananchi hivyo
tunawashukuru na kuwapongeza sana kwa kazi hii nzuri.
Awali akisoma Taarifa ya Utekelezaji wa Mradi huu kwa kiongozi
wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025,Meneja wa Ankara na Makusanyo wa Tanga Uwasa Francis
Barabara alisema kwamba mradi huo ulianza kutekelezwa mwezi Julai mwaka jana na una thamani ya Shilingi za Kitanzania
Bilioni 1.87 na unatekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu kupitia programu ya
IFF-OBA na Mfuko wa Maji wa Taifa.
Francis alisema kwamba utekelezaji wa mradi huo kwa sasa umefikia
asilimia 55.05 kwa ufungaji wa dira 2,202 kati ya dira 4,000.
Aidha alisema utekelezaji wa mradi huu utaongeza Ufanisi wa
ukusanyaji wa mapato na kupunguza madeni ya wateja, udhibiti wa upotevu wa maji,
uimarishaji wa matumizi sahihi ya maji kwa wateja na hivyo kupunguza malalamiko
ya bili za maji.
Akizungumza wakati mara baada ya Mwenge wa Uhuru kukagua na
kutembelea mradi huo,Mwenyekiti wa Bodi
ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo alisema maboresho kupitia mradi wa
hati fungani ambao upo kwenye hatua ya utekelezaji una thamani ya Sh.Bilioni 53.
Alisema kwamba katika mradi huo wamedhamiria kuboresha
miundombiniu kwenye chanzo cha maji bwawa la mabayani ambalo lilijengwa muda mrefu
1978 hivyo kutokufanyiwa ukarabati hivyo wameona walifanyie ukarabati ili
liweze kuendana na uhitaji wa maji kwenye mji wa Tanga,Pangani na Mkinga.
Aliongeza kwamba hivyo wanarekebisha mtambo kwenye bwawa na
katika pampu ambazo zinapeleka maji kwenye mtambo wa kutibu maji sehemu hiyo ikiwemo kurekebisha kuweka
mabomba mapya na kutoka eneo hilo kupelekea mjini kuna bomba kubwa linalazwa .
Mwenyekiti huyo alisema kwamba hatua nyengine ni kusambaza maji kwenye
mji wa Tanga na mabomba yaliyopo ni ya zamani yamechakaa na kama watafanikiwa presha itakuwa kubwa na
mabomba ya zamani yanashindwa kuhimili na watarekebisha ili kuweza kuhimili na
mradi huo mpaka Octaba mwaka huu utakuwa wamemaliza marekebishi na utaanza
kufanya kazi.
Akizungumza mita za Luku, Dkt Fungo alisema kwamba matarajio yao
ni kuhakikisha wananchi wanaunganishwa na nazo kwa wale ambao hawajafikiwa
ambapo alisema kabla ya kufunga mita za luku kulikuwa na malalamiki sana kwa
wateja kuona kama wanabambikiziwa bili kitu ambacho hakiwezekana.
Alisema lakini kwa kuondoa shida hiyo kwa wananchi na Rais alitoa maelekezo kuona njia bora ya kuweza kurekebisha dosari zilizojitokeza na hivyo njia bora wakaona ni mita za luku na walifanya majaribio kwa miaka miwili na sasa wamefikia mita ambazo zinaweza kukudhi mahitaji.
“Tumeanzaa na kuzifungwa kwa wateja wetu na na tulianza na mita 4000 na mpaka sasa tumefikia asilimia 60 wamefunga mita 2200 na tunatarajia kuzimaliza kwa kuwafungia watu wenye uhitaji na wale waliokuwa na madeni na muda mfupi tutakuwa tumezimaliza kwa wenye madeni”Alisema
Awali ya pili mradi wa Mradi wa Hat fungani utakuwa na mita
10,000 kwa hiyo wanataraji kuwafikia wananchi kwa wananchi wengi Tanga kutokana
na mahitaji ni mengi kutokana wenye uhitaji wa kubadilishiwa mita za luku wana
wateja kkaribia 50,000 bado wanaendeleaa kuomba na wanatarajiwa kufikia mpaka
75,000 na ubadilishaji wa mita utakuwa ni urtarbu wa kudumu wataweka za luku.
MWISHO.