Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

REA KUENDELEA KUWEZESHA WAENDELEZAJI WA MIRADI YA NISHATI VIJIJINI

June 17, 2025 Add Comment
-RC Njombe apongeza usimamizi wa miradi ya REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) utaendelea kutoa sapoti kwa waendelezaji wa miradi ya kuzalisha na kusambaza umeme kote nchini ili kuwezesha wananchi wengi kufikiwa na huduma bora ya nishati ambayo inachangia kuinua uchumi wa wananchi pamoja na huduma za kijamii.

TFS YAJIDHATITI KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO MSITUNI

June 17, 2025 Add Comment

 

Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.

Na Fredy Mgunda,Mufindi

Ikiwa ni kuelekea msimu wa kipindi cha kiangazi, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS kupitia Shamba la Miti Sao Hill umeendesha zoezi la usahili kwa watumishi wa muda watakaounda kikosi maalumu kwa  ajili ya kupambana na kudhibiti majanga ya moto katika maeneo yanayolizunguka Shamba.


Zoezi hilo limefanyika leo Juni 16, 2025 katika viwanja vya Shamba la Miti Sao Hill likishirikisha wahifadhi wa Shamba, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na Jeshi la Polisi, likilenga kupata vikosi vitakavyohudumu katika Makao Makuu ya Shamba pamoja na Tarafa ya II ya Shamba Ihefu.


Akizungumza katika zoezi hilo Mhifadhi Mwandamizi anayesimamia Utumishi na Utawala Felista Bayo amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 Shamba linatarajia kuajiri watumishi wa muda 192 kwa ajili ya kukabiliana na kupambana na majanga ya moto kwa kipindi chote cha kiangazi.


Ameongeza kuwa licha ya maombi kuwa mengi kulinganisha na nafasi zilizotajwa, Shamba la Miti Sao aaHill lina shughuli nyingine zinazoendelea katika vituo vyake vyote ikiwa ni pamoja shughuli za bustani na usafi wa mashamba, hivyo wanaokosa nafasi katika vikosi hivyo wanapata fursa ya kuendelea na shuguli nyingine za Shamba.


Kwa upande wake Mhifadhi anayesimamia Kitengo cha Ulinzi wa Msitu dhidi ya moto Murya Sawa amesema kuwa baada ya kukamilisha zoezi hili ni matarajio ya TFS kupitia Shamba la Miti SaoHill kuwa watumshi hawa muda  waliopata nafasi watafanya kazi hiyo kwa weledi kwa kutanguliza uzalendo huku akihimiza ushirikiano baina ya wananchi wote wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi katika kulinda rasilimali za misitu.


Naye Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Wilaya ya Mufindi Ashery Kitundu amesema kuwa lengo mama la jeshi la zimamoto ni kuhakikisha matukio ya moto hayatokei kwa kutoa elimu, na kuyadhibiti pindi yanapotokea hivyo ni watumishi hawa wa muda watakuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao waliyotoka kwa kushirikiana na jeshi la zimamoto katika kutoa elimu ya kuepuka na kukabilina na majanga ya moto.


Usaihili huo unatarijiwa kuendelea hapo kesho katika Tarafa ya Kwanza ya  Shamba Irundi kisha Tarafa ya Tatu Ihalimba, na Tarafa ya Nne Mgololo.

MAADHIMISHO YA MIAKA 25 YA JUMUIYA YA TATHIMINI AFRIKA ( AfrEA ) WAFANYIKA ADDIS ABABA-ETHIOPIA

June 16, 2025 Add Comment


*Na Mwandishi Wetu – Addis Ababa, Ethiopia*


Tanzania imeshiriki Maadhimisho ya Miaka 25 ya Jumuiya ya Tathmini Afrika (AfrEA) yanayofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 16  hadi 18 Juni, 2025, katika Kituo cha Mikutano cha Umoja wa Mataifa (UNECA), jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bi. Sakina Mwinyimkuu.

 Washiriki wengine kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ni Mkurugenzi wa Mipango na Bajeti Bw. Eleuter Kihwele na Mkaguzi Mkuu wa Ndani katika Ofisi hiyo Bw. Exavery Salira.


Maadhimisho hayo ya siku tatu yameandaliwa kwa lengo la kuenzi mchango wa tathmini katika maendeleo barani Afrika, na kuimarisha uwajibikaji wa sera kwa kutumia ushahidi (Evidence Based) katika kufanya maamuzi.

Aidha Washiriki kutoka nchi mbalimbali ndani na nje ya bara la Afrika wanajadili mbinu bunifu na jumuishi za tathmini kwa maendeleo endelevu yenye muktadha wa Kiafrika.




*MWISHO*

WAACHENI WATOTO WAENDE SHULE- RAIS SAMIA

June 16, 2025 Add Comment


Na John Mapepele -OR TAMISEMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi nchini kuwaachia watoto wa kike kusoma shule maalum za msingi na sekondari ambazo zimejengwa na Serikali.

DKT. ADESINA AMALIZA ZIARA YA SIKU NNE NCHINI TANZANIA

June 15, 2025 Add Comment
Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) anayemaliza muda wake, Dkt. Akinwumi Adesina amemaliza ziara yake ya kikazi ya siku 4 aliyoifanya nchini Tanzania kuanzia tarehe 12 hadi 15 Juni 2025.

Dkt. Adesina aliondoka nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kusindikizwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC), Mhe. Denis Londo.

Ziara ya Dkt. Adesina nchini imetokana na mwaliko kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa madhumuni ya kutembelea miradi ambayo benki hiyo imetoa fedha ya kuigharamia.

Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato na barabara ya mzunguko ya Dodoma ambayo kwa pamoja Rais Samia na Dkt. Adesina waliitembelea jijini Dodoma Juni 14, 2025.

Dkt. Adesina ni Rais wa 8 wa AfDB na katika uongozi wake amefanya mageuzi makubwa katika benki hiyo na kuifanya kuwa chombo imara, chenye mtaji wa kutosha na utaalamu wa kuchagiza mageuzi ya kiuchumi barani Afrika hususan katika sekta za miundombinu, kilimo, afya, nishati, mabadiliko ya tabianchi na mifumo ya kifedha.

Kutokana na mchango mkubwa alioutoa barani Afrika, Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam kilimtunikia Shahada ya Heshima ya Falsafa katika Sayansi katika mahafali ya 55, duru ya kwanza yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam Juni 13, 2025.