Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU AIPONGEZA TANGA UWASA KWA MATUMIZI YA MITA ZA MALIPO KABLA

June 17, 2025 Add Comment

 





Na Oscar Assenga,TANGA

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) imepongezwa kwa kiongozi wa mbio wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 Ismail Ali Ussi kwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Rais Dkt Samia Suluhu la ufungaji wa mita za maji za malipo kabla kwa wananchi lengo likiwa kuboresha utoaji wa huduma

Pongezi hizo zimetolewa leo na Kiongozi wa Mbio mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa Ufungaji wa Dira za Malipo kabla katika eneo la Mwakidila kata ya Tangasisi Jijini Tanga  baada ya kupokea taarifa ya mradi na  kujionea hali ya halisi ya utekelezaji wake.

Alisema kwamba amewapongeza kutokana na kwamba mamlaka hiyo kuwa wasikivu na kutekeleza agizo la MRais kwa  mradi huo wa kimkakati unaoenda kuondosha changamoto ya muda mrefu ambayo walikuwa wakiipata wananchi ya malalamiko ya bili za maji.

Alisema kwamba mfumo huo sasa unaenda kuondosha lawama kwa viongozi  kwani wananchi wanaenda kupata maji kulingana na uwezo wao hivyo kutokana na hilo wamehaidi kwenda kuwa mabalozi waziri kwa kuwasemea juu ya usimamizi wao mzuri wa mfumo huo kwa sababu unaenda kuwasaidia wananchi hivyo tunawashukuru na kuwapongeza sana kwa kazi hii nzuri.

Awali akisoma Taarifa ya Utekelezaji wa Mradi huu kwa kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025,Meneja wa Ankara na Makusanyo wa Tanga Uwasa Francis Barabara alisema kwamba mradi huo ulianza kutekelezwa mwezi Julai mwaka jana  na  una thamani ya Shilingi za Kitanzania Bilioni 1.87 na unatekelezwa kwa fedha za Serikali Kuu kupitia programu ya IFF-OBA na Mfuko wa Maji wa Taifa. 


Francis alisema kwamba utekelezaji wa mradi huo kwa sasa umefikia asilimia 55.05 kwa ufungaji wa dira 2,202 kati ya dira 4,000.

Aidha alisema utekelezaji wa mradi huu utaongeza Ufanisi wa ukusanyaji wa mapato na kupunguza madeni ya wateja, udhibiti wa upotevu wa maji, uimarishaji wa matumizi sahihi ya maji kwa wateja na hivyo kupunguza malalamiko ya bili za maji.

 

Akizungumza wakati mara baada ya Mwenge wa Uhuru kukagua na kutembelea mradi huo,Mwenyekiti  wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo alisema maboresho kupitia mradi wa hati fungani ambao upo kwenye hatua ya utekelezaji una thamani ya Sh.Bilioni 53.

 

Alisema kwamba katika mradi huo wamedhamiria kuboresha miundombiniu kwenye chanzo cha maji bwawa la mabayani ambalo lilijengwa muda mrefu 1978 hivyo kutokufanyiwa ukarabati hivyo wameona walifanyie ukarabati ili liweze kuendana na uhitaji wa maji kwenye mji wa Tanga,Pangani na Mkinga.

 

Aliongeza kwamba hivyo wanarekebisha mtambo kwenye bwawa na katika pampu ambazo zinapeleka maji kwenye mtambo wa kutibu maji  sehemu hiyo ikiwemo kurekebisha kuweka mabomba mapya na kutoka eneo hilo kupelekea mjini kuna bomba kubwa linalazwa .

 

Mwenyekiti huyo alisema kwamba hatua nyengine ni kusambaza maji kwenye mji wa Tanga na mabomba yaliyopo ni ya zamani yamechakaa  na kama watafanikiwa presha itakuwa kubwa na mabomba ya zamani yanashindwa kuhimili na watarekebisha ili kuweza kuhimili na mradi huo mpaka Octaba mwaka huu utakuwa wamemaliza marekebishi na utaanza kufanya kazi.

Akizungumza mita za Luku, Dkt Fungo alisema kwamba matarajio yao ni kuhakikisha wananchi wanaunganishwa na nazo kwa wale ambao hawajafikiwa ambapo alisema kabla ya kufunga mita za luku kulikuwa na malalamiki sana kwa wateja kuona kama wanabambikiziwa bili kitu ambacho hakiwezekana.

Alisema lakini kwa kuondoa shida hiyo kwa wananchi na Rais alitoa maelekezo kuona njia bora ya kuweza kurekebisha dosari zilizojitokeza na hivyo njia bora wakaona  ni mita za luku na walifanya majaribio kwa miaka miwili na sasa wamefikia mita ambazo zinaweza kukudhi mahitaji.

“Tumeanzaa na kuzifungwa kwa wateja wetu na na tulianza na mita 4000 na mpaka sasa tumefikia asilimia 60 wamefunga mita 2200  na tunatarajia kuzimaliza kwa kuwafungia watu wenye uhitaji na wale waliokuwa na madeni na muda mfupi tutakuwa  tumezimaliza kwa wenye madeni”Alisema  

Awali ya pili mradi wa Mradi wa Hat fungani utakuwa na mita 10,000 kwa hiyo wanataraji kuwafikia wananchi kwa wananchi wengi Tanga kutokana na mahitaji ni mengi kutokana wenye uhitaji wa kubadilishiwa mita za luku wana wateja kkaribia 50,000 bado wanaendeleaa kuomba na wanatarajiwa kufikia mpaka 75,000 na ubadilishaji wa mita utakuwa ni urtarbu wa kudumu wataweka za luku.

 Kwa hiyo mita za zamani zitapeleekwa kwenye maeneo ambao hawajayafikia lengo kuhakikisha maeneo yote zinawekwa mita za kisasa,lengo kufiia asilimia 95 na maeneo mengine ni 85 na lengo ni kufikia asilia 100

 

MWISHO.

 

 

REA KUENDELEA KUWEZESHA WAENDELEZAJI WA MIRADI YA NISHATI VIJIJINI

June 17, 2025 Add Comment
-RC Njombe apongeza usimamizi wa miradi ya REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) utaendelea kutoa sapoti kwa waendelezaji wa miradi ya kuzalisha na kusambaza umeme kote nchini ili kuwezesha wananchi wengi kufikiwa na huduma bora ya nishati ambayo inachangia kuinua uchumi wa wananchi pamoja na huduma za kijamii.

TFS YAJIDHATITI KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO MSITUNI

June 17, 2025 Add Comment

 

Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.Baadhi ya vijana wakipewa mafunzo ya utimamamu wa mwili kwa ajili ya kulinda na kuzuia mtoto usiharibu miti ya mashamba ya miti Sao Hill.

Na Fredy Mgunda,Mufindi

Ikiwa ni kuelekea msimu wa kipindi cha kiangazi, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS kupitia Shamba la Miti Sao Hill umeendesha zoezi la usahili kwa watumishi wa muda watakaounda kikosi maalumu kwa  ajili ya kupambana na kudhibiti majanga ya moto katika maeneo yanayolizunguka Shamba.


Zoezi hilo limefanyika leo Juni 16, 2025 katika viwanja vya Shamba la Miti Sao Hill likishirikisha wahifadhi wa Shamba, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na Jeshi la Polisi, likilenga kupata vikosi vitakavyohudumu katika Makao Makuu ya Shamba pamoja na Tarafa ya II ya Shamba Ihefu.


Akizungumza katika zoezi hilo Mhifadhi Mwandamizi anayesimamia Utumishi na Utawala Felista Bayo amesema kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 Shamba linatarajia kuajiri watumishi wa muda 192 kwa ajili ya kukabiliana na kupambana na majanga ya moto kwa kipindi chote cha kiangazi.


Ameongeza kuwa licha ya maombi kuwa mengi kulinganisha na nafasi zilizotajwa, Shamba la Miti Sao aaHill lina shughuli nyingine zinazoendelea katika vituo vyake vyote ikiwa ni pamoja shughuli za bustani na usafi wa mashamba, hivyo wanaokosa nafasi katika vikosi hivyo wanapata fursa ya kuendelea na shuguli nyingine za Shamba.


Kwa upande wake Mhifadhi anayesimamia Kitengo cha Ulinzi wa Msitu dhidi ya moto Murya Sawa amesema kuwa baada ya kukamilisha zoezi hili ni matarajio ya TFS kupitia Shamba la Miti SaoHill kuwa watumshi hawa muda  waliopata nafasi watafanya kazi hiyo kwa weledi kwa kutanguliza uzalendo huku akihimiza ushirikiano baina ya wananchi wote wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi katika kulinda rasilimali za misitu.


Naye Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Wilaya ya Mufindi Ashery Kitundu amesema kuwa lengo mama la jeshi la zimamoto ni kuhakikisha matukio ya moto hayatokei kwa kutoa elimu, na kuyadhibiti pindi yanapotokea hivyo ni watumishi hawa wa muda watakuwa mabalozi wazuri katika maeneo yao waliyotoka kwa kushirikiana na jeshi la zimamoto katika kutoa elimu ya kuepuka na kukabilina na majanga ya moto.


Usaihili huo unatarijiwa kuendelea hapo kesho katika Tarafa ya Kwanza ya  Shamba Irundi kisha Tarafa ya Tatu Ihalimba, na Tarafa ya Nne Mgololo.

MAADHIMISHO YA MIAKA 25 YA JUMUIYA YA TATHIMINI AFRIKA ( AfrEA ) WAFANYIKA ADDIS ABABA-ETHIOPIA

June 16, 2025 Add Comment


*Na Mwandishi Wetu – Addis Ababa, Ethiopia*


Tanzania imeshiriki Maadhimisho ya Miaka 25 ya Jumuiya ya Tathmini Afrika (AfrEA) yanayofanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 16  hadi 18 Juni, 2025, katika Kituo cha Mikutano cha Umoja wa Mataifa (UNECA), jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bi. Sakina Mwinyimkuu.

 Washiriki wengine kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ni Mkurugenzi wa Mipango na Bajeti Bw. Eleuter Kihwele na Mkaguzi Mkuu wa Ndani katika Ofisi hiyo Bw. Exavery Salira.


Maadhimisho hayo ya siku tatu yameandaliwa kwa lengo la kuenzi mchango wa tathmini katika maendeleo barani Afrika, na kuimarisha uwajibikaji wa sera kwa kutumia ushahidi (Evidence Based) katika kufanya maamuzi.

Aidha Washiriki kutoka nchi mbalimbali ndani na nje ya bara la Afrika wanajadili mbinu bunifu na jumuishi za tathmini kwa maendeleo endelevu yenye muktadha wa Kiafrika.




*MWISHO*

WAACHENI WATOTO WAENDE SHULE- RAIS SAMIA

June 16, 2025 Add Comment


Na John Mapepele -OR TAMISEMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka wazazi nchini kuwaachia watoto wa kike kusoma shule maalum za msingi na sekondari ambazo zimejengwa na Serikali.