Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts

SERIKALI YAENDELEA NA UJENZI WA VYUO 65 VYA UFUNDI STANDI VETA UTAKAOGHARIMU BILIONI 54

July 12, 2023 Add Comment
Waziri wa Elimu Sayansi na Teklonojia Profesa Adolf Mkenda

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu, Mafunzo ya Ufundi Stadi Veta Anthon Mzee Kasore



Na Mashaka Mhando Tanga

SERIKALI imesema inaendelea na ujenzi wa vyuo 65 vya ufundi stadi Veta utakaohharimu kiasi cha shilingi bilioni 54 katika Mikoa na Wilaya hapa nchini, ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha inatoa elimu ya Amali itakayokidhi matakwa ya mabadiliko ya sera ya elimu. 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teklonojia Profesa Adolf Mkenda alisema hayo jana alipotembelea chuo cha ufundi stadi Veta Jijini Tanga ili kujionea namna kinavyotoa mafunzo ya Ufundi Stadi lakini pia kuhakikisha wanatoa huduma zinazostahiki kwa jamii. 

Waziri Mkenda amesema kuwa kati ya vyuo 65 vinavyojengwa Nchini, Vyuo 64 ni za Wilaya na Chuo Kimoja cha Mkoa ambapo hadi sasa tayari imetoa kiasi cha shilingi bilioni 37 huku matumaini yakiwa makubwa katika kila maeneo yanayojengwa vyuo hivyo ambavyo ni mkakati wa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan. 

"Tukiwa bungeni swali kubwa ambalo limekuwa likiulizwa mara nyingi kuliko maswali mengine yote katika wizara ya elimu sayansi na teknolojia ni kuhusu veta kila mmoja anauliza ni lini veta itajengwa kwake watu wanamatarajio makubwa sana kwenye veta kwa maana hiyo sisi tuna kazi ya kuhakikisha tunakidhi matarajio yao kwa kutoa elimu ya amali ambayo ni bora na ambayo itakidhi matakwa ya vijana, "alisema Waziri Mkenda. 

Prof Mkenda amesema zipo namna mbili za kuendelea kuwapima wahitimu wa Mafunzo ya Ufundi Stadi Veta ambapo moja ya njia ni kuangalia wahitimu wanafanya wapi kazi mara baada ya kuhitimu mafunzo yao na kuwahoji waliowaajiri namna walivyoridhika na utendaji kazi wao. 

Pia Waziri Profesa Mkenda aliwaagiza viongozi wa Veta kuhakikisha wanaandaa bajeti na kuiwasilisha wizarani itakayoomba fedha kwa ajili ya kununulia zana bora zinazokidhi teklonojia ya sasa katika karakana za Ufundi wa magari ili vyuo hivyo vya Veta viweze kuingia sokoni kutengeneza magari ya serikali, mashirika na watu binafsi.

Mkurugenzi wa Veta kanda ya Kaskazini Monica Mbele, alisema wamepokea maagizo hayo ambayo pindi wakipata nyenzo na zana bora za kisasa wataweza kuwa na utayari wa kutengeneza magari lakini pia kuongeza walimu wenye ujuzi wa teklonojia ya kisasa.

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi VETA Antony Mzee Kasore alisema watahakikisha wanakwenda kutekeleza maagizo ya Waziri ya utoaji wa mafunzo bora na kuhakikisha wanatoa mafunzo yanayohitajika na yanayozingatia ubora unahitajika. 

"Kama tulivyosikia kuna vyuo vinavyojengwa 65 katika wilaya mbalimbali na Mkoa na chenyewe pia tunakwenda kusimamia kama maelekezo aliyotoa ya kuhakikisha tunasimamia ujenzi huo uweze kufanyika tukiamini tutakuwa tumekwenda kutekeleza yale yote yaliyoanishwa, "alisema 

Mwisho.

KITUO CHA STERM PARK CHATUMIA WIKI YA SAYANSI AFRIKA KUTOA MAFUNZO YA HISABATI,TEKNOLOJIA N UHANDISI KWA WANAFUNZI 350

June 22, 2023 Add Comment


Meneja wa Kituo cha Sayansi cha Sterm Park Max George akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani

Meneja wa Kituo cha Sayansi cha Sterm Park Max George akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani
Wanafunzi wa shule za Msingi kutoka maeneo mbalimbali Jijini Tanga wakifuatilia kwa umakini mafunzo mbalimbali


Na Oscar Assenga,TANGA

KITUO cha Sayansi cha Sterm Park cha cha Jijini Tanga kimetumia wiki ya Sayansi Afrika kutoa mafunzo ya Hisabati ,Teknolojia na uhandisi kwa wanafunzi 350 wa shule mbalimbali za msingi zilizopo jijini hapa yakilenga  kuongeza ari kwa wanafunzi kupenda kujifunza masomo ya sayansi kwa malengo yao ya baadaye na kuja kulisaidia Taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Sterm Park Max George amesema kuwa tangu kuanzishwa kwa kituo hicho kimeweza kusaidia na kuongeza ari kwa wanafunzi wengi kupenda kujifunza masomo ya sayansi na hisabati hatua ambayo inaleta mabadiliko chanya kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla juu ya kile kinachoelezwa kuwa masomo hayo ni magumu.

Alisema kuwa wanafunzi hao wa shule za msingi ambao wamejitokeza na kupata bahati ya kujifunza technologia, uhandisi pamoja na hisabati ni mwanzo wa Juni 26 hadi 30 mwaka huu ambapo kutakuwa na wanafunzi wa shule za sekondari kutoka mikoa mbalimbali ambao watajifunza teknologia ya juu kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi ambayo imekuwa ikipelekea na adha mbalimbali.

“Tumesherehekea wiki ya sayansi kwa Afrika na watoto 350 kutoka shule mbalimbali za msingi wanaopatikana hapa jijini Tanga wamejifunza juu ya maswala ya hisabati , uhandisi na techolojia kwa vitendo na katika mwendelezo wa kuhakikisha vijana wanedelea kujifunza kwa vitendo zaidi tarehe 26 hadi 30 tutakuwa na vijana wa sekondari kutoka mikoa tofauti toafauti ya Tanzanzia na wao watatengeneza projekti ambayo itakwenda kutatua changamoto ya mabadiliko ya tabianchi.” Alisema Max.

Awali akizungumza Dkt. Isaya Ipiana ambaye ni balozi wa Next Einstein Forum ambao ni waandaaji wa makongamano ya sayansi Afrika kwa wakishirikiana na Sperm Parka katika mkoa wa Tanga amepongeza jitihada mbalimbali zinazofanyika katika sekta ya elimu ikiwemo miundombinu na mabadiliko ya sera ambapo ameiomba serikali kuzidi kuboresha sekta hiyo kwa kuongeza vifaa vya kujifunza na kujifunzi ili iwe rahisi kwa wanafunzi kuelewa zaidi.

Aidha alisema wanaipongeza serikali kwa kuwa imekuwa ikifanya mabadiliko katika sera mbalimbali za elimu lakini imekuwa inaruhusu wadau wanohusika na masuala ya elimu kufanya kazi katika mazingira mazuri hivyo wao kama wadau wataendelea kuhakikisha wanasonga mbele

Kituo hicho cha Sterm Park kwa kushirikiana na halmashauri ya jiji la Tanga june 23 imeandaa tuzo maalum ambazo watatrunukiwa walimu wa kike wanaofanya vizuri katika masomo ya hesabu pamoja na sayansi hii ikilenga hasa kuongeza hamasa kwa walimu kuongeza molari ya kufanya kazi na wanafunzi kupenda na kuwa mabalozi kwa wengine juu ya masomo ya sayansi na hisabati .

TASAC YATUMIA MAONESHO YA BIASHARA,UWEKEZAJI NA FURSA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

March 31, 2023 Add Comment


SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limetoa elimu kwa wananchi kuhusu namna linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Sheria wakati wa maonesho ya Biashara, Uwekezaji na Fursa yaliyokuwa yakifanyika katika viwanja vya Mashujaa kuanzia tarehe 19 hadi 31 Machi, 2023 Mkoani Mtwara.

Akizungumza na vyombo ya habari wakati wa maonesho hayo Kaimu Afisa Mfawidhi wa Mkoa wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania Mkoa wa Mtwara,Joseph Myaka amesema kuwa katika kutekeleza majukumu yao shirika hilo limejikita katika kutoa elimu kwa wananchi kufahamu shirika hilo linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.

Amesema kuwa licha ya majukumu makubwa waliyonayo waliamua kushiriki maonesho hayo ili kuwapa elimu wananchi kuhusu fursa za biashara zilizopo katika Sekta ya Usafiri kwa njia ya Maji sambamba na elimu kuhusu Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa mazingira majini jukumu linalotekelezwa na Shirika hilo.

“TASAC tunashiriki maonesho haya ya Biashara Uwekezaji na Fursa mkoani Mtwara ili kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yanayotekezwa Kisheria. kama mdhibiti wa shughuli za usafiri kwa njia ya maji tunasimamia huduma zinazotolewa na Bandari, tunadhibiti na kusimamia ulinzi, usalama na utunzaji wa mazingira na kuratibu shughuli za uokoaji na utafutaji pale panapotokea dhoruba majini”

“Pia tunatoa elimu kwa wananchi wa Mtwara na wadau wa usafiri kwa njia ya maji katika jukumu letu la Udhibiti wa Safari kwa njia ya Maji na udhibiti Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa Mazingira majini, wanaweza kufanya shughuli zao kwa usalama na kupata maendeleo na kuongeza pato la Taifa.” Ameeleza Joseph.

Kwa mujibu wa Sheria, TASAC ina wajibu wa kusimamia kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhimiza usimizi na shughuli za uwakala wa meli wenye ufanisi, kuhimiza shughuli za bandari na huduma za meli zenye ufanisi, kuhakikisha kunakuwepo usalama na ulinzi wa shehena, kuhimiza na kutunza mazingira, usalama na ulinzi wa bahari, maziwa na mito.

Maonesho hayo ya Biashara, Uwekezaji na Fursa ni maonesho ya Kwanza kufanyika Mkoani Mtwara yakiwa na lengo la kuwaleta pamoja wadau mbalimbali katika Sekta hiyo ili kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kujifunza biashara na uwekezaji wa kisasa pamoja na fursa zilizopo katika sekta hiyo na Mkoa wa Mtwara kwa ujumla.





SHULE YA SEKONDARI COASTAL YA JIJINI TANGA KUANZA KUNUFAIKA NA MKONGE

February 28, 2023 Add Comment

 

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) ,Saad Kambona akizungumza wakati wa maafali ya kidato cha sita shule ya Sekondari Coastal High School ya Jijini Tanga yaliyofanyika kwenye Hotel ya CBA Jijini Tanga

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) ,Saad Kambona akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita katika shule ya Sekondari Coastal High School ya Jijini Tanga kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Coastal High School Andrew Gasper akifuatiwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo,Lulu George



Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) ,Saad Kambona akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita katika shule ya Sekondari Coastal High School ya Jijini Tanga kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Coastal High School Andrew Gasper akifuatiwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo,Lulu George




Na Oscar Assenga,Tanga.

Shule ya Sekondari Coastal ya jijini Tanga,itaanza kunufaika na uwekezaji wa sekta ya mkonge baada ya Bodi ya Mkonge Tanzani (TSB) kuahidi kuiingiza katika majaribio ya klabu za vijana watakaoendelezwa.

Pia shule hiyo imeahidiwa kupewa ekari 100 kwa ajili ya kilimo cha mkonge ikiwa ni sehemu ya kuiongezea kipato .

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mko n ge nchini,Saad Kambona alitoa ahadi hiyo wakati wa mahafali ya kuwaaga wahitimu wa kidato cha sita walioanza mtihani ya kitaifa.

Alisema bodi hiyo imeandaa programu maalumu itakayowawezesha vijana kujiinua kiuchumi kuptia kilimo cha mkonge na bidhaa zitoakanazo na zao hilo.

Alisema kama inavyofahamika Bodi ya Mkonge ni taasisi ambayo kwa muda mrefu ilikuwa ni kama imekufa sasa imeshafungua rasmi ofisi katika jengo lake na kuwezesha kuinua sekta ya mkonge kwa ujumla wake.

“Lakini tunategemea tunapokwenda mbele vijana wengi sana kutoka kwenye shule za Tanga ndiyo wahusike kwenye mpango mzima wa kuleta mapinduzi kwenye zao la mkonge kwani sasa hivi tunapozungumzia mkonge tunazungumzia bidhaa moja tu ya nyuzi za mkonge zitengeneze vikapu, makapeti, magunia, kamba na bidhaa nyingine zitokanazo na zao hilo ,lakini kuna bidhaa nyingti zinahitajika kama sukari,mbolea mvinyo na hata vyakula vya kunenepesha mifugo” alisema Kambona

Mkuu wa shule hiyo,Joseph Gaspar alisema ilianza rasmi mwaka 2000 na kwamba kwa miaka mitatu mfululizo imekuwa ikitoa ufaulu wa daraja la kwanza A na pili kwa wanafunzi wote wa kidato cha sita wote katik a mitihani ya kitaifa ya mchepuo wa sayansi.

“Hadi sasa shule hii imetimiza miaka 22 lakini kwa kipindi cha miaka miatatu mfululizo i mekuwa ikitoa wanafunzi wenye ufaulu wa daraja la kwanza na la pili katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha sita...tunatarajia mitihani hii ufaulu utakuwa wajuu zaidi”alisema Gasper.

Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo,Lulu George alisema kuwa miongoni mwa mambo yanayotiliwa mkazo ni masomo ya sayansi wakiamini kuwa jukumu lao ni kupata wataalamu watakaoiendeleza nchi katika sekta ya uhandisi,udaktari na utafiti mbalimbali ikiwamo sekta ya kilimo na ufugaji.

DC TANGA ALISHUKURU SHIRIKA LA BRAC MAENDELEO TANZANIA KWA KUWAKOMBOA WASICHANA KIELIMU

December 07, 2022 Add Comment




Mkuu wa Wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati akifungua wa kikao cha wadau cha kujadili na kutathimini mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa miaka minne uliokuwa unaotoa elimu, uwezeshaji na stadi za maisha ( Education Empowerment and Life Skills for Adolescent and Young Children -EELAY) Mkoa wa Tanga tangu Juni 2018 hadi Desemba 2022. kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo 
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo wakati akifungua wa kikao cha wadau cha kujadili na kutathimini mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa miaka minne uliokuwa unaotoa elimu, uwezeshaji na stadi za maisha ( Education Empowerment and Life Skills for Adolescent and Young Children -EELAY) Mkoa wa Tanga tangu Juni 2018 hadi Desemba 2022
Meneja awa Mradi huo kutoka Shirika la Brac Maendeleo Tanzania Hope Jassson akizungumza wakati wa kikao hicho
Meneja awa Mradi huo kutoka Shirika la Brac Maendeleo Tanzania Hope Jassson akizungumza wakati wa kikao hicho
Afisa Elimu Msingi Jiji la Tanga Kassim Kaonekana akizungumza
Mmoja wa wanafunzi walionufaika na mradi 
Maafisa wa Shirika la Brac Maendeleo Tanzania mkoani Tanga wakiwemo na wadau wengine
Wadau wakiwa kwenye kikao hicho
Sehemu ya wadau wa kikao hoicho
Waheshimiwa madiwani wakiwa kwenye kikao hicho


Na Oscar Assenga,TANGA.


Mkuu wa Wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa amelishukuru Shirika la BRAC Maendeleo Tanzania kwa kuwakomboa Mabinti na Wasichana ambao hawakupata elimu kupitia mfumo maalumu,

Mgandilwa aliyasema hayo wakati wa kikao cha wadau cha kujadili na kutathimini mafanikio ya utekelezaji wa mradi wa miaka minne uliokuwa unaotoa elimu, uwezeshaji na stadi za maisha ( Education Empowerment and Life Skills for Adolescent and Young Children -EELAY) Mkoa wa Tanga tangu Juni 2018 hadi Desemba 2022.

Mradi huo ulikuwa na vipengele viwili muhimu,kipengele cha kwanza kinalenga wasichana walioko kwenye rika balehe wenye umri kati ya miaka 15-24 kwa kutoa elimu ya Sekondari ,mafunzo ya stadi za maisha na fursa za ajira kwa wasichana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu kwa kutumia programu ya muda mfupi yenye matokeo chanya kusaidia wasichana katika kukamilisha miaka minne ya elimu ya Sekondari ndani ya miaka miwili.

Alisema kwamba wanashukuru sana kwa mradi huo ambao unawaachia urithi mkubwa wa elimu kwa Watoto hivyo wap kama Serikali wanawaomba wakakae chini watathmini upya kisha warudi tena katika Mkoa huo na Halmashauri ya Jiji la Tanga kuendelea.

Alisema miradi yote ambayo inaachwa na mradi huo itaendelezwa na kwamba hakuna mradi hata mmoja ambao utatelekezwa huku akiwakikishia kuwa miradi yote itaendelezwa kwa gharama yoyote ile na Serikali itasimamia kuhakikisha watoto wanaendelea kupata elimu.

Awali akizungumza Meneja awa Mradi huo kutoka Shirika la Brac Maendeleo Tanzania Hope Jassson alisema kwamba hadi sasa zaidi ya Wasichana 900 ambao hawakufanikiwa kupata Elimu katika mfumo maalumu wa Elimu ya upili ( Sekondari) wamefanikiwa kupata Elimu hiyo kupitia Mradi wa Elimu na Stadi za Maisha unaotekelezwa  katika Mkoa wa Tanga.

Hope alisema Shirika hilo Chini ya Ufadhili wa Shirika la Norad la Nchini wamefanikiwa kuwapatia Elimu ya Sekondari Mabinti hao zaidi ya 900 chini ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,

" Asilimia 86.8 ya Wasichana walioko kwenye Rika Balehe wamefaulu na kupewa Cheti Cha Elimu ya Sekondari kuanzia Mwaka 2017 Hadi 2021, Vituo 30 vya Masomo vinaendelea ya Elimu chini ya usimamizi wa Jamii ambapo Kati ya hivyo Vituo 20 vipo katika Halmashauri ya Jiji la Tanga na 10 vipo Wilaya ya Korogwe " Alisisitiza Hope

Alisema Wasichana zaidi ya 1161 walipatiwa Mafunzo ya kuanzisha Biashara ndogo pamoja na Mitaji kupitia SIDO,VETA na Ustawi wa Jamii,

"Zaidi ya asilimia 65 ya Wasichana hususani katika Halmashauri ya Jiji la Tanga Wanajishughulisha na shughuli za kujiongezea kipato na kubadili mfumo wao wa Maisha ya awali kabla ya kupata Elimu " Alisisitiza Hope

Aliongeza kuwa Wasichana 10 wa wamefanikiwa kujiunga na Chuo kikuu kwa kozi za Shahada ya Kwanza huku Wasichana 22 Walioko kwenye Rika Balehe Wamehitimu ngazi ya Cheti kutoka Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Kampasi ya Tanga Wakati,


"Wasichana wengine 3 waliandikishwa katika Vyuo mbalimbali vikiwamo chuo Cha maji,chuo Cha Taifa Cha Zanzibar na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha, Watoto 1670 wa miaka 3-5 walipata Elimu ya Makuzi ,Malezi na Maendeleo ya awali, nafasi za kazi zaidi ya 450, Ujenzi wa Madara mapya 22 na Ukarabati wa madarasa 13 pamoja na Walimu 41 wa Elimu ya Awali kutoka Shule za Serikali walipatiwa Mafunzo juu ya Mtaala wa Elimu ya Awali pamoja na kutoa Vifaa vya kufundishia" Alisisitiza Hope