JIHADHARINI NA MATUMIZI YA ANTIBIOTIKI KIHOLELA

October 07, 2015

  13
Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohammed Bakari akifafanua jambo.
zote na Magreth Kinabo-maelezo.
12
Mwenyekiti wa Antibiotic Resistance Partnership (GARP), Profesa Said Aboud kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi za Tiba Shirikishi (MUHAS) kushoto akitoa ripoti ripoti ya dunia kuhusu matumizi na usugu wa dawa za Antibiotiki ya mwaka 2015,uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.Katikati ni Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohammed Bakarina kulia ni Mfamasia Mkuu wa Serikali Henry Irunde.
14
Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohammed Bakari(kushoto wa pili) akizindua ripoti ya dunia kuhusu matumizi na usugu wa dawa za Antibiotiki ya mwaka 2015,uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Kushoto ni Mwenyekiti wa Antibiotic Resistance Partnership (GARP), Profesa Said Aboud kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi za Tiba Shirikishi (MUHAS)na kulia wa pili ni Makumu Mwenyekiti wa wa Antibiotic Resistance Partnership (GARP), Profesa  Robinson Mdegela kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine na kulia wa pili ni Mfamasia Mkuu wa Serikali Henry Irunde.
15
Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohammed Bakari akionesha ripoti hiyo.
10
picha ya pamoja kati ya Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohammed Bakari na wadau wa uzinduzi huo.
……………………………………………………………….
Na Magreth Kinabo – Maelezo Dar es Salaam
 
 Juhudi zaidi zinahitajika  na utashi wa kisiasa katika  kudhibiti usugu wa dawa za antibiotiki ili isije ikafikia mahali ambapo  dawa hizo zikakosekana katika kutibu magonjwa ya kuambukiza, pia wito umetolewa kwa jamii  kuwa na matumizi sahihi ya dawa za antibiotiki ili kuweza kupunguza usugu wa dawa hizo.
Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa Antibiotic Resistance  Partnership (GARP), Profesa Said Aboud kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi za Tiba Shirikishi( MUHAS) wakati wa uzinduzi wa ripoti ya dunia kuhusu matumizi na usugu wa dawa za Antibiotikiya mwaka 2015,uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ambapo alisema ripoti hiyo imetoa mapendekezo hayo.
Aidha tatizo la usugu wa dawa hizo linachangiwa na kutokuwepo kwa usimamizi madhubuti katika kununua dawa kutoka katika maduka ya dawa bila cheti cha daktari.
 Akizungumzia kuhusu suala hilo, Profesa Aboud alisema  Watafiti wa Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Magonjwa, Uchumi, na Sera(Center for Disease Dynamics,Economics & Policy(CDDEP) )wakishirikiana na nchi washiriki ikiwemo Tanzania walitoa ripoti mpya inayoonesha kiwango kikubwa cha usugu wa dawa hizo zinazotumika kutibu magonjwanya kuambukiza ambayo yanapelekea kuhatarisha maisha ya watu dunia.
Alisema ripotoi hiyo ilizinduliwa Septemba 17,mwaka 2015 mjini Washington,Marekani inaonyesha usugu na matumizi yasiyosahihi ya dawa za antibiotiki na mipango ya kitaifa inayotumika katika kupambana na tatizo hilo.
“The State of the World’s Antibiotics 2015 ni ripoti ya kwanza kuonyesha kwa kina ukubwa wa tatizo la usugu wa dawa za antibiotiki kidunia kwa binadamu, wanyama na mazingira. Ripoti hiyo imetoa mikakati mipya ambayo kila nchi ikiwemo Tanzania ionapendekezwa kuifanyia kazi ya kupambana na tatizo hilo linaloenea kwa kwa kasi.
“Ripoti hiyo inaonyesha kuwa matumizi sahihi ya dawa za antibiotiki kutibu magonjwa ya kuambukiza ni mojawapo  ya njia muhimu kupambana na usugu wa dawa za antibiotiki na hili  likiwezekana litaondosha dhana kuwea suluhisho la usugu wa dawa za antibiotiki ni kukosekana kwa dawa mpya za antibiotiki za kutibu magonjwa ya kuambukiza ,” alisema Profesa Aboud.
Aliongeza  kwamba nchi tajiri duniani zinatumia dawa za antibiotiki kwa kiasi kikubwa ,tatizo la usugu wa dawa za antibiotiki kwa nchi masikini na zenye uchumi wa kati ni kubwa duniani linahitaji juhudi za makusudi kupambana nalo.
Profesa Aboud alisema tafiti zilizofanyika Tanzania zinaoyesha kuwa kuna kiwango kikubwa cha usugu kwa dawa za antibiotiki kwa bakteria aina ya Streptococcus pneumonia anayesababisha homa ya mapafu kwa watoto. Magonjwa ya kifua pamoja na homa ya mapafu yanasababisha kwa asilimia 15 ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano katika mwaka 2013 na Watanzania 35,000 walikufa kwa homa ya mapafu mwaka 2012 kutokana na bacteria sugu aina ya Streptococcus pneumonia.
 Alifafanua kwamba usugu wa dawa hizo umeonekana katika vinyememea vya maradhi vya bacteria katika uambukizo wa njia ya mkojo,kisonono na kaswende katika miaka 15 iliyopita.
“ Kama hali ya usugu wa dawa za antibiotiki itaachwa kuendelea ,magonjwa Ya kisonono na kaswende hayatatibika na kusababisha ugumba na upofu wa watoto wa change wanaozaliwa,” alisisitiza.
 Alisema kwa mara ya kwanza ripoti hiyo inaonyesha taarifa kutoka nchi masikini kama Tanzania na zenye uchumi wa kati ambapo tatizo la usugu wa dawa za antibiotiki ni kubwa lakini haionyeshi juhudi za makusudi zikichukuliwa kupambana na tatizo hilo.
Ripoti hiyo imetumia uzoefu uliopatikana kutoka nchi nane katika Afrika ikiwemo Tanzania na Asia kupitia mradi wake wa kimataifa wa kupambana na usgu wa dawa za antibiotiki(Global  Antibiotiki Resistance  Partnership(GARP).
 Alizitaja njia nyingine ambazo zimetolewa kama mapendekezo yanayowezakutumika kupambana na tatizo hilo kuwa ni kuwa na kampeni ya matumizi sahihi ya dawa hizo kutibu magonjwa ya kuambukiza, kudhibiti magonjwa ya kuambukiza katika hospitali, kutoa  chanjo kukinga magonjwa ya kuambukiza na kupunguza matumizi ya antibiotiki yasiyo ya lazima ya lazima kutibu magonjwa ya kuambukiza, ikiwemo na utoaji wa elimu kwa umma.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohammed Bakari alisema Serikali imeyapokea mapendekezo ya ripoti hiyo, hivyo wizara yake itatoa miongozo juu ya suala hilo baada ya kujadiliana na wataalamu mbalimbali.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »