MRADI WA KUZALISHA UMEME WA JUA KISHAPU WAFIKIA ASILIMIA 63.3 - MD TWANGE

June 08, 2025 Add Comment


📌Asema awamu ya kwanza utazalisha Megawati 50 na kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa

Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Bw. Lazaro Twange amesema Mradi wa uzalishaji umeme unaotokana na jua wa Kishapu Mkoani Shinyanga umefikia asilimia 63.3 kukamilika ambapo amesema awamu ya kwanza ya Mradi huo utazalisha Megawati 50 ambazo zitaingizwa kwenye gridi ya Taifa ifikapo mwishoni mwa mwezi wa kumi mwaka huu.

MD Twange ameyasema hayo leo Juni 8 mwaka 2025 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya mradi huo ambao unagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 118 kwa awamu ya kwanza huku awamu ya pili ikitarajia kutumia kiasi cha shilingi Bilioni 204.

‘’Kwanza tunamshukuru Mhe. Rais kwa kutupatia fedha kwa awamu zote, kama mnavyoona kazi inaendelea na Mradi unatarajia kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa mwishoni mwa mwezi wa kumi kwa ajili ya kuwasambazia umeme wananchi, lakini pia tuko katika hatua  za mwisho za manunuzi kwa ajili ya kumpata mkandarasi atakayetekeleza Mradi kwa  awamu ya pili ambayo itazalisha megati 100’’ alisisitiza Mkurugenzi Mtendaji Twange.

Aidha, amewahakikishia wananchi kuwa TANESCO inafanya jitihada za makusudi za kuhakikisha Mradi unakamilika kwa wakati  ili kuendana na ongezeko la mahitaji ya watu na shughuli za uwekezaji ambazo zinategemea nishati ya umeme kujiendesha.



Naye Meneja wa Mradi huo Mhandisi Emmanuel Andarson amesema awali Mradi huo ulipaswa kukamilika mwezi  February mwaka huu lakini Mkandarasi aliongezewa muda baada kukabiliwa na baadhi ya changamoto ambapo ameahidi kukamilisha Mradi huo kwa mujibu wa makubaliano ya mkataba .

Mradi wa uzalishaji wa umeme unaotokana na nguvu ya jua wa Kishapu uliopo katika Kijiji cha Ngunga Mkoani Shinyanga ulianza utekelezaji wake Desemba 8  mwaka 2023 na unatarajia kukamilika rasmi Oktoba 29 2025 ambapo unagharimu jumla ya shilingi bililioni 323 kwa awamu zote mbili ukitarajia kuzalisha megawati 150 za umeme.m



MAANDALIZI YA MAC D BONANZA YAKAMILIKA ,WASHIRIKI WAVUKA LENGO

June 08, 2025 Add Comment


Maandalizi ya Mac D Bonanza 2025 & Fun Run (Mbio za kujifurahisha) yamekamilika kwa asilimia kubwa huku washiriki wa mbio za kujifurahisha wakivuka lengo la wakimbiaji lililowekwa jambo linaonyesha kuwapo na mwamko kubwa wa watu kushiriki tamasha hilo litakalofanyika Juni 7, 2025.


Akiongea leo Jijini Dar es Salaam kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa Eb Twenty Five, Mratibu wa Mac D Bonanza Denzel Rweyunga amesema wamefurahishwa na namna jamii ilivyohamasika katika kushiriki Bonanza hilo kwa mwaka huu.


“Sisi waandaaji tulijiwekea lengo la kupata washiriki wa mbio za kujifurahisha 700 tu, lakini kutokana na mwamko mkubwa wa jamii na hamasa iliyokuwapo mitaani hadi kufikia leo tuna idadi ya washiriki zaidi ya 1,800,” alisema Denzel.

Amesema kwamba kwa sasa zoezi la kutoa fulana bure na namba za washiriki waliojisajili kwa ajili ya kukimbia mbio za Kilomita 10 na Kilomita 5 nalo linaenda vizuri ambapo washiriki wengi wameshachukua fulana zao katika vituo mbalimbali tayari kwa maandalizi mbio.


Ameeleza kuwa mgeni rasmi wa Mac D Bonanza 2025, ambalo litafanyika katika viwanja vya Chuo Cha Taifa cha Ulinzi (NDC) Kunduchi, likishirikisha mbio za kujifurahisha, burudani na baadae jioni mchezo wa soka kati  ya Mac D FC na IPP Media, atakuwa Mhe. Hamis Mwinjuma, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi Calvin Obeld amesema amesema kwamba mbio zitaanza 12:00 asubuhi kwa mbio za Kilomita 10 na kufuatiwa na mbio za Kilomita 5, ambapo  zitaanzia katika viwanja vya Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) kilichopo Kunduchi na kuhitimishwa katika viwanja hivyo hivyo.


Mac D Bonanza 2025 inadhaminiwa na Bodi ya Utalii Tanzania ( TTB ), Isumba Trans Limited ( ITL ), Kilimanjaro Water, Namis Corporate Limited, JC Hall, Zakys Bay, Pwani Inland Clearance Deport Ltd PICD) na EB Twenty Five na ITV & Radio One.

DKT.BITEKO AELEZA MAPINDUZI YALIYOFANYWA NA SERIKALI SEKTA YA ELIMU

June 08, 2025 Add Comment


📌 Ataka CWT wasigawanyike, ahimiza amani, upendo na mshikamano*


📌 Serikali kuendelea kuajiri walimu kila mwaka


📌 Serikali ya Awamu ya Sita yajenga madarasa 62,685 ya shule za msingi na sekondari, shule mpya za msingi na sekondari 2,611 na nyumba za walimu 1,792


📌 Serikali kufanyia tathmini ombi la kuwa na chombo kimoja cha kusimamia walimu nchini


📌 CWT yaipongeza Serikali kwa kuendelea kulipa stahiki za walimu


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Serikali imeendelea kutambua mchango wa walimu katika maendeleo ya sekta ya elimu kwani ni wazalishaji wa watalaamu mbalimbali waliopo katika sekta zote ikiwemo afya, nishati, sayansi na teknolojia. Sambamba na kufanya maboresho yatakayowaongezea walimu ari ya kufanya kazi kwa bidii, weledi, uadilifu na kutanguliza mbele maslahi ya Taifa.


Mafanikio yaliyopatikana katika sekta hiyo yanachangiwa moja kwa moja na walimu. Hivyo, Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kina mchango mkubwa kwa jamii na kwa Taifa kwa ujumla kwa kuwa pamoja na jukumu la kufundisha na kujengea watu maarifa, mwalimu ni mzazi wa kiroho, kiongozi wa fikra, na ni mjenzi wa maadili katika jamii.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko Juni 8, 2025 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Saba wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT).


Amesema katika kuimarisha sekta ya elimu ili kuongeza ufanisi na kusogeza huduma kwa jamii. Serikali imefanikiwa kujenga jumla ya madarasa 62,685 kwa shule za msingi na sekondari, shule mapya za sekondari 1,031, shule mpya za msingi 1,580 na nyumba za walimu 1,792.



Ameongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2020/21 hadi 2024/25, Serikali imefanikiwa kuwalipa malimbikizo ya mishahara walimu 101,596, kulipa watumishi 156,556 madeni yasiyo ya mishahara na kuongeza mshahara kwa watumishi wa umma ambapo kima cha chini kuanzia mwezi Julai, 2025 kitakuwa shilini 500,000 badala ya 370,000.


“Serikali inaendelea kutoa ajira za walimu ambapo kuanzia mwaka 2021 hadi sasa, jumla ya walimu 40,527 wameajiriwa katika maeneo mbalimbali nchini. Lengo la kufanya hivi ni kutatua changamoto mbalimbali zilizopo,” amesema Dkt. Biteko.


Amepongeza matokeo ya zoezi la ‘Samia Teachers Mobile Clinic’  kwa kuwafikia walimu 48,380 pamoja na kutatua kero zao huku akiwaomba kuongeza ubunifu utakaowawezesha kuwa na mikakati mingine yenye lengo la kuimarisha utendaji katika sekta ya elimu na kushirikiana na Serikali kwa kutekeleza miradi ya Elimu ya TEHAMA kwa walimu na miradi mingine isambae  kwenye mikoa yote nchini.

Kuhusu ombi la walimu kuwa na mwajiri mmoja anayeshughulikia masuala yote ya walimu ili kuimarisha ufanisi katika kuwasimamia. Dkt. Biteko amesema Serikali imelipokea ombi hilo na italifanyia tathmini ili kubaini endapo utaratibu uliopo sasa una changamoto zinazolazimu kutatuliwa kwa kuanzisha chombo kitakachosimamia walimu wote nchini.


Amezungumzia utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa na kusema kuwa lengo lake ni kukuza elimu inayotolewa nchini na kuwafanya wanafunzi waweze kujitegemea wanapomaliza masomo yao. Aidha, Serikali inaendelea kuchukua hatua stahiki kuhakikisha kuwa walimu wote wanapata mafunzo ili waweze kuendana na mabadiliko hayo. 


Fauka ya hayo, kufuatia kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa CWT, amewasihi wajumbe wa Mkutano huo kutumia haki yao katika kuchagua viongozi watakaowaongoza vyema na kuwataletea maendeleo pamoja  wagombea kuomba kura kwa heshimiana.

  


“ Nawasihi kuendelea kusimamia misingi ya haki, usawa na uwazi hususan wakati wa majadiliano na utatuzi wa masuala yote yanayohusu chama chenu. Niwaombe watakaoshinda msiwanange watakaoshindwa na mtakaokosa nafasi msikasirike, asitokee mtu wa kuwagawanya, msigawanyike hii ni taalamu ya pili ya uumbaji, mshikamane, mpendane na mshirikiane,” amesisitiza Dkt. Biteko.


Naye, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwan Kikwete amesema kuwa Serikali inathamini mchango wa walimu katika mipango mbalimbali ya Taifa na kuahidi kuendeleza ushirikiano mzuri kwa ajili ya ujenzi wa Taifa na uchumi imara.

Kupitia mkutano huo, Rais wa Chama Cha Walimu Tanzania, Leah Ulaya amempongeza Rais Samia kwa utendaji kazi wake na kuahidi kuwa CWT itaendelea kushirikiana na Serikali .


Naye, Kaimu Katibu Mkuu wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT), Joseph Misalaba ameishukuru Serikali kwa kuendelea kulipa stahiki mbalimbali za walimu ambapo walimu wamenufaika kwa kupandishwa vyeo, ulipwaji wa malimbikizo ya mishahara na madeni yasiyo ya mishahara.


“ Kwa niaba ya watumishi wa Tanzania hususan walimu wote tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kusikiliza kilio cha wafanyakazi juu ya suala la kikokotoo cha mafao ya kustaafu na kuridhia kuboresha kikokotoo kutoka asilimia 33 hadi asilimia 40. Chama cha Walimu Tanzania kinaiomba Serikali yako iendelee kufanya maboresho zaidi ili kuleta ustawi wa walimu wetu wastaafu ambao wameitumikia nchi yao kwa uaminifu mkubwa,” amesema Misalaba.

Amefafanua kuwa CWT ni chama cha wafanyakazi ambacho msingi wake mkubwa ni kutetea haki na maslahi ya wanachama wake. Kama mdau wa elimu CWT itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali wa elimu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya elimu nchini.


Aidha, Mkutano huo wa mwaka wa CWT umehudhuriwa pia na wawakilishi wa vyama vya walimu kutoka nchi za Rwanda, Burundi, Afrika Kusini na Namibia. 


Mwisho

TFS yawakaribisha wawekezaji katika vivutio vya utalii wa misitu — yaweka bayana fursa mpya za kipekee

June 07, 2025 Add Comment

 


Na Mwandishi Wetu, Arusha

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeeleza mikakati na fursa mbalimbali za uwekezaji na utalii wa misitu, huku ukizindua aina mpya ya vivutio ikiwemo usafiri wa waya (zipline) katika Ziwa Duluti, ikiwa ni sehemu ya kuongeza mazao na shughuli za utalii katika kampeni ya kuvutia watalii na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Akizungumza katika Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Karibu Kilifair 2025 yanayoendelea jijini Arusha Juni 6,2025, Yusuph Tango - Mhifadhi TFS, alisema lengo la kushiriki maonesho hayo ni kuwafikia wadau muhimu na kuwaeleza fursa zilizopo katika sekta ya utalii wa misitu nchini.

 "Tuko hapa kuwaeleza wadau wetu kuhusu mazao ya utalii tuliyonayo. Tuna maeneo mengi ya misitu nchini yenye vivutio vya kipekee vinavyofaa kwa utalii wa kimazingira na pia tuna fursa nyingi za uwekezaji wa huduma kama vile malazi, burudani (recreations) ndani ya misitu,” alisema Tango.

Aliendelea kusema, TFS kwa kushirikiana na wadau imeanzisha mazao ya kipekee ikiwemo usafiri wa waya (zipline) katika Ziwa Duluti, Arusha, ambacho kitakuwa cha kwanza nchini kupita juu ya maji, jambo linalotoa fursa ya kumbukumbu za kipekee kwa watalii.

    “Utalii huu ni sehemu ya jitihada za TFS kubuni njia mpya za kutumia fursa ya huduma
zitokanazo na misitu kama chanzo cha mapato ya taifa na ajira,” aliongeza.

Kwa mujibu wa Tango, TFS imeweka mkazo katika kukuza utalii wa misitu kwa kushirikiana na sekta binafsi kuwekeza katika maeneo yenye vivutio vya asili, huku akibainisha kuwa baadhi ya misitu tayari imeanza kunufaika na uwekezaji huo.



Akitolea mfano wa matukio yanayotarajiwa mwezi huu wa Juni, Tango alieleza kuwa TFS inaandaa matukio mawili makubwa ya utalii wa mazingira — Rubare Marathon itakayofanyika ndani ya Shamba la Miti Rubare, Bukoba, na West Kili Forest Challenge itakayofanyika katika Shamba la Miti West Kilimanjaro, jirani na geti la Londorosi linaloelekea Mlima Kilimanjaro.

    “Katika matukio haya kutakuwa na shughuli kama mbio za msituni, kuendesha baiskeli, mbio za pikipiki, pamoja na kutembelea maporomoko ya maji na vivutio vya kipekee ndani ya misitu,” alisema.

Mbali na hayo, TFS pia imetangaza kuongeza msukumo katika kukuza utalii wa nyuki (api-tourism), ambao umeanza kuonyeshwa kama zao jipya la kiutalii nchini. Kwa sasa, shughuli hiyo inatekelezwa katika maeneo ya Mlima Hanang, Vikindu (Mkuranga), na maeneo mengine yanayoratibiwa kuingizwa kwenye mpango huo.

    “Mhe. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati walionesha kuvutiwa sana na api-tourism. Walituhimiza tuiendeleze maeneo mengine ili itoe tija kwa taifa na jamii zinazozunguka misitu hiyo,” alieleza Tango.

Alisisitiza kuwa TFS imejipanga kushiriki kikamilifu katika kufanikisha azma ya serikali ya kuongeza idadi ya watalii nchini, kwa mujibu wa malengo ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala.

    “Malengo ya serikali ni kuongeza watalii. Sisi TFS tumepewa jukumu la kuchangia hilo kupitia vivutio vya misitu na huduma bunifu za utalii. Kwa hiyo, tuko tayari kushirikiana na wadau wote kuifikia Tanzania ya utalii endelevu,” alihitimisha.

Maonesho ya Karibu Kilifair 2025 yanayofanyika jijini Arusha, yamekusanya wadau wa sekta ya utalii kutoka mataifa mbalimbali, ambapo TFS ni miongoni mwa taasisi za serikali zinazotumia jukwaa hilo kuhamasisha uwekezaji na kukuza utalii wa ndani.

--

Tulizo Henry Kilaga I A Brand Communication Strategist,

Located: Dodoma I Dar es Salaam - Tanzania. 

Call/WhatsApp: +255 765 888887

www.thestrategist.co.tz


TAASISi 762 ZATUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA NCHINI-DKT.MPANGO

June 07, 2025 Add Comment


📌 Taasisi chini ya Wizara ya Nishati zqpewa tuzo kutambua mchango wao katika Gesi, Umeme na Nishati Jadidifu


Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Philip Isdor  Mpango ameeleza kuwa jumla ya taasisi 762 nchini zinatumia nishati safi ya kupikia ikiwa ni jitihada za kuepuka athari za kimazingira, kiafya, kijamii na kiuchumi.


Amesema hayo tarehe 5 Juni 2025 katika kilele cha Siku ya Mazingira Duniani ambayo  kitaifa imeadhimishwa jijini Dodoma katika kituo cha  Mikutano cha Jakaya Kikwete.


 "Taasisi nyingi za Serikali na Binafsi zimeanza kutekeleza katazo la matumizi ya nishati isiyo safi na  kuanza kutumia nishati safi ya kupikia ambapo  hadi Machi 2025 jumla ya Taasisi 762 zilikuwa zimeanza kutumia nishati safi ya kupikia." Amesema Dkt. Mpango


Ameongeza kuwa,  kati ya taaisis hizo, taaisisi za Umma ni 495 na taasisi binafsi ni 267.i 


 Makamu wa Rais amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa kinara wa kuendeleza na kusukuma matumizi ya nishati safi ya kupikia Tanzania, Afrika na Duniani kwa ujumla.

Sambamba na hilo Dkt. Mpango amezipongeza taasisi zote zilizotekeleza katazo hilo la kutotumia nishati isiyo safi  na kutoa rai kwa taasisi ambazo hazijatekeleza agizo hilo ziendelee kuwekeza katika matumizi ya nishati safi ya kupikia. 


Katika hafla hiyo ya Siku ya Mazingira dunian,   Dkt. Mpango ametoa Tuzo kwa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati ikiwa upande wa REA tuzo imepokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Bw. Renatus Msangira tuzo ya kutambua mchango wa REA katika kutunza mazingira  kupitia utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia.

Miradi hiyo ambayo ni utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ni pamoja na usambazaji wa mitungi ya gesi pamoja na majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa nishati safi ya kupikia vijijini .


Aidha, TANESCO tuzo hiyo imepokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Bw. Lazaro Twange,ikiwa ni kutambua mchango wa TANESCO katika kuhifadhi mazingira kupitia utekelezaji wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ambao umeendelea kuzingatia misingi ya utunzaji wa mazingira sambamba na kuchangia kupunguza gesi joto.

Huku, CPA Mussa M. Makame - Mkurugenzi Mtendaji TPDC, amepokea TUZO  ya kutambua mchango wa TPDC katika kuhifadhi  na kutunza mazingiza kupitia matumizi ya gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG).