Na Oscar Assenga, Tanga.
KADA wa Chama Cha ACT –Wazalendo Mkoani Tanga John
Charles Mboggo amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania Ubunge katika Jimbo
la Tanga kupitia chama hicho huku akihaidi kuirejesha Tanga ya Viwanda ambayo ni
ndoto kubwa ya wananchi wa mkoa huo.
Akizungumza leo na waandishi wa habari mara baada ya
kuchukua fomu hiyo alisema lenbgo la kuchukua fomu ya kuwania Ubunge ni kutaka
kuhakikisha anatoa mchango wake katika kurejesha viwanda vya Tanga ambavyo
wananchi wamekuwa na kiu navyo.
Alisema kwamba kwa sababu viwanda ni ajira na nguvu kazi ya Tanga wanaongelea kuna
vijana asilimia 68 ya vijana wakitumika kwenye viwanda watakuwa na uchumi
kwenye Jimbo hilo na Mkoa kwa Ujumla.
“Tanga tunaamini sisi ni watu tunaamini watu wa kuleta
maendeleo na ndio maana tunawahamasisha wananchi wenye sifa za kupiga kura
kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye zoezi la kura kwa lengo la kuwachaguoa viongozi
watakaowaongoza”Alisema
Awali akizungumza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Jimbo la
Tanga Anasi Mohamed Rweymamu alisema
kwamba wanaendelea kuwakaribisha wagombe na kura zao wa maoni ndani ya chama
ndizo zitakazoamua nani anaweza kupeperusha tiketi ya chama hicho kwenye nafasi
ya Ubunge.
Alisema kwamba ACT Wazalendo ndio chama pekee ambacho
kinaweza kupeperusha vyema B
Naye kwa upande Katibu wa ACT WaaJimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda alisema
kwamba wapo kwenye maandalizi ya uchaguzi kama chama hicho Taifa kilipotangaza
kwamba zoezi la kuchukua fomu kutoka Aprili 18 mwaka huu mpaka 31 mwezi Mei
katika nafasi za Ubunge na Udiwani.
Alisema kwamba katika uchaguzi huo wamejipanga kwamba
wagombea watakao wapitisha katika kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo hilo
watakuwa imara kuhakikisha wanapeperusha vyema bendera hiyo.
Mwisho.
EmoticonEmoticon