Mzee mwenye umri wa miaka 75 ashikiliwa na polisi kwa tuhumza na bangi Pemba

May 28, 2015

downloadNa Masanja Mabula -Pemba 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linamshikilia mzee mwenye umri wa miaka 75 akikabiliwa na tuhuma ya kupatikana na majani makavu yanayosadikiwa kuwa ni bangi .
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Shekhan Mohammed Shekhan amemtaja mzee huyo kuwa ni Hamad Hamad Bakar Mkaazi wa Mchangamdogo Wilaya ya Wete .
Amesema kuwa mzee huyo amepatikana akiwa na nyongo 75 na mafurushi mawili ya majani makavu yanayo sadikiwa kuwa ni bangi baada ya kufanyiwa upekuzi ndani ya nyumba yake .
Ameeleza kwamba tukio hilo limetokea juzi  na kuongeza kuwa walipokea taarifa juu ya uwepo kwa bangi katika nyumba ya mzee huyo kutoka kwa Polisi Jamii ambao waliambatana nao kufanya upekuzi ndani ya nyumba hiyo .
Aidha Kamanda Shekhan amesema kuwa jeshi hilo kwa sasa linaendelea kumhoji mzee huyo na atafikishwa mahakamani upelelezi utakapo kamlika kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili .
“Ni kweli kwamba jeshi la Polisi linamshikilia mzee Hamad Hamad Bakar baada ya kukamatwa akiwa na nyongo 75 pamoja na mafurushi mawili ya majani makavu yanayosadikiwa kuwa ni bangi na tutamfikisha mahakamani upelelezi utakapo kamilika ” alifahamisha Kamanda .
 Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi polisi Jamii katika Shehia hiyo wamesema kuwa bado vyombo vya sheria ikiwemo Mahakama hazijakuwa tayari kushirikiana na polisi kwani mzee huyo ameshakamatwa mara nyingi lakini kesi zake hazipatiwa hukumu stahili
Wamesema kuwa mzee huyo anaugonjwa wa Ukoma  ni mzoefu wa biashara hiyo na kwamba amewahi kukamatwa na kufikishwa mahakamani zaidi ya mara moja lakini hakuna adhabu iliyochukuliwa dhidi yake .
“Hatuwezi kufanikisha udhibiti na utumiaji wa dawa za kulevya iwapo watuhumiwa wanashindwa kuchukuliwa hatua kwani huyu mzee si mara ya kwanza kukamatwa na bangi lakini hakuna adhabu iliochukuliwa dhidi yake ” alifahamisha Kiongozi wa Polisi Jamii .
Hivyo wameviomba vyombo vya sheria kuhakikisha kwamba wanachukua hatua inayostahili ili kukomesha biashara hii haramu ya madawa ya kulevya kwa lengo la kuwalinda vijana dhidi ya majanga mbali mbali .

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »